kilimasera
JF-Expert Member
- Dec 2, 2009
- 3,069
- 265
Mwalimu amvunja mkono mwanafunzi wake
Mwalimu wa Kiingereza katika Shule ya Msingi Furaha jijini Mwanza, Jafeth Manyirizu, anatafutwa na Jeshi la Polisi mkoani humo kufuatia kudaiwa kumvunja mkono mwanafunzi wake, Asia Yasini, wakati akimwadhibu kwa kumpiga kwa ubao.
Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi mkoani humo, Simon Siro, chanzo cha mwalimu kumvunja mkono mwanafunzi huyo ni kupindisha mstari wakati akifundishwa somo hilo. Jeshi langu linaendelea na upelelezi wa tukio hili ili liweze kumtia katika nguvu za dola na sheria iweze kuchukua mkondo wake dhidi iya mwalimu huyu katili, alisema Siro ambaye amewaomba Walimu wenye tabia hiyo kuacha vitendo hivyo kwani kitendo alichofanyiwa binti huyo ni cha ukatili.
Mkuu wa shule hiyo, Emmanuel Manoni, amesema hana taarifa za kitendo alichofanya Mwalimu huyo lakini akaahidi kuwa atazifuatilia ili kuzifahamu kwa undani.
Mwalimu wa Kiingereza katika Shule ya Msingi Furaha jijini Mwanza, Jafeth Manyirizu, anatafutwa na Jeshi la Polisi mkoani humo kufuatia kudaiwa kumvunja mkono mwanafunzi wake, Asia Yasini, wakati akimwadhibu kwa kumpiga kwa ubao.
Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi mkoani humo, Simon Siro, chanzo cha mwalimu kumvunja mkono mwanafunzi huyo ni kupindisha mstari wakati akifundishwa somo hilo. Jeshi langu linaendelea na upelelezi wa tukio hili ili liweze kumtia katika nguvu za dola na sheria iweze kuchukua mkondo wake dhidi iya mwalimu huyu katili, alisema Siro ambaye amewaomba Walimu wenye tabia hiyo kuacha vitendo hivyo kwani kitendo alichofanyiwa binti huyo ni cha ukatili.
Mkuu wa shule hiyo, Emmanuel Manoni, amesema hana taarifa za kitendo alichofanya Mwalimu huyo lakini akaahidi kuwa atazifuatilia ili kuzifahamu kwa undani.