MUNGU huombwa wakati gani?

MUNGU huombwa wakati gani?

Ziroseventytwo

Platinum Member
Joined
Mar 27, 2011
Posts
9,160
Reaction score
17,061
Mimi ni Mchagga ambaye bado nafanya mila zote. Kuanzia kuchinja na hata kutambika.

Na pia ni mkristu mkatoliki. Nakiri imani yangu kila jumapili. Naamini katika utatu mtakatifu. Yaani Baba, Mwana na Roho Mtakatifu.

Wachagga tuna MUNGU Wetu. Anaitwa RUWA. au RUWA MANGI kwa maana ya MUNGU MKUU.

Kwa mujibu wa wazee wetu wa zamani wachagga walikuwa wakimwomba Mungu wakati wa shida tu. Na nyingi ya shida/tatizo walilokuwa wakiomba walikuwa wanapata tena kwa wakati Kwa mfano kulikuwa hamna haja ya kwenda kumwomba Mungu kama kila kitu kilikuwa kinakwenda sawa. Mazao yanapatikana, mifugo inazaliana, mvua zinanyesha na magonjwa hamna.

Ikitokea kwa mfano kijana wa miaka kati ya 18-40 akafa basi ilikuwa lazima kijiji au hata kata nzima baada ya kumaliza kuzika ilibidi wakae wazee na kwenda kwa RUA kumwomba aepushe jambo hilo lisitokee tena. Nawalikuwa wakitoa sadaka haswa mbuzi aliyenono au hata ng'ombe dume aliyenona kisawasawa.

Kwa wakati huo vifo vingi vilikuwa ni kwa wazee na watoto wadogo. Mtoto alikuwa akishafikisha miaka 5 ilikuwa ndio nitolee. Kama

Sasa baada ya kuja dini za kutoka magharibi na uarabuni wakatuletea vitu vya ajabu. Kwamba tukeshe tukiomba. Unaomba nini wakati huna shida? Una familia ina afya njema. Mali kibao, biashara inayofanya vizuri. Je una haja ya kwenda kuomba? Unaenda kanisani/msikitini kuomba nini? Upele ujikune?

MUNGU HUOMBWA WAKATI GANI?
 
Mkuu pole sana aisee..wewe ni vuguvugu kuzimu upo na kwa Mungu upo.

Mungu huombwa wakati wote.
Kila jambo na wakati wake na majira Yake.
 
Kanisani tunaenda kumwabudu Mungu, maombi yanafanyika pale tu unapokuwa na shida, haijalishi ni yako,ndugu,jamii nk
 
Mkuu pole sana aisee..wewe ni vuguvugu kuzimu upo na kwa Mungu upo.

Mungu huombwa wakati wote.
Kila jambo na wakati wake na majira Yake.
Unaenda kuomba nini mama kwa mfano.
 
ndugu yangu mungu huombwa wakati wote yeye ndie aliyekupa na yeye ndie anakunyima elewa kuwa mungu hufurahi sana unapomuomba na hata kama wewe tajiri kuliko yeyote yule unapaswa kuomba mungu akuzidishie na asikupe kiburi na muombe uwakumbuke masikini pia unapopata utajiri unapaswa kumshukuru usiku na mchana
 
tena unauliza maswali ya kitoto kwa kumkejeli mungu kwakuwa una afya na pesa ya kula ngoja siku akiiondoa afya kutoka kwako akupe ugonjwa ndio utajua mungu huombwa muda gani na na imani ukiwa hoi utakuwa kila mara mungu nisaidie ooh mungu niokoe na ugonjwa huu kila dakika utakuwa unaomba na kulia kiburi chako ndio kimekufanya uulize eti mungu anaombwa wakati gani
 
Hakuna wakati maalum wa kumuomba Mungu. Wewe chapa kazi kwa kujiamini ila usimtendee binadamu mwenzako kitu ambacho hutaki kutendewa. Nashukuru kwa kua unakumbuka mila zako
 
Najaribu kutafakari kwa mapana na kugundua hasa Wafrika tunatumia nguvu nyingi na kupoteza muda kuomba Mungu
Badala ya kutafakari uweza wa Mungu na maajabu aliyomptia mwanadamu kutenda
Kwan naamini Mungu alishafanya kazi yake na alimaliza kwa binadamu na binadamu anatakiwa kumshukuru Mungu na kuendelea kutumia uweZa waliotupatia wa kupambanua mambo na ndio maana bara la Ulaya walielewa mapema

Mungu kampa binadamu kila kitu akitawale na ndio maana maendeleo kwako ndio msingi na kuendelea kuvumbua na sisi kuwaona ma Mungu watu wao wameweka dini pembeni na kutuadaa na kuona eti tunamjua Mungu kuliko wao

Tuache ujinga kupoteza muda wa kuomba badala ya kukimbiZana na mambo aliyotuandalia tuyafanye Na kupata maendeleo

Kwa mtu anaetumia muda mwingi kusoma maandiko ya dini ni ngumu kunielewa

Kuna watu wanaamina kuomba kunaleta maajabu tuache huo upuuzi Maajabu yanakuja kwa kufanya kazi ya kupambana haswa na kuumiza vichwa na c kupiga goti na kuomba (KUNAHITAJIKA MJADALA MPANA KUHUSU HILI)
 
tena unauliza maswali ya kitoto kwa kumkejeli mungu kwakuwa una afya na pesa ya kula ngoja siku akiiondoa afya kutoka kwako akupe ugonjwa ndio utajua mungu huombwa muda gani na na imani ukiwa hoi utakuwa kila mara mungu nisaidie ooh mungu niokoe na ugonjwa huu kila dakika utakuwa unaomba na kulia kiburi chako ndio kimekufanya uulize eti mungu anaombwa wakati gani
Sijamkejeli. Kama umesoma post yanyu #1 utanielewa vizuri. Mimi nimeuliza Mungu anatakiwa kuombwa wakati gani. Ulipaswa kuniambia siku flani au wakati flani.

Pia nimesema huwa nakiri imani yangu kila j2.
 
Back
Top Bottom