Nahitaji msaada wa kuandika upya Kitabu

MwanaWA Ebrania

JF-Expert Member
Joined
Oct 6, 2017
Posts
939
Reaction score
1,147
Ndugu zangu wana (JF) na watanzania kwa ujumla.

Mimi kijana wenu, naitwa James Yustar.

Natanguliza msamaha kwa yeyote atakayekwazika kwa namna moja ama nyingine sikio lake kusikia habari mbaya.. Kwa maana simulizi yangu sio nzuri masikioni mwa wenye hekima[emoji120]

Ila naomba nitajitahidi kuandika kwa ufupi ili tu' kupata picture nzuri nachotaka kuwakilisha kwenu, kama sitaeleweka mwenye swali ataniuliza nami nitamjibu.

Hiko hivii; kabla ya kuwa kijana nilikuwa mtoto mchanga, niliyetupwa kama kifurishi cha taka kilichoviringishwa ndani ya box. Ila kwa msaada na huruma nyingi za mwenyezi mungu, niliokotwa na mama msamalia mwema aitwaye (yusta) ndio maana naitwa james yustar.

Mamaangu mpendwa alinilea mpaka nilipofika umri wa miaka 7. Kwa bahati mbaya alifariki dunia... Baada ya kufariki kwa mamaangu mlezi, maisha yangu yakawa ni magumu yenye maumivu makali sana... Hivyo ndugu wenye tamaa ya mali walitaka hata kuniuwa. Hivyo kuanzia hapo nikaanza rasmi kuishi maisha ya mtaani.

Robo 3 ya maisha yangu nimeyaishi mtaani, yaani (maisha ya kichokoraa) kama wengine wanavyotuita.

Kwa leo siwezi kuyaongelea maisha ya mtaani kwa mapana ama ufupi, kwa sababu sio siku yake.

Leo nimekuja kwenu ninaombi moja tu'

Kijana wenu nahitaji msaada wa kuandika upya kitabu cha (maisha halisi ya mtoto wa mtaani)

Ambacho kwa sasa nimeandika kwa lugha hisiyo rasmi sana. (lugha ya mtaani zaidi)

Ambayo baraza la kiswahili (bakita ) wanataka nirekebishe na kukipanga kitabu upya, ili kiweze kutumika ktk mifumo ya mitaara na kama liwaya vyuoni.

Vile vile pia ninaomba kwa yeyote mwenye kuweza kunisaidia ku-translate kitabu kwa lugha ya kiingereza nitashukuru saana.

Binafsi sina pesa ya kumlipa wala sina chochote cha kumzawadia ila mungu mkuu atamlipa huyo mtu kwa kazi atakayofanya.

Lengo kuu ni kupeleka ujumbe kwa jamii.

Ili kupunguza, ama kutokomeza kabisa wimbi la watoto waishio mtaani (mazingira hatarishi)....



Kwa kuitimisha;

Naomba niwashukuru nyooote mtakaoguswa kufanya chochote ktk ombi langu hili.



Ktk bandiko hili, nitaambatanisha picture za kitabu cha sasa cha (maisha halisi ya mtoto wa mtaani)







Sent from my infinix x657 using jamiiforums mobile app
 
Hizi picture nikiwa na VIJANA wenzangu ambao nimeishinao mtaani
Kwa miaka mingi tangu nikiwa mdogo.
Na hapa kuna picha ya KITABU CHA MAISHA HALISI YA MTOTO WA MTAANI
Pamoja na hayo kuna picture ambayo nipo na kaka mkubwa Dr Isaac Maro
Pamoja na picture ya Logo ya taasisi ya jamesfoundation2@gmail.comView attachment 1946978View attachment 1946976View attachment 1946977View attachment 1946979View attachment 1946981View attachment 1946980View attachment 1946982View attachment 1946983

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…