Mwenyekiti wa Bodi: Simba tumejipanga kusajili wachezaji wenye njaa ya mafanikio

Ghazwat

JF-Expert Member
Oct 4, 2015
23,718
66,262
Mwenyekiti wa bodi ya Wakurugenzi wa Simba SC, Salim Abdallah 'Try Again' amezungumza na Azam Tv kwamba, rais wa heshima wa timu hiyo Mohammed Dewji 'MO' anarudi kusajili.

Try Again amesema kuwa tayari wamefanya kikao na rais wa heshima wa Simba SC, Mohammed Dewji'MO' watasajili kwa kishindo ili msimu ujao wafanye maajabu.

"Tumeshindwa kufanya vizuri msimu huu hilo halitutoi mchezoni, tumekutana kama viongozi kwa lengo la kusawazisha makosa yetu hilo limefanyika kwa usahihi".

"Tutasajili wachezaji ambao wana njaa ya mafanikio, tutabaki na wachezaji kadhaa, kuna wengine mikataba yao imekwisha, na wengine kutokana na viwango vyao tutawaaga, lakini nawapongeza wachezaji wetu wamepambana kweli kweli".

"Na kwa sasa tunafanya mchakato wa kupitia CV ya makocha waliotuma maombi na baada ya kumpata atakayekuwa sahihi kabla ya msimu huu haujaisha atapewa nafasi ya kutoa mapendekezo ya usajili na tutaanza bila kuchelewa ili tuendane na mbio za maandalizi mazuri ya mwanzo wa msimu 'Pre Season".
amesema Try Again

Wakati huo huo Try Again alitaja sababu zilizomuondoa Kocha Pablo Franco Martin kuwa ni kushindwa kufikia malengo ya klabu, kutwaa taji la Ligi Kuu, Kombe la Azam Sports Federation Cup, Klabu Bingwa Afrika hatua ya Nusu Fainali, ambayo yalikuwa kama sehemu ya makubaliano ndani ya mkataba.
 
shida si kusajili bali kuwatumia kwa usahihi wachezaji waliosajiliwa! hata mwaka huu usajili wenu Mikia FC ulikuwa mzuri sana ila kilichokosekana ni muunganiko wa wachezaji kucheza kitimu, consistently na kwa nidhamu na morali!!

Si vibaya mkimuomba ushauri na mbinu Professor Nabi nyie ni watani zetu sio maadui.

Wachazaji kama Sakho, Kibu, Banda, Inonga na Kanoute ni wazuri mno ila timu yenu haikujenga formation ya kuwaunganisha. Sisi wananchi tunapenda kuipiga timu bora ya Makolo FC sio timu mbovu kama ile mliyoleta CCM Kirumba, mtoto mdogo Feisaaaaaal anatoka na mpira toka katikati ya uwanja na kwenda kumsalimia Kakolanya bila bugudha yoyote!
 
Kama kweli tunataka kuvuka pale tunapoishia yaani robo fainali na kwenda mbele nusu au fainali ya michuano ya CAF, bila shaka wachezaji hawa pamoja na Kocha msaidizi Matola tungewaaga, kwa kuwashukuru.

Mhilu (mkopo)
Jimmyson (mkopo)
Gadiel
Nyoni
Dilunga
Mzamiru
Mugalu
Kagere
Wawa
Lwanga
Bwalya
Morrison
 
shida si kusajili bali kuwatumia kwa usahihi wachezaji waliosajiliwa! hata mwaka huu usajili wenu Mikia FC ulikuwa mzuri sana ila kilichokosekana ni muunganiko wa wachezaji kucheza kitimu, consistently na kwa nidhamu na morali!!

Si vibaya mkimuomba ushauri na mbinu Professor Nabi nyie ni watani zetu sio maadui.

Wachazaji kama Sakho, Kibu, Banda, Inonga na Kanoute ni wazuri mno ila timu yenu haikujenga formation ya kuwaunganisha. Sisi wananchi tunapenda kuipiga timu bora ya Makolo FC sio timu mbovu kama ile mliyoleta CCM Kirumba, mtoto mdogo Feisaaaaaal anatoka na mpira toka katikati ya uwanja na kwenda kumsalimia Kakolanya bila bugudha yoyote!
Mtu mwenye akili timamu hawezi kwenda kuomba ushauri kutoka kwa timu ambayo wao na kocha wao ktk mashindano ya CAF huwa wanaishia hatua za awali tena kwa vipigo vya bila kujitetea "Ndani Nje" halafu timu yenyewe katika viwango vya ubora caf ni ya 100 na unaetaka aombe ushauri ni wa 12 kwa ubora.

Labda kama ni ushauri wa kutaka tujue ni mbinu gani huwa mnaitumia kuishia hatua za awali na vipigo vya ndani nje , hapo ni sawa tutakuja kuomba ushauri
 
Simba ya msimu ujao kama sio nusu fainali basi fainali yenyewe
Ndo maana usajili ni kwa ajili ya kuangalia michuano ya Kimataifa, na siyo kusajili kwa ajili ya Ligi Kuu

Kwani malengo ya klabu kucheza nusu fainali au fainali kwenye michuano ya CAF.
 
Bocco
Mhilu
Onyango
Wawa
Mkude
Nyoni
Mzamilu
Kagere
Mugalu
Banda
Kanoute
Kakolanya

Hawa wote wasepeshwe

Bila kumsahau Matola
Duh, ni Timu yote sasa..! Ila kwa Matola haiwezekani kuendelea kubakia hapo Simba, na njia ya kumuondoa ni Kocha mpya kuja kuchagua msaidizi wake mwenyewe..!

Banda na Kanoute waendelee, bado wana nafasi ya kuonyesha uwezo wao


Halafu mbona Gadiel na Dilunga hawapo?
 
Timu haiwezi kuendeshwa kwa kutegemea maamuzi ya MTU mmoja hayo ndiyo yametufikisha hapa, kila kiti mpaka mumusubiri moja.
Kunatakiwa kuwe na project ya muda mrefu na mfupi, kusajili wachezaji wazuri in ili tuweze kufika mbali kimataifa ila kuchukua kombe in lazima tuandae timu kama asec mimosa wanavyoandaa timu yao.
Time inatakiwa kujijenga kiuchumi kama Luna biluoni 20 kwanini tunashindwa kukopa benki na kujenga uwanja mkubwa ambao yukiuza haki za matangazo ya uwanja na kuuza tiketi za msimu tuna uwezo was kulipa deni muda mfupi, jengo la simba limekaa sehemu nzuri libomolewe na kujengwa jengo kubwa la kisasa na kuwa kitega uchumi.
Viongozi was kuchaguliwa na kuteuliwa wa bodies wawe watu wanaojua Moira sio watu wameshindwa ubunge wanakuja kujificha kwenye mpira
 
Bocco
Mhilu
Onyango
Wawa
Mkude
Nyoni
Mzamilu
Kagere
Mugalu
Banda
Kanoute
Kakolanya

Hawa wote wasepeshwe

Bila kumsahau Matola
Kwa hiyo hamtaki tena kuwa na kikosi kipana! Halafu unataka Matola asepeshwe kwenda wapi? Unataka timu yenu ishuke daraja msimu ujao?

Usisahau ana majukumu mengine, nje ya kuwa kocha msaidizi!
 
Timu haiwezi kuendeshwa kwa kutegemea maamuzi ya MTU mmoja hayo ndiyo yametufikisha hapa, kila kiti mpaka mumusubiri moja.
Kunatakiwa kuwe na project ya muda mrefu na mfupi, kusajili wachezaji wazuri in ili tuweze kufika mbali kimataifa ila kuchukua kombe in lazima tuandae timu kama asec mimosa wanavyoandaa timu yao.
Time inatakiwa kujijenga kiuchumi kama Luna biluoni 20 kwanini tunashindwa kukopa benki na kujenga uwanja mkubwa ambao yukiuza haki za matangazo ya uwanja na kuuza tiketi za msimu tuna uwezo was kulipa deni muda mfupi, jengo la simba limekaa sehemu nzuri libomolewe na kujengwa jengo kubwa la kisasa na kuwa kitega uchumi.
Viongozi was kuchaguliwa na kuteuliwa wa bodies wawe watu wanaojua Moira sio watu wameshindwa ubunge wanakuja kujificha kwenye mpira
Mmiliki akishasema, hakuna wa kumpinga! Mnachotakiwa mashabiki kwa sasa ni kujiandaa tu kumsifia mitandaoni kwa usajili atakao ufanya msimu.

Halafu suala la bilioni 20, achana nalo! Litakuletea matatizo. Huna sababu ya kuhoji wakati timu imefika robo fainali klabu bingwa Afrika na shirikisho mara kadhaa, ndani ya miaka michache!

Nani kama Dr. Moo na Try Again,
🗣️ Hakunaaaa!!!!
 
Back
Top Bottom