Mwanzo wa mwisho wa utawala wa Makonda Dar?

Quinine

JF-Expert Member
Jul 26, 2010
21,271
47,271
Matukio ya hivi karibuni yanayozunguka utendaji wa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda na kauli zilizotolewa na viongozi wakuu wa nchi kuhusu mwenendo wake, zimeibua shauku kubwa kuhusu hatima ya kiongozi huyo kijana.

Sasa kuna dalili kuwa ile hali ya kumwagiwa sifa na Rais John Magufuli, iliyochangia kung’arisha nyota yake, imebadilika.

Wachambuzi wa mienendo ya siasa za Tanzania wanasema, kitendo cha Rais Magufuli kuagiza hadharani makontena ya Makonda yalipiwe ushuru ni dalili za kumchoka mteule wake.

“Umesikia hili sakata la Dar es Salaam, eti Mkuu wa Mkoa ameleta makontena, ameambiwa alipe kodi, kwa nini asilipe kodi"? Alihoji Rais Magufuli.

Kabla ya kauli hiyo ya rais, tayari Makonda alikwishaandika barua kwa Waziri wa Fedha, Dk Philip Mpango na barua yake kuvuja kwa bahati mbaya? akitaka vifaa hivyo visamehewe kodi.

Baada ya TRA kusisitiza kuuza makontena hayo Makonda alitahadharisha kuwa atakayeyanunua atalaaniwa na Mungu.

Siku moja baada ya kauli hiyo, Dk Mpango aliagiza yapigwe mnada akisema, “Kamishna piga mnada mara ya kwanza, ya pili na ya tatu kadri sheria inavyoruhusu. Hata mimi ningekuwa na hela ningekuja kununua tuone hiyo laana itatoka wapi.”

Wachambuzi wanadai kuwa ujasiri wa Dk Mpango dhidi ya Makonda, hata kama alikuwa anasimamia sheria haukuwa wa kawaida.

Kuna makada mbalimbali wa CCM nao wamejitokeza hadharani kupinga uongozi wa Makonda.

Katibu Mkuu wa CCM Bashiru Ally alikaririwa akisema Makonda alipaswa kuwashirikisha wenzake tangu hatua za awali, kwa kuwa Serikali ni moja, akikumbusha kuwa Dar es Salaam ni mmojawapo ya mikoa isiyotekeleza vyema Ilani ya CCM kutokana kufanya kazi bila ushirikiano.

“Na hii habari ya Dar es Salaam ya Makonda, hakuna Dar es Salaam ya Makonda, ni Dar es Salaam chini ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Makonda.” alisema.

“Kuna wakati namsikia anasema wananchi wangu, nani kamwambia anao wananchi wake? Hakuna wananchi wako. Hakuna kiongozi anamiliki wananchi, ni wananchi wenzangu.”

Aliyekuwa Katibu Mkuu wa CCM, Yusufu Makamba, alipotakiwa kutoa maoni yake juu ya uongozi wa Makonda alisema, kwa sakata la makontena ni bora mlengwa akatumia busara na kujipima.

"Rais akishasema kamaliza wewe mteuliwa utumie busara kuamua, ayatafakari hayo maneno ya bwana mkubwa ambaye ndiye mwamuzi wa mwisho, akishasema lipa lazima ulipe". alisema.


Kada mwingine maarufu wa CCM na mhadhiri wa chuo kikuu cha Dar es salaam Dr. Benson Bana alisema, matamshi yaliyotolewa na viongozi wenzake ni fundisho tosha ajitafakari na kupima kauli zake.

"Ingawa anafanyakazi nzuri, na kuleta maendeleo lkn lazima awe mstari wa mbele kusimamia sheria. Nadhani ameshapewa ujumbe wa kutosha sasa ajitafakari na abadilike". Bana alisema.

Chanzo: Mwananchi.

Mwanzo wa mwisho utawala wa Makonda Dar?
 
Hivi bado hamuachi kumjadili huyu mtu. Hawezi kutoka madarakani na muombe abaki hapo vinginevyo atapewa uwaziri
 
Yaani jana tu nimepisha nae, mbele kukiwa na gari ya polisi imewasha king'ora gari yake ikifuatia nyuma, rangi nyekundu, sijui ni lexus ile au Vx.. Sioni dalili yeyote ya bwana Bashite kutumbuliwa..
 
Bado mnasubiria!!! Huyo dogo jiwe acheni nae na hupaswi kumuiga kama afanyavyo Muro ipo siku ataumbuka .
 
Chadema acheni propaganda ,mleteni dereva ahojiwe na polisi.

Makonda bado yupo sana dar ,msiomtaka mjinyonge tu tunajua mnampiga vita ili aondoke muuze kwa uhuru madawa yenu
 
Chadema acheni propaganda ,mleteni dereva ahojiwe na polisi.

Makonda bado yupo sana dar ,msiomtaka mjinyonge tu tunajua mnampiga vita ili aondoke muuze kwa uhuru madawa yenu
 
Jiwe alianza kwa mbwembwe sana lakini amewaangusha sana Watanzania katika masuala ya Makonda na ufisadi wa chaguzi ndogo za ubunge.
Viongozi waliopita kama Mkapa wasingeruhusu ujinga huo. Double standard ya kiwango cha juu.
 
Yaani jana tu nimepisha nae, mbele kukiwa na gari ya polisi imewasha king'ora gari yake ikifuatia nyuma, rangi nyekundu, sijui ni lexus ile au Vx.. Sioni dalili yeyote ya bwana Bashite kutumbuliwa..
Ulitaka ukutane naye akitembea peke yake kwa miguu.
 
Chadema acheni propaganda ,mleteni dereva ahojiwe na polisi.

Makonda bado yupo sana dar ,msiomtaka mjinyonge tu tunajua mnampiga vita ili aondoke muuze kwa uhuru madawa yenu
Siyo Chadema ni viongozi wako wakuu wanasema,

Katibu Mkuu wa CCM Bashiru Ally alikaririwa akisema Makonda alipaswa kuwashirikisha wenzake tangu hatua za awali, kwa kuwa Serikali ni moja, akikumbusha kuwa Dar es Salaam ni mmojawapo ya mikoa isiyotekeleza vyema Ilani ya CCM kutokana kufanya kazi bila ushirikiano.

“Na hii habari ya Dar es Salaam ya Makonda, hakuna Dar es Salaam ya Makonda, ni Dar es Salaam chini ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Makonda.” alisema.

“Kuna wakati namsikia anasema wananchi wangu, nani kamwambia anao wananchi wake? Hakuna wananchi wako. Hakuna kiongozi anamiliki wananchi, ni wananchi wenzangu.”
 
Yaani jana tu nimepisha nae, mbele kukiwa na gari ya polisi imewasha king'ora gari yake ikifuatia nyuma, rangi nyekundu, sijui ni lexus ile au Vx.. Sioni dalili yeyote ya bwana Bashite kutumbuliwa..

Mganga wa Bashite sio wa nchi hii. Dawa zinafanya kazi hadi kwa Jiwe? Kweli chui naye ana mkwewe na hamna mkate mgumu kwa chai.
 

Na mkiendelea kumusemasema mwaka 2020 anagombea ubunge namupa uwaziri mkuu. Ili muwone siwaogopi.

Ahiiiiiii.... Toba! Geeez....🤗 Asije akamteua kuwa Waziri wa Mambo ya Ndani. Tutaona viroja balaaa.
 
hiki ndio kinatufanya tusiendelee kama Nchi

ku discuss watu baada ya falsafa za watu....

ku discuss maneno ya watu na sio falsafa zao

lazima tubadilike kama nchi kama tunadiscuss Makonda tumdiscuss kama taasisi ya mkuu wa mkoa sio personal issues je nikweli Makonda amefail majukumu yake kama taasisi? au ni propaganda?

Tukitoka hapo tena tuanze tuanze kulilia utawala bora na democrasia lazima tukubaliane kuwa tofauti kimaono na kimawazo na kimtazamo wa mambo.

ndio maana mpaka leo mimi naamini ccm ni nzuri lakini falsafa za ccm ndio mbovu watunga sera ndani ya ccm ndio wabovu ila chama ni kizuri kitaasisi ila utendaji kama team ndio wanafail ila huwezi kusema pole pole hana akili ila angalia yupo kwenye mfumo gani?
 
Matukio ya hivi karibuni yanayozunguka utendaji wa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda na kauli zilizotolewa na viongozi wakuu wa nchi kuhusu mwenendo wake, zimeibua shauku kubwa kuhusu hatima ya kiongozi huyo kijana.

Sasa kuna dalili kuwa ile hali ya kumwagiwa sifa na Rais John Magufuli, iliyochangia kung’arisha nyota yake, imebadilika.

Wachambuzi wa mienendo ya siasa za Tanzania wanasema, kitendo cha Rais Magufuli kuagiza hadharani makontena ya Makonda yalipiwe ushuru ni dalili za kumchoka mteule wake.

“Umesikia hili sakata la Dar es Salaam, eti Mkuu wa Mkoa ameleta makontena, ameambiwa alipe kodi, kwa nini asilipe kodi"? Alihoji Rais Magufuli.

Kabla ya kauli hiyo ya rais, tayari Makonda alikwishaandika barua kwa Waziri wa Fedha, Dk Philip Mpango na barua yake kuvuja kwa bahati mbaya? akitaka vifaa hivyo visamehewe kodi.

Baada ya TRA kusisitiza kuuza makontena hayo Makonda alitahadharisha kuwa atakayeyanunua atalaaniwa na Mungu.

Siku moja baada ya kauli hiyo, Dk Mpango aliagiza yapigwe mnada akisema, “Kamishna piga mnada mara ya kwanza, ya pili na ya tatu kadri sheria inavyoruhusu. Hata mimi ningekuwa na hela ningekuja kununua tuone hiyo laana itatoka wapi.”

Wachambuzi wanadai kuwa ujasiri wa Dk Mpango dhidi ya Makonda, hata kama alikuwa anasimamia sheria haukuwa wa kawaida.

Kuna makada mbalimbali wa CCM nao wamejitokeza hadharani kupinga uongozi wa Makonda.

Katibu Mkuu wa CCM Bashiru Ally alikaririwa akisema Makonda alipaswa kuwashirikisha wenzake tangu hatua za awali, kwa kuwa Serikali ni moja, akikumbusha kuwa Dar es Salaam ni mmojawapo ya mikoa isiyotekeleza vyema Ilani ya CCM kutokana kufanya kazi bila ushirikiano.

“Na hii habari ya Dar es Salaam ya Makonda, hakuna Dar es Salaam ya Makonda, ni Dar es Salaam chini ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Makonda.” alisema.

“Kuna wakati namsikia anasema wananchi wangu, nani kamwambia anao wananchi wake? Hakuna wananchi wako. Hakuna kiongozi anamiliki wananchi, ni wananchi wenzangu.”

Aliyekuwa Katibu Mkuu wa CCM, Yusufu Makamba, alipotakiwa kutoa maoni yake juu ya uongozi wa Makonda alisema, kwa sakata la makontena ni bora mlengwa akatumia busara na kujipima.

"Rais akishasema kamaliza wewe mteuliwa utumie busara kuamua, ayatafakari hayo maneno ya bwana mkubwa ambaye ndiye mwamuzi wa mwisho, akishasema lipa lazima ulipe". alisema.


Kada mwingine maarufu wa CCM na mhadhiri wa chuo kikuu cha Dar es salaam Dr. Benson Bana alisema, matamshi yaliyotolewa na viongozi wenzake ni fundisho tosha ajitafakari na kupima kauli zake.

"Ingawa anafanyakazi nzuri, na kuleta maendeleo lkn lazima awe mstari wa mbele kusimamia sheria. Nadhani ameshapewa ujumbe wa kutosha sasa ajitafakari na abadilike". Bana alisema.

Chanzo: Mwananchi.

Mwanzo wa mwisho utawala wa Makonda Dar?
Issue ya kutumbuliwa Ma-Konda nime ngojea mpaka nimechoka...........Sasa nasema hv Ma-Konda piga kazi
 
Back
Top Bottom