Mkuu nakuunga mkono kwa asilimia mia moja, cdm wasimame kama chama pekee na mgombea awe Tundu Lissu. Ni ukweli usioacha shaka kuwa Lissu ana mvuto na uwezo mkubwa wa kujenga hoja, huyu ndio mgombea pekee anayeweza kunifanya nipige kura, na ndiye mgombea anayeweza kurudisha hamasa ya siasa iliyouliwa na Magufuli kwakuwa hawezi siasa za ushindani. Huyu ndiye mgombea wa upinzani anayeweza kuamsha hamasa ya umma kudai tume huru ya uchaguzi na katiba mpya. Jambo pekee watakaloweza ccm ni kumfunga jela na sio zaidi ya hilo.