Mwenyekiti wa CCM Rufiji apigwa risasi na kufariki dunia

R.B

JF-Expert Member
May 10, 2012
6,296
2,573

Mbunge wa Rufuji Mohamed Mchengerwa.


MWENYEKITI wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) tawi la Mparange na mjumbe wa serikali ya kijiji cha Ikwiriri Kaskazini, wilayani Rufiji mkoani Pwani, Michael Lukanda, ameuawa kwa kupigwa risasi ya kichwani na watu wasiojulikana.

Watu hao wanadaiwa kuwa ni wawili waliotumia usafiri wa pikipiki ambapo mmoja walimpiga risasi marehemu mlangoni akiwa anataka kuingia nyumbani kwake kisha walitokomea. Tukio hilo limefuatia baada ya Mwenyekiti wa Kitongoji cha Mparange kijijini hapo, Bakari Mpanawe kunusurika kifo baada ya kupigwa risasi ya tumboni na mkononi march 19.

Kamanda wa Polisi wa mkoa wa Pwani, Onesmo Lyanga, alikiri kutokea kwa tukio hilo usiku wa kuamkia march 29. Alisema tukio hilo ni la tano kutokea ndani ya mwezi huu, likihusisha uhalifu wa kutumia silaha za moto. Kamanda Lyanga, alieleza kwamba wanaendelea kuwasaka watu waliohusika kufanya matukio hayo ili waweze kuchukuliwa hatua za kisheria .

Kwa upande wake, Katibu wa CCM wilayani Kibiti, Zena Mgaya, alisema hali ya kiusalama sio shwari katika baadhi ya maeneo wilaya ya Kibiti na Rufiji kijumla.
Alisema hali hiyo inajenga hofu kwa viongozi kupitia CCM ambao baadhi yao wameamua kukimbia miji kwa kuhofia kuuawa.

Zena alibainisha kwamba,matukio ya aina hiyo yanawasababishia kuishi pasipo na amani na wanaCCM kuhofia kugombea nafasi mbalimbali za uongozi katika chaguzi zijazo za chama na serikali za vijiji na vitongoji.

Alihamasisha wanaCCM kugombea nafasi mbalimbali bila kuweka uoga kwani kifo kinapangwa na Mungu. Nae Diwani wa kata ya Dimani, Ramadhani Manyema, alisema kuna wenyeviti wa vitongoji na vijiji vinne wamekimbia miji yao wakihofia maisha yao .
Alisema kukimbia maeneo yao ya kazi kumetokana na kutokea matukio ya hivi karibuni ambapo kuna Mwenyekiti wa kijiji cha Nyambonda pamoja na wenyeviti wa vitongoji viwili na mtendaji wa kijiji hicho kupigwa risasi.

Maeneo mengine ni Jaribu Mpaka ambako OC CID na mgambo wa maliasili walipigwa risasi na kufariki na huko eneo la Kifugo tendaji alijeruhiwa kwa kupigwa risasi.
Manyema alieleza, hali ya kiusalama sio shwari hivyo wanatilia mashaka kama watafanikiwa katika zoezi la uchaguzi wa chama.

Aliliomba jeshi la polisi mkoani Pwani, lishuke vijijini ambapo hali sio nzuri pasipo kukaa mjini pekee. Akizungumza katika ziara yake wilayani Kibiti, Katibu wa CCM mkoani Pwani, Hassan Mtenga aliwataka wazazi na walezi kuwafuatilia nyendo watoto wao kwani wapo vijana wanaotumika kwenye matukio ya kiuhalifu. Mtenga alisema ifikie hatua ya watu kubadilika kwa kuacha kuficha wahalifu kisa ni ndugu ,jamaa ama marafiki .
 
Tuendako siko, tusiingize itikadi za kichama hapa.Tuungane katika kutokomeza mauaji haya. Taabu inakuja pale chama fulani kinaona kinahaki kuliko wengine. Hivyo kupekea watu mwenye grievances za kuonewa kuamua kurespond kimya kimya. This is very dangerous to our country.
 
Ngoja tusubiri uchunguzi wa vyombo vya usalama, ingawa usalama wetu wanapenda kutumiwa na wanasiasa kwenye maswala nyeti.
Usalama wanafanya jazi kama watu wa itukadi na uenezi badala ya kufuata taaluma refer nape kutishiwa bastola
 
Hapo ndio wale wahusika na mambo ya usalama wa ndani wa nchi wanapotakiwa kujitathmini juu ya weredi na utaalamu wao katika masuala ya investigation, and intelligence , kwani Picha linaloendelea pande hizo za kibiti, rufiji, ikwiriri na maeneo mengineyo linadhihirisha uthabiti na udhaifu tulionao katika masuala mazima ya usalama hasa wa raiana mali zao.

Ni rai yangu kwa polisi na vyombo vingine vya ulinzi na usalama kufanya kazi kiweredi na kitaalamu zaid na kuachana na mambo ya kufukuzana na watu wasio na madhara /wasiohitajia matumizi wakubwa ya Jeshi hilo (wengin mnajua hawa jamaa wanaweka nguvu kubwa kwa ishu au matukio gani) Bali nguvu zao wawekeze kwenye mambo nyeti kama hayo ili matukio kama haya yadhibitiwe mapema kabisa kabla halijageuka kuwa usaha utaozaa donda Ndugu.

Namalizia kwa kuwapa pole Sana Ndugu zetu wahanga wa mambo hayo ya mauwaji yanayoendelea pande hizo.
 
Tuendako siko, tusiingize itikadi za kichama hapa.Tuungane katika kutokomeza mauaji haya. Taabu inakuja pale chama fulani kinaona kinahaki kuliko wengine. Hivyo kupekea watu mwenye grievances za kuonewa kuamua kurespond kimya kimya. This is very dangerous to our country.


Mkuu nikikumbukia alphonce mawazo nahisi haki unatolewa kwa upendeleo
 
Mkuu hili swala wanalichukulia juu juu lakini kumlea na kumtetea bashite wakati kavunja sheria ya nchi kunaonyesha Kuna baadhi ya watu wapo chini ya sheria na wengine wapo juu ya sheria
Unaacha kuzungumzia mada husika unaleta ushamba wa kisiasa, tangu umeanza kumtaja huyo bashite umefanikiwa nini? umemtoa madarakani au? Mauaji ya Rufiji na bashite wako huyo wapi na wapi?
 
Iparamasi anawajua hao wenzie waliofanya ilo tukio inaonyesha, hata mimi nashauri kikosi kazi kidili nae
 
shida ya rufiji ni kuwa na idadi kubwa sana ya watu wanao miliki silaha kiholela,na wengi sn walikuwa wanajihusisha na ujangili wa meno ya tembo na mazao ya misitu ktk mapori ya selous vijiji km mkongo,mloka,kilimani,ruwe na delta ya rufiji.ss kudhibitiwa kwa ujangali na biashara ya magogo pamoja na kukamatwa kwa baadhi ya majangili naona wahanga wamegeuzwa viongozi wa chama na serikali wanaosimamia kwa dhati na pia labda waliotoa habari luganikisha vita ya ujangili.
 
Vitendo hivi vya mauaji sasa basi , serikali ichukua hatua madhubuti kukomesha mauaji ya raia wasio na hatia, uchunguzi ufanyike kwa kina, mambo haya yasijirudie tena.
 
  • Thanks
Reactions: SDG

Similar Discussions

Back
Top Bottom