kitambiheshima
JF-Expert Member
- May 27, 2013
- 452
- 116
1: ufisadi; mpango uliolenga kuichonganisha serikali ya ccm na wananchi. Mpango umeshindwa na hausikiki tena.
2: Nchi kutotawalika; mpango huu ulilenga kuwatia hasira wananchi mara baada ya uchaguzi mkuu 2010 ili waikatae serikali ya ccm kupitia mpango wa kutotii sheria na baadae mapinduzi. Mpango huu ulitekelezwa kwa matamko ya mfululizo yasiyo na tija dhidi ya serikali, uchochezi wa kuihusisha serikali na maovu mbalimbali yakiwemo mauaji ya raia n.k. Mpango huu nao ulishindwa kutokana na serikali ya ccm kuyatambua malengo ya mpango huo hivyo kuchukua tahadhari kwa umakini.
3: Kuiga mpango wa machafuko Libya, Tunisia na Misri: Mpango huo uliigwa na chadema kwa kuendesha maandamano nchi nzima wakidhani kuwa ingeweza kuwa njia rahisi ya wao kuingia ikulu. Mpango huu ulishindwa kwa kuwa haukuwa mwafaka na wenye tija kwa watanzania. Yaliyokuwa yakizikabili nchi hizo tatu na hasa influence za kiuchumi kwa mataifa ya magharibi hazikufanana na za TZ. Hivyo mpango huo ulikufa kifo cha mende.
4: Migomo ya w.kazi na wnfunzi vyuo vikuu: Chadema kilitumia mbinu ya kuwafarakanisha w.funzi vyuo vikuu na w.kazi na serikali. Kwa w.kazi walitumia kigezo cha mishahara na kwa w.funzi walitumia kigezo cha mikopo na fedha za kujikimu. Katika hoja zao walidai kuwa ccm ndiyo inayokwamisha maboresho ya maslahi yao. Mbinu hiyo ilifanikiwa kwa muda mfupi kwani ni kweli wafanyakazi na wanafunzi waliichukia serikali ya ccm na kuiadhibu vikali wakati wa uchaguzi mkuu. Hata hivyo hila hiyo kwasasa haina nguvu na imeshindwa kabisa kwani wanafunzi na wafanyakazi wamekwishabaini hila za chadema katika kuwatumia wao kama daraja la kufamikishia malengo yao ya kisiasa.
5: Operations sangara, m4c n.k: Operations hizi ziliambatana na vitendo viovu vya ma..u...aji kwenye mikutano. Kwa mazingira tata ya mauaji (ukiondoa la Mwangosi) katika mikutano hiyo mtu yeyote mwenye akili timamau unabaini kuwa mauaji hayo yalikuwa yakipangwa na chadema wenyewe ili kuuhadaa ulimwengu kuwa ccm ndiyo inafanya mauaji hayo. Mifano iliyopo ni mauaji ya muuza magazeti Morogoro, mauaji Igunga, mauaji huko Arusha na matukio tata ya milipuko ya mabomu Mwanza. Mbinu hii imeonekana kushindwa kwakuwa watanzania wamewashtukia. Hata hivyo mbinu hii inaonekana kutaka kubadilishwa. Tumeshuhudia juzi kiongozi wa Tahiliso huko Mwanza eti alitekwa na badae kuachiwa bila kudhuriwa!.
6: Uchonganishi wa kidini: Yaliyotokea huko kanda ya ziwa wakati waislamu na wakristu wakigombea kuchinja, yana sura ya kisiasa na yalisukwa kwa ustadi wa hali ya juu. Lengo la mpango huu lilikuwa kuwafarakanisha waislamu na wakristu na kikubwa kilicholengwa kilikuwa ni kuibua vita ya udini ili mchi isitawalike kama ilivyokuwa imeahidiwa. Tunamshukuru Mungu hilo nalo lilishindwa.
7: Kushadidia upande wa maadui- mgogoro wa malawi/Rwanda vs Tanzania: Siyo siri, wakati mgogoro huo umepamba moto ilitushangaza tulio wengi kuona baadhi ya viongozi wa chadema wakitoa matamko yaliyoonesha kubeza msimamo wa serikali katika kutetea maslahi ya nchi. Baadhi yao walisikika wakishabikia kuwa eti malawi ilikuwa na haki kwenye mpaka huku wengine wakishabikia na kuwatisha watz kuwa PAKA ana nguvu kubwa ya kijeshi hivyo angetutwanga. Ilinishangaza sana. Hata hivyo ushabiki huo haukuungwa mkno na.watz hivyo haukuwa na madhara yoyote kwa taifa.
8: UKAWA: Mbinu iliyopo mikononi.mwa chadema (kwa ulaghai wa kuvishirikisha vyama vingine) kwa sasa ni huo unaoitwa Umoja wa Katiba ya Wananchi. Lengo la umoja huo unaelezwa kuwa ni kutetea mapendekezo ya Warioba kuwa ndiyo mawazo sahihi ya wananchi. Wameibeba agenda hiyo wakiamini kuwa ndiyo kete yao ya mwisho. Wanaamini kuwa mapendekezo ya Warioba si rafiki kwa Muungano hivyo wamewalaghai CUF na NCCR kuwa kwa mapendekezo hayo yatawawezesha "kugawana madaraka", CUF ikichukua Zanzibar na CHADEMA bara "tanganyika". Katika hili wanajua madhara ya kuuvunja/kuudhoofisha muungano lakini kwasababu ya madaraka tu wamepiga haidhuru!.
My take: chadema wana mipango mingi isiyo na dhamira njema kwa mstakabali wa Tanzania. Wameamua kufanya lolote alimradi liwaingize Ikulu. Ninawapongeza baadhi ya viongozi na wanachama.wa chadema ambao kila mmoja kwa wakati wake wanaendelea kubaini uovu ulioko ndani ya chama hicho na hivyo wanajitoa na kuhamia vyama vingine vya siasa.
Niwaombe chadema kuwa, waendeshe siaasa zao huku wakiongozwa na uzalendo na mapenzi kwa nchi yao na watanzania wenzao. Waache siasa za kilaghai za kuwaonesha wananchi kuwa wao ndiyo watetezi wao huku nyuma ya pazia wao ndiyo wabaya wao.
2: Nchi kutotawalika; mpango huu ulilenga kuwatia hasira wananchi mara baada ya uchaguzi mkuu 2010 ili waikatae serikali ya ccm kupitia mpango wa kutotii sheria na baadae mapinduzi. Mpango huu ulitekelezwa kwa matamko ya mfululizo yasiyo na tija dhidi ya serikali, uchochezi wa kuihusisha serikali na maovu mbalimbali yakiwemo mauaji ya raia n.k. Mpango huu nao ulishindwa kutokana na serikali ya ccm kuyatambua malengo ya mpango huo hivyo kuchukua tahadhari kwa umakini.
3: Kuiga mpango wa machafuko Libya, Tunisia na Misri: Mpango huo uliigwa na chadema kwa kuendesha maandamano nchi nzima wakidhani kuwa ingeweza kuwa njia rahisi ya wao kuingia ikulu. Mpango huu ulishindwa kwa kuwa haukuwa mwafaka na wenye tija kwa watanzania. Yaliyokuwa yakizikabili nchi hizo tatu na hasa influence za kiuchumi kwa mataifa ya magharibi hazikufanana na za TZ. Hivyo mpango huo ulikufa kifo cha mende.
4: Migomo ya w.kazi na wnfunzi vyuo vikuu: Chadema kilitumia mbinu ya kuwafarakanisha w.funzi vyuo vikuu na w.kazi na serikali. Kwa w.kazi walitumia kigezo cha mishahara na kwa w.funzi walitumia kigezo cha mikopo na fedha za kujikimu. Katika hoja zao walidai kuwa ccm ndiyo inayokwamisha maboresho ya maslahi yao. Mbinu hiyo ilifanikiwa kwa muda mfupi kwani ni kweli wafanyakazi na wanafunzi waliichukia serikali ya ccm na kuiadhibu vikali wakati wa uchaguzi mkuu. Hata hivyo hila hiyo kwasasa haina nguvu na imeshindwa kabisa kwani wanafunzi na wafanyakazi wamekwishabaini hila za chadema katika kuwatumia wao kama daraja la kufamikishia malengo yao ya kisiasa.
5: Operations sangara, m4c n.k: Operations hizi ziliambatana na vitendo viovu vya ma..u...aji kwenye mikutano. Kwa mazingira tata ya mauaji (ukiondoa la Mwangosi) katika mikutano hiyo mtu yeyote mwenye akili timamau unabaini kuwa mauaji hayo yalikuwa yakipangwa na chadema wenyewe ili kuuhadaa ulimwengu kuwa ccm ndiyo inafanya mauaji hayo. Mifano iliyopo ni mauaji ya muuza magazeti Morogoro, mauaji Igunga, mauaji huko Arusha na matukio tata ya milipuko ya mabomu Mwanza. Mbinu hii imeonekana kushindwa kwakuwa watanzania wamewashtukia. Hata hivyo mbinu hii inaonekana kutaka kubadilishwa. Tumeshuhudia juzi kiongozi wa Tahiliso huko Mwanza eti alitekwa na badae kuachiwa bila kudhuriwa!.
6: Uchonganishi wa kidini: Yaliyotokea huko kanda ya ziwa wakati waislamu na wakristu wakigombea kuchinja, yana sura ya kisiasa na yalisukwa kwa ustadi wa hali ya juu. Lengo la mpango huu lilikuwa kuwafarakanisha waislamu na wakristu na kikubwa kilicholengwa kilikuwa ni kuibua vita ya udini ili mchi isitawalike kama ilivyokuwa imeahidiwa. Tunamshukuru Mungu hilo nalo lilishindwa.
7: Kushadidia upande wa maadui- mgogoro wa malawi/Rwanda vs Tanzania: Siyo siri, wakati mgogoro huo umepamba moto ilitushangaza tulio wengi kuona baadhi ya viongozi wa chadema wakitoa matamko yaliyoonesha kubeza msimamo wa serikali katika kutetea maslahi ya nchi. Baadhi yao walisikika wakishabikia kuwa eti malawi ilikuwa na haki kwenye mpaka huku wengine wakishabikia na kuwatisha watz kuwa PAKA ana nguvu kubwa ya kijeshi hivyo angetutwanga. Ilinishangaza sana. Hata hivyo ushabiki huo haukuungwa mkno na.watz hivyo haukuwa na madhara yoyote kwa taifa.
8: UKAWA: Mbinu iliyopo mikononi.mwa chadema (kwa ulaghai wa kuvishirikisha vyama vingine) kwa sasa ni huo unaoitwa Umoja wa Katiba ya Wananchi. Lengo la umoja huo unaelezwa kuwa ni kutetea mapendekezo ya Warioba kuwa ndiyo mawazo sahihi ya wananchi. Wameibeba agenda hiyo wakiamini kuwa ndiyo kete yao ya mwisho. Wanaamini kuwa mapendekezo ya Warioba si rafiki kwa Muungano hivyo wamewalaghai CUF na NCCR kuwa kwa mapendekezo hayo yatawawezesha "kugawana madaraka", CUF ikichukua Zanzibar na CHADEMA bara "tanganyika". Katika hili wanajua madhara ya kuuvunja/kuudhoofisha muungano lakini kwasababu ya madaraka tu wamepiga haidhuru!.
My take: chadema wana mipango mingi isiyo na dhamira njema kwa mstakabali wa Tanzania. Wameamua kufanya lolote alimradi liwaingize Ikulu. Ninawapongeza baadhi ya viongozi na wanachama.wa chadema ambao kila mmoja kwa wakati wake wanaendelea kubaini uovu ulioko ndani ya chama hicho na hivyo wanajitoa na kuhamia vyama vingine vya siasa.
Niwaombe chadema kuwa, waendeshe siaasa zao huku wakiongozwa na uzalendo na mapenzi kwa nchi yao na watanzania wenzao. Waache siasa za kilaghai za kuwaonesha wananchi kuwa wao ndiyo watetezi wao huku nyuma ya pazia wao ndiyo wabaya wao.