Mwakyembe avutia pumzi 'unga' airport


E bwana naona mambo mazito sasa.
 
Suleiman Suleiman Mkurugenzi TAA naye ni muuza unga (anaogopa kuzungumzia biashara yake haramu)
Ile list aliyonayo Dhaifu inaongezeka..


Mbona watu wa dini fulani ndio wengi sana kwenye masuala ya sembe?Lipumba atasemaje ?ndio hawa second class citizen?
 
Ninaamini bishara ya madawa ya kulevya Tanzania haijafikia katika kiwango cha nchi kama Afghanistan, Pakistan, Colombia, Jamaica, Mexico, etcetera etcetera.

Siamini kama kwa sasa Tanzania kuna drug cartels ambazo zimejipanga kama za nchi ambazo nimezitaja hapo juu ambapo utendaji wake mara nyingi unakuwa wa makini ukijumuisha vitengo kama hitmen, falcons and drug lords wakati mwingine yanajinasibisha kwa utendaji hata zaidi ya makampuni ambayo yanajulikana duniani.

Muda wa kulishughulikia swala hili ni SASA wakati bado hakujakuwa na ngome imara na nina imani na utendaji wa Dk. Mwakyembe even though action and instinct lazima ziwe zaidi ya zile alizotumia wakati alipoifumua Mamlaka ya Bandari nchini (TPA).

I wish Tanzania kungekuwa na waandishi wa habari makini na siyo hawa corrupt, fake and ill-educated.

Badala ya waandishi wa habari Tanzania kufukuzana na vihabari vya vyama vya siasa, wangeweka nguvu zao kwanza kwenye kugundua mtandao na kilichoko nyuma ya biashara hii chafu na kwa kufanya hivyo, wangeweza kuitendea haki jamii na kwa wakati huo huo, wangeweza kutengeneza pesa sana kwa kuuza habari.

Hii inadhihirisha hata hapa Jf pale thread inapokuja kuhusu madawa kwa jinsi inavyopata watu wengi wanaoisoma.

Hakuna habari nyingine Tanzania ambayo ni HOT CATE kwa sasa kama kugundua mtandao wa madawa ya kulevya.

Watu kama Dk. Mwakyembe wanapaswa kupongezwa kwa maamuzi ya busara na yenye hatari mbele yake.
 
Mwakyembe acha longolongo fanya kazi hawa wauza unga wanaliaribu taifa.
 
>Jk Anayo List ya majina yao.
>Mzee Mwinyi alishakumbwa na kadhia hii.
>B.W.MKAPA alishang'aka kuhusu biashara hii
>Sumaye Naye alishatoa tahadhari.
>I.G.P MWEMA anaijua vyema biashara
>ROBERT MANUMBA mambo yamemzidi anamsukumia zigo kamishina 'Nzowa'
>Pinda mpaka takwimu alitutajia

.......AND LIST GOES ON......

Rais Na vigogo wa hili Taifa Wamefyata Mkia.
MWAKYEMBE Ni nani???

Nchi Hii, Bangi na Mirungi, ndio madawa ya kulevya, hizo zingine ni 'UFADHILI WA SERIKALI YETU'.

R.I.P AMINA CHIFUPA(AC)
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…