Mwenye dawa ya Tinnitus

Mwenye dawa ya Tinnitus

quantumQ

Senior Member
Joined
Dec 11, 2013
Posts
111
Reaction score
84
Kuna dawa nilipewa hospitali (dawa ya kutibu brucellosis), dozi ya mwezi mzima, nilivyokuwa naitumia kama wiki ya pili hivi nikaanza ku experience ringing noise kwenye masikio yote.

Nikajua ni dawa tu nikimaliza dozi hiyo hali itaisha. Ila baada ya kumaliza dozi wapi hiyo hali haikuisha. Nilienda kwa daktari bingwa wa masikio (ENT - Ear Nose Throat) pale Benjamin Mkapa akani diagnose na Tinnitus akanipa tu Vitamin B complex akassma nitumie baada ya wiki mbili kama hali haijaisha nirudi. Nilitumia ila hali ikawa ipo pale pale.

Nika google google nikakuta online wanasema kuwa hadi leo hakuna dawa ya hiyo kitu kwani zile hairy parts za masikio zinazo sense sauti zimekuwa damaged kwa hiyo zinakuwa zina pick sauti ambazo hazipo.

Kwa hiyo ndio hivyo mpaka leo nina zaidi ya miezi 8 naishi na hii hali. Mchana haini affect sana maana kunakuwa na makelele ya nje ila usiku kwenye hali ya utulivu nakuwa nasikia mngurumo masikioni. Ila nimeshazoea siku hizi but nimemiss complete silence.

Kama kuna yoyote mwenye solution/experience na hii kitu ashare maana hii hali inatesa sana.
 
RUDI HOSPITALINI KWA USHAURI NA MATIBABU ZAIDI

POLE SANA
 
Madawa ya siku hizi yana madhara mengi madhara mojawapo ni kupata hayo maradhi ya sauti katika masikio aka miungurumo (Tinnitus) .

Na hayo maradhi ya (Tinnitus) hakuna dawa ya kuweza kukutibu ukapona kwa dawa za hospitali lakini kwa dawa za asili tiba ipo unapona kabisa ukitumia dawa za asili.
 
Madawa ya siku hizi yana madhara mengi madhara mojawapo ni kupata hayo maradhi ya sauti katika masikio aka miungurumo (Tinnitus) . Na hayo maradhi ya (Tinnitus) hakuna dawa ya kuweza kukutibu ukapona kwa dawa za hospitali lakini kwa dawa za asili tiba ipo unapona kabisa ukitumia dawa za asili.
Ndio zipi hizo ndugu kama unazijua
 
Back
Top Bottom