Mwambe: TRA igawanywe na kila Idara ijitegemee kama ilivyokuwa awali yaani Income Tax Dept, VAT Dept na Customs

johnthebaptist

JF-Expert Member
May 27, 2014
84,018
142,058
Mbunge wa Masasi aliyewahi kuwa Waziri wa Biashara na Uwekezaji mh Mwambe amesema mifumo ya sasa ya TRA siyo rafiki, imejaa Uonezi na ni Sumbufu.

Mwambe amesema hii inatokana na kila mmoja pale TRA kujiona anajua kila Kitu hali inayopelekea usumbufu mkubwa kwa Walipa kodi na hata miongoni mwa Wafanyakazi wenyewe.

Mwambe amependekeza TRA igawanywe na iwe na Idara zinazojitegemea kama ilivyokuwa awali kabla ya Sanare.

Idara hizo ni Income Tax, VAT Dept na Customs.

Mh Mwambe alikuwa anajadili Ripoti ya CAG.

Chanzo: TBC
 
Mh Mwambe ana hoja, asikilizwe.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…