Mzazi/Mlezi unamlindaje mwanao Mtandaoni?

Mzazi/Mlezi unamlindaje mwanao Mtandaoni?

Wild Flower

JF-Expert Member
Joined
Jul 20, 2023
Posts
857
Reaction score
1,653
ZINGATIA HAYA KUMLINDA MWANAO MTANDAONI

1731053584815.png

1. Mzazi/Mlezi ongea na mtoto kwa kumfundisha kuhusu matumizi sahihi ya kifaa cha kidigitali kama vile simu au kompyuta

2. Mzazi mpatie mtoto miongozo ya kutumia Mitandao ya Kijamii, mwelekeze maudhui anayoweza kuweka na watu anaoweza kuchangamana nao Mtandaoni

3. Mzazi/Mlezi weka mipaka ya mambo ambayo mtoto anaweza kuyafanya mtandaoni au katika Kifaa chake cha Kidijitali.

4. Mzazi/Mlezi kuchuja maudhui yasiyofaa kwa kutumia programu maalumu (parental control programs) kwenye vifaa vya mwanao.

5. Mzazi/Mlezi mfundishe mtoto namna ya kulinda taarifa binafsi. Mwelekeza athari anazoweza kupata kwa kuchapisha mtandaoni taarifa hizo

6. Muhamasishe mtoto wako kutoa taarifa kwako endapo atakutana na tatizo lolote mtandaoni.
 
Ni elimu ya muhimu sana kwa watoto wetu wa sasa uwe umemnunulia simu ama la. Nasema hivyo kwa sababu gani wewe kama mzazi unawea kuwa hujamnunulia kwa sababu mbili. Moja ni kwa sababu huna uwezo na ya pili huoni umuhimu wa mtoto wako kuwa nao vifaa hivi kwa wakati huo.

Uzuri wa kumpa elimu hiyo ni kwavile shule wanaweza kuwa na vifaa hivi na wanatumia, marafiki zao wanawea kuwa nao na hata kuna sehemu hizi za kuperuzi maarufu kama cybercafé.

Mtoto akiwa amepata elimu hii itamsaidia hata akikutana na challenge yoyote kama wale watu wazima wanao kaa mitandaoni na kupenda kuchat na watoto wadogo na kuwadanganya wakutane nao, kuwaongelesha mambo ya mapenzi na yasiyo na maadili, kuwaambia wawatumie picha cha utupu ama hata wao kuwatukia picha ama hata kuwaonyesha miili yao wakiwa bila nguo moja kwa moja kutumia video calls, mtoto akishapata elimu hii na umwambie ikiyokea jambo lolote kati ya hayo na lingine lolote ampe taarifa mzazi mlezi ama hata mwalimu.

Na pia ajaribu kuto chat na mtu yoyote usie mjua mtandaoni. Itazuia kwa kiasi kikubwa kumlinda mwanao.
 
Back
Top Bottom