Msittu
Member
- Apr 6, 2012
- 7
- 36
Tathimini binafsi ya Baba wa Taifa ilijikita katika uzoefu alioupata kifalsafa, kiutawala na kiuongozi. Mwalimu alianza kwa kutabanaisha kuwa ili Tanzania ipate maendeleo ni sharti kuwakabiri maadui watatu: Umasikini, Ujinga na Maradhi.
Katika kutambua ugumu na mwelekeo wa vita hiyo, Mwalimu aliona mtikisiko katika Taifa uliozaa nyufa tatu: Rushwa, Muungano na Katiba.
Kwa bahati nzuri utatuzi wa masuala hayo Mwalimu aliuweka bayana kuwa ni lazima kuwe na Siasa safi, Uongozi bora, Ardhi na Watu.
Sina shaka haya mambo yapo bayana kwa Umma. Huu ni mtego wa Umma, ni mapinduzi pekee yanayoweza kuleta mabadiliko. Mwalimu aliamini katika mapinduzi ya fikra, aliamini njia salama ni kupitia fikra pingani.
Mawazo na maarifa ni lazima yasigane kujenga misingi imara.
Katika kutambua ugumu na mwelekeo wa vita hiyo, Mwalimu aliona mtikisiko katika Taifa uliozaa nyufa tatu: Rushwa, Muungano na Katiba.
Kwa bahati nzuri utatuzi wa masuala hayo Mwalimu aliuweka bayana kuwa ni lazima kuwe na Siasa safi, Uongozi bora, Ardhi na Watu.
Sina shaka haya mambo yapo bayana kwa Umma. Huu ni mtego wa Umma, ni mapinduzi pekee yanayoweza kuleta mabadiliko. Mwalimu aliamini katika mapinduzi ya fikra, aliamini njia salama ni kupitia fikra pingani.
Mawazo na maarifa ni lazima yasigane kujenga misingi imara.