Nakuonea huruma John Magufuli

Nakuonea huruma John Magufuli

Dingswayo

JF-Expert Member
Joined
May 26, 2009
Posts
4,019
Reaction score
2,930
Ni hivi majuzi tulisikia habari kuhusu kuzolewa na mvua kwa daraja la Singida lililokuwa kwenye barabara ya lami mpya. Habari hiyo ilizua mjadala humu jamvini vilevile na wadau kadhaa kuchangia:

https://www.jamiiforums.com/jukwaa-la-siasa/378518-ccm-hizi-ndio-barabara-mnazotambia.html
Habari hii iliyoandikwa kwenye gazeti nayo inaongelea jambo hilo kwa kirefu na athari za kutegemea barabara hizo zenye kiwango cha chini:


Kama kuna waziri ninayemhurumia sana kwenye Baraza la Mawaziri lililoundwa na Rais Jakaya Kiwete, basi ni John Magufuli aliyetwishwa majukumu mazito ya kutandika mkeka kwenye barabara zote hapa nchini.

Namhurumia Waziri Magufuli kwa kuwa hawezi kabisa kufikia ndoto zake za kuifanya Tanzania ing'are kwenye medani za kimataifa kama nayo ni moja ya nchi maskini inayojitutumua katika ujenzi wa barabara za lami.

Kwangu mimi naziita barabara za mkeka kwa kuwa zinafanya kazi ya kuanika unga wa muhogo ukisha kauka thamani ya mkeka huishia hapo, unakunjwa na kuwekwa kwenye kona ya chumba ili kusubiri unga mwingine na wanaofaidi unga huo hukumbuka mkeka siku unga ukiisha.

Leo nataka niseme na Dk. Magufuli najua ni mmoja wa mawaziri wachapa kazi kweli kweli lakini kwa bahati mbaya amefungwa kitambaa cheusi usoni hajui hatima ya barabara zetu na mwisho wake ni nini.

Bahati nzuri waziri huyo amekuwa bingwa wa kuwa na takwimu za kutosha za kile kinachoendelea kuhusu ujenzi wa barabara zote hapa nchini, akiimba moja baada ya nyingine na majina ya wakandarasi anayataja mithiri ya watoto wake.

Dk. Magufuli pia ni bingwa wa kujua na kukariri shughuli karibu zote zinazofanywa na wizara yake na naweza kusema ni mmoja wa mawaziri aliyefanikiwa kuzigusa na kuzikoga nyoyo za marais alimgusa Rais wa awamu ya tatu, Benjamin Mkapa na sasa anaendelea kukonga nyoyo za Rais Jakaya Kikwete kila linapotokea tukio la uzinduzi wa barabara na madaraja.

Pia huzikonga nyoyo za wananchi ambao kwa bahati nzuri miradi ya barabara imefanikiwa kupita katika maeneo yao licha ya upande wa pili wananchi wameumizwa na sheria ya akiba ya barabara na kuonekana kuwa kero kubwa kwao kwa kila aliyejenga jirani na barabara.

Huko sitaki kuingilia sana najua kuwa uamuzi wa kuwepo kwa upana wa kiasi gani kutoka upande mmoja wa barabara hadi mwingine si maamuzi ya Waziri Magufuli ni maamuzi ya sheria zilizopitishwa na Bunge ili kuwa na barabara zenye viwango hilo halina ubishi.

Namhurumia Dk. Magufuli kwa kuwa jitihada za kuimba takwimu na idadi ya barabara zinazoendelea kujengwa, madaraja na vivuko kazi hiyo kwa ujumla wake si rahisi kwenye nchi inayojaribu kujiondoa kwenye lindi la umaskini wa kujitakia na kufikiria kuwa siku moja Tanzania itakuwa miongoni mwa nchi tajiri.

Sawa barabara zetu zinaendelea kujengwa kwa kasi, zinatofautiana kwa viwango na ubora kutokana na aina ya makandarasi waliopatikana na wao pia wanatofautiana kwa dhana za kazi na utaalamu kutoka nchi moja kwenda nyingine kulingana na namna walivyopatikana.

Hilo la makandarasi nalo siliingilii sana kwa kuwa nafahamu jinsi Wakala wa Barabara hapa nchini (TANROADS) ni mabingwa pia wa kutoa zabuni za ujenzi wa barabara na madaraja kwenye makampuni yenye sifa ndiyo maana barabara zetu hazidumu kwa muda mrefu.

Kwa nini barabara zetu licha ya kuwa na wataalamu wenye sifa na makandarasi wa kimataifa, iweje zianze kuharibika kabla nyingine hazijazinduliwa, ni nini kinachosababisha barabara ziwe mbovu kwa muda mfupi? Hapo ndipo ninapoanza kumuonea huruma Waziri Magufuli.

Sasa tatizo nini na kwa nini leo hii nimuonee huruma Dk. Magufuli na barabara zake? Hivi kwa nini nimuonee huruma na madaraja yanayojengwa kutoka Tunduma hadi Sumbawanga? Kuna nini hapo? Pole sana Magufuli.

Nakupa pole kwa kuwa hujui kuwa umefunikwa kitambaa cheusi usoni, pengine hajui kuwa mkeka unaondelea kuuanika wanaokula unga ni wengi. Hawajui thamani ya mkeka na hawajui mtu aliyeusuka mkeka huo ndiyo maana ukitumika kuanika unga haijulikani lini utakumbukwa.

Sasa nikuambie kuwa watu wanaoharibu barabara zetu zinazojengwa kwa gharama kubwa si wengine ni wamiliki wa malori makubwa ya mizigo, naweza kusema kuwa adui mkubwa wa barabara za Watanzania ni magari makubwa ya mizigo.

Utafiti nilioufanya katika barabara zote kuu, tatizo kubwa la uharibifu wa barabara na madaraja ni magari makubwa ya mizigo, hakika hatuwezi kufika popote kwa mwendo huu wa kupitisha kwa siku magari zaidi ya 5,000 kutoka Dar es Salaam hadi Tunduma, kutoka Dar es Salaam hadi Arusha, kutoka Dar es Saalam hadi Mwanza.

Kila barabara hapa nchini zinaumizwa kwa kiasi kikubwa na uzito wa magari hayo yanayobeba bidhaa mbalimbali kutoka ndani ya nchi na nje, mizani zinazoendelea kujengwa hazisaidii kitu, hazizuii magari makubwa ya mizigo kupita.

Mizani za barabarani zimekuwa kero kubwa kwa mabasi ya abiria wanapita, kwenye mizani kwa uzito wa tani 10 hadi 18 huku malori yakiwa yanapitisha mizigo ya uzito kati ya tani 60 hadi 70. Kwa jibu la haraka ni magari ya aina gani yanayostahili kupita kwenye mizani?

Kama tumegundua au nimegundua kuwa adui mkubwa wa barabara ni magari makubwa ya mizigo, hiyo mizani imejengwa kwa ajili ya kupima nini, barabara karibu zote zinazounganisha mkoa na mkoa haziwezi kudumu kwa kuwa utitiri mkubwa wa magari ya mizigo si mkombozi wa barabara zetu.

Nakuonea huruma Dk. Magufuli kwa kuwa tumeua reli zetu ili tufanye biashara ya usafirishaji kwa njia ya barabara, madhara yake ni makubwa zaidi kwa nchi inayojaribu kujikomboa kiuchumi kama Tanzania, hatuwezi kufika popote pale kwa hasara kubwa inayofanywa na magari hayo.

Angalia jinsi mizigo mizito inavyosafirishwa kwa njia ya barabara inavyochangia kuharibu na kutia hasara ambazo Dk. Magufuli inawezekana haoni kuwa nyingi zimegeuka kuwa na vibiyongo, zina nundu na mashimo yasiyoweza kuzibwa.

Kwenye miinuko ya milima na miteremko barabara za lami zimeshindwa kuhimili uzito wa mizigo, zinagawanyika katikati hali ambayo inahatarisha zaidi usalama wa abiria wanaosafiri kwenye mabasi, maeneo kama hayo ni hatari lazima mabasi na magari madogo yahame njia na mengine mengi yamekuwa yakipata ajali.

Kuna maana gani ya kuzidi kuruhusu shaba nzito kutoka Zambia kuja Bandari ya Dar es Salaam isafirishwe kwa njia ya barabara wakati Reli ya Tazara ipo? Kuna sababu gani ya kusafirisha mbao kutoka Malawi hadi Dar es Salaam wakati reli hiyo ipo.

Kuna sababu gani ya kusafirisha saruji kutoka Tanga kwa magari mazito ya mizigo wakati reli ipo? Kuna sababu gani ya kusafirisha saruji kutoka Mbeya hadi Dar es Salaam kwa malori huku mabehewa ya kubebea mizigo yakiendelea kuota kutu? Ni nini kipo nyuma ya pazia kuhusu malori hayo?

Dk. Magufuli utajenga barabara ngapi zinazoendelea kuharibika kila siku huku ukijua kuwa reli zipo? Unawajua vizuri wamiliki wa magari hayo? Nini siri ya biashara hiyo ya usafirishaji kwa njia ya barabara? Nakuonea huruma kwa kuwa tambo na takwimu zinazomfurahisha rais si suluhu ya matatizo ya wananchi na mustakabali wa uchumi wa nchi.

Sura yako ya ucheshi na ukarimu ielekeze kwa waziri mwenzako wa uchukuzi, Dk Harrison Mwakyembe, mwambie: "Safirisha mizigo mizito kwa reli, meli na ndege, barabara zangu zinaumia, zinabomoka, mbona hunionei huruma?" Mwambie Mwakyembe akuonee huruma, huwezi kufika popote, malori haya ni balaa kwa uchumi wa nchi. Kama ndio ufahari mwambie Rais Kikwete kuwa nchi inaliwa

[TD="bgcolor: #ffffff"]
Nakuonea huruma John Magufuli
Christopher Nyenyembe
[/TD]
[TD="width: 140, bgcolor: #FFFFFF, align: center"][/TD]
 
Kama marekani au kama Uchina?:target:
 
kazi ipo kweli mizani haina msaada ni bora kuyaacha magari yapite bila kukaguliwa
 
John Pombe Magufuli mzalendo ambaye Historia itamkumbuka kwa Uchapakazi na sio Politik!
 
Ingekuwa treni ni za watu binafsi bac usingeona malori barabarani maana treni inabeba mzigo mkubwa na kwa bei chee lakini kwa kuwa treni ni za serikali ndio maana zinahujumiwa ila iko siku MUNGU ataondoa haya mateso kwn kila jambo lina mwisho wake
 
poor minister among the good for nothing leaders in tanzania.
Ye amekalia serikari ya ccm na ahadi za dk Jakaya Mrisho Kikwete, na kudanganya umma kwa takwimu zake mbofu mbofu.
Sasa anapata majibu ya kazi yake.
 
dk. magufull ni mmoja wa wa2 wanaoipa ccm na nchi ahuen. hasifki kwa rushwa zaid ya ile issue ya nyumba. lait kama wangekuwepo wa2/viongoz bora naamin yey angekuwa bora zaid. mungu akujalie busara zaid
 
Hongera dr. Wangu wa ukweli johm pombe magufuli. Ni kweli ingefaa kama ukimwambia huyo dr. Mwenzio harisson mwakyembe akuonee huruma.

john pombe magufuli mzalendo ambaye historia itamkumbuka kwa uchapakazi na sio politik!
 
Magufuli hakustahili baraza jipya


picture-73.jpg

Na Nyaronyo Kicheere - Imechapwa 09 May 2012

Waraka wa Wiki
Mwanahalisi



magufuli_293.jpg



MIONGONI mwa mawaziri machachari walioteka hata nyoyo za wananchi ni Waziri wa Ujenzi, Dk. John Pombe Magufuli.
Waziri Magufuli ni mtu anayejifunza kwa haraka kazi na mazingira ya kila wizara anayopangiwa. Hii ndiyo sababu amekuwa bingwa wa kukariri vituo vya daladala, treni, viwanja vya ndege, na hata mifugo na samaki katika wizara alizowahi kusimamia.

Kukariri barabara za lami na za changarawe, zilijengwa lini na nani na kwa gharama gani ndipo kumempa sifa na umashuhuri, lakini yanayofanyika katika wizara yake yanatisha.
Hata hivyo, rais makini, anayefuatilia utendaji kazi wa mawaziri katika kila wizara, angemwajibisha siku nyingi Dk. Magufuli kwa kushindwa kuzuia wizi, ubadhirifu au kutoa maagizo yaliyolisababishia taifa hasara kubwa.
Katika baraza hilo jipya ambalo aliyeteua anatuaminisha kwamba ni zuri kuliko lile la akina William Ngeleja, Omar Nundu, Mustapha Mkullo, Haji Mponda, Cyril Chami, Ezekiel Maige itabidi tujiulize kwa kigezo gani?
Kama ni ubadhirifu, wizi na udanganyifu Wizara ya Ujenzi ni nambari moja. Hii ndiyo wizara iliyonunua ile meli au boti maarufu pale Magogoni iitwayo MV Magendo ingawaje ubavuni imeandikwa RESCUE, yaani UOKOZI.

Boti hii ilinunuliwa enzi zile Magufuli akiwa Waziri wa Ujenzi chini serikali ya awamu ya tatu iliyoongozwa na Rais Benjamin Mkapa. Hadi leo boti ile iliyonunuliwa kwa fedha za kigeni haijafanya kazi.
Ilipofika kwenye fukwe za Tanganyika boti hiyo ikawa inatumika kuchota na kufyonza mafuta kwenye meli na boti zingine bandarini na kuyauza kwa wavuvi, ndiyo maana ikaitwa MV Magendo.

Baada ya muda kidogo boti hiyo ikapwelezwa kwenye mchanga ambako hadi leo haifanyi kazi ya kuokoa kama tulivyotangaziwa siku ya uzinduzi kwenye kivuko cha kuelekea Kigamboni.
Bahati mbaya si wafanyakazi wa wakala wa vivuko au serikali wanaohoji aliyehusika kuagiza boti mbovu isiyofanya kazi wala kudai wahusika waitengeneze boti hiyo ili iweze kuwadumia wananchi.
Si hivyo tu, hakuna hata mfanyakazi mmoja kuanzia watendaji serikalini hadi wakala wa vivuko aliyepewa adhabu. Hata Waziri Magufuli hakuwajibishwa kwa hilo na sasa yumo kwenye baraza jipya.

Ubadhirifu mwingine uliofumbiwa macho katika wizara hiyo ni juu ya uagizaji, ununuzi na ufungaji mitambo ya kukatia tiketi kwenye kivuko cha kigamboni ambayo haikuwahi kufanya kazi tangu inunuliwe miaka yapata sita au saba iliyopita.
Sisi tunaokaa Kigamboni tunakumbuka vizuri sana jinsi serikali ilivyotutangazia kuwa wafanyakazi Kivukoni ni wezi sana na kwamba wanaiba mapato hivyo ikasema imekuja na mbinu mpya ya kukomesha wizi huo wa mapato – ikanunua wa mitambo ya kukatia tiketi.

Mitambo iliagizwa kwa pesa za kigeni, ikafungwa pale Kivukoni upande wa Magogoni na kusababisha milango miwili ya wapita kwa miguu kufungwa kwa miaka yote sita sasa.
Mitambo haitumiki, haitengenezwi na wala haiondolewi licha ya kusababisha kero ya msongamano kwa wasafiri kulazimika kupita mlango mmoja uliobaki.
Japokuwa hakuna ushahidi wa Magufuli kuhusika moja kwa maoja katika ununuzi wa boti mbovu na mitambo chakavu ya kukatia tiketi, alipaswa kuwashtaki wahusika au yeye mwenyewe kuwajibishwa kutokana na makosa ya waliochini yake. Magufuli hakuwajibishwa.

Lakini hakuna atakayebisha Magufuli alivyohusika kupigia debe uuzwaji wa nyumba za serikali bila kujali gharama ya maeneo nyumba hizo zilipokuwa zimejengwa.

Mbaya zaidi baadhi ya watu waliouziwa nyumba hizo hawakustahili kwani hawakuwa watumishi wa serikali. Kwa nini Magufuli hakuwajibishwa?
Wauzaji nyumba walitoa kigezo kwamba anayestahili kuuziwa nyumba hizo lazima awe mfanyakazi tu wa serikali ya muungano. Kigezo hicho hakikuzingatiwa.

Hii si mara ya kwanza habari hizi kuandikwa. Wakati zilipoandikwa magazetini yapata miaka minne iliyopita si Magufuli aliyejali wala mamlaka iliyomteua. Mpaka leo hajawajibishwa.
Dk. Magufuli pia aliagiza kuvunjwa kituo cha mafuta jijini Mwanza na kuliingiza taifa katika mgogoro mkubwa ambao uliishia mahakamani na serikali ikatakiwa kulipa mamilioni ya shilingi. Magaufuli hakuwajibishwa.
Kituo cha mafuta kimejengwa ndani ya mipaka ya jiji la Mwanza kwa vibali vya uongozi wa jiji. Lakini badala ya Magufuli kufuata taratibu za kisheria za kuchukua eneo la mtu binafsi alitumia mabavu na jazba huku akidai anatekeleza sheria.

Dk. Magufuli pia alilazimisha kuvunjwa nyumba katika barabara ya Morogoro pale Ubungo na Kimara mwaka 1997 na kuliingiza taifa katika mgogoro na raia wake na kuisababishia serikali hasara ya Sh. 65 milioni. Magufuli hakuwajibishwa.
Kwa bahati nzuri kwa upande wa serikali wakazi wa Ubungo - Kimara walikuwa mbumbumbu hawakwenda mahakamani kudai fidia ya mamilioni ya shilingi baada ya kuelewa vibaya hukumu ya maombi yaliyowasilishwa na wakili wao Profesa Mgongo Fimbo ndiyo maana hawakwenda mahakamani kudai.

Mmoja wa raia hao ambaye alilielewa vizuri shauri hilo Bw. Ebeneza Massawe, alikwenda mahakamani na kushinda kesi. Alilipwa na serikali Sh. 65 milioni.

Je, wote waliovunjiwa nyumba zao Ubungo na Kimara wapatao zaidi ya 350 wangefika mahakamani kudai fidia, serikali ingelipa kiasi gani?
Ikiwa mawaziri sita waliotemwa, Rais Jakaya Kikwete amesema ni uwajibikaji wa kisiasa, kwa rekodi hii ya usimamizi wa Dk. Magufuli alipaswa kuwajibishwa kwa kuondolewa kwenye baraza la mawaziri mara moja kwa sababu hatufai.


John Pombe Magufuli mzalendo ambaye Historia itamkumbuka kwa Uchapakazi na sio Politik!
 
Pamoja na yote bdo Watanzania wengi wana imani naye,wapuuzi wachache wanajaribu kumuangusha
 
poor minister among the good for nothing leaders in tanzania.
Ye amekalia serikari ya ccm na ahadi za dk Jakaya Mrisho Kikwete, na kudanganya umma kwa takwimu zake mbofu mbofu.
Sasa anapata majibu ya kazi yake.
Bado uko hai mkuu?
 
Back
Top Bottom