Mamia kwa mamia ya abiria wanaochukuliwa na mabasi ya mwendo kasi kutoka Mbezi Luis kwenda mjini kwenye shughuli za ujenzi wa taifa wote huteremshwa Kimara terminal halafu tena mabasi hayo hayo au mengine huanza kuwapakia tena kwa nauli nyingine kwenda mjini.
Haijajulikana hasa sababu kubwa ya kuwatesa abiria na kuwapotezea muda wao mwingi kwa kuwashusha na kuwapakia tena.
Hata hivyo abiria wengi wameshagundua kuwa wahusika akili yao yote ni kupata hela zaidi kutoka 650/= na ile ya 400/= na kuwa 1050/=.
Kama shida ni hela kwanini isihalalishwe ili abiria wasiwe wanasumbuliwa na kupotezewa muda wao kwa kuruhusu ruti ya moja kwa moja kwenda mjini? Na ile ruti ya mjini kwenda Kimara nayo iwe ya moja kwa moja hadi Mbezi.
Tunaomba viongozi wenye dhamana sio mhusika na hii UDART waliangalie hili kwa makini kwani linatia aibu kubwa kwa sababu linaondoa dhana yote ya mwendokasi kuwa kero iliyokubuhu.
Haijajulikana hasa sababu kubwa ya kuwatesa abiria na kuwapotezea muda wao mwingi kwa kuwashusha na kuwapakia tena.
Hata hivyo abiria wengi wameshagundua kuwa wahusika akili yao yote ni kupata hela zaidi kutoka 650/= na ile ya 400/= na kuwa 1050/=.
Kama shida ni hela kwanini isihalalishwe ili abiria wasiwe wanasumbuliwa na kupotezewa muda wao kwa kuruhusu ruti ya moja kwa moja kwenda mjini? Na ile ruti ya mjini kwenda Kimara nayo iwe ya moja kwa moja hadi Mbezi.
Tunaomba viongozi wenye dhamana sio mhusika na hii UDART waliangalie hili kwa makini kwani linatia aibu kubwa kwa sababu linaondoa dhana yote ya mwendokasi kuwa kero iliyokubuhu.