Mwanafunzi mtanzania afariki China katika mazingira ya kutatanisha

Zakamwamoba

Senior Member
Jul 28, 2016
173
602
KUNA HII HABARI NILIKUTNA NAYO JANA
Kuna Binti wa kitanzania alikuwa anasoma nchini china kwa jina amefahamika kama Safina John Msemo alikutwa amefariki chumbani kwake. Binti huyo alikuwa anasoma katika chuo cha Nanchang kilichopo nchini humo alikutwa amefariki usiku wa kuamkia tarehe 13, januri 2017.

Kutokana na utata wa kifo chake, chanzo cha kifo bado hakijajulikana ,madaktari wanaendeleana uchunguzi ila kwa habari za kunyapinyapia zinasema eti inawezekana kuna watu wamehusika kusababisha kifo hicho. Tunaomba ubalozi wa Tanzania nchini china tupeni taarifa kamili'

NB: watu mnaoenda nchi za watu kuweni makini sana

=======

Kuna taarifa za huzuni zimetufikia kwenye meza yetu ya habari zinasema Binti mtanzani aliyekuwa anasoma nchini china katika chuo cha "Nanchang", Safina John Msemo amefariki dunia. Marehemu alikutwa amefariki usiku wa kuamkia jana 13 januari 2016 chumbani kwake.

Bado kuna utata mkubwa juu ya chanzo cha kifo cha marehemu kutokana na kuwa na taarifa tofauti zinazokinzana,taarifa kutoka kwa watu wa karibu yake zinasema marehemu alikuwa anaumwa kwa takribani wiki mbili zilizopita na alikuwa haonekani darasani wakati wakala wa marehemu huyo (Global Education Link) ametoa taarifa na kusema kifo ni cha ghafla "sudden death", Bado uchunguzi wa chanzo chakifo hicho unaendelea. MTILAH BLOG inaendelea kufuatilia tukio hilo

Taratibu zakusafirisha mwili wa marehemu zinafanyika

KUHUSU KUSAFIRISHA MWILI

Taarifa iliyotolewa na uongozi wa TASAFIC (Umoja wa wanafunzi wanaosoma China) ni kwamba, gharama za kusafirisha mwili ni Dola 10000 ambayo ni sawa na 63,000RNM yaani takribani Tsh Millioni 20. Gharama hizi zinatakiwa kulipwa na familia ya marehemu na siyo wakala wake"Agent" japo wakala amesema atalipa halafu familia itazirudusha.

Pia TASAFIC imetoa wito kwa wanafunzi wote wanaosoma nchini china na watanzania kwa ujumla kutoa michango yao katika kusaidia kusafirisha mwili wa marehemu.

Unaweza kuwasilisha mchango wako kupitia mtandao wa wechat ID Gwasa722936,
Bank account:China construction Bank 6217000010061194463
 
Kutokana na utata wa kifo chake, chanzo cha kifo bado hakijajulikana...
Halafu hii habari hapo binafsi sijaielewa sijui ilitakiwa kutuonesha nini.

Hata hivyo mazingira ya chumbani na alivyokutwa yangeweza kufanya tuone kama kifo ni cha utata kama habari inavyosema ama la. Mtazamaji wa pembeni inabidi niendelee kuwa mtazamaji mpaka ripoti itakavyotoka.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom