Mume wa mtu kaning'ang'ania......

Hatumlaumu Kisukari ila tunampa ushauri kuwa yeye hapo ndio mwenye hasara (Rejea uzi wa mzizi mkavu). Hakuna atakacho gain whether mwenye makosa ni yeye au hilo libaba. Mfano anapoteza chance za kupata right partner kwa kukubali kugandwa na hilo libaba whether walisha du au la...maana unategemea jamii inayowaona close itakubali story za kuwa bado wako kwenye process. Kwa kifupi hicho ni kiwingu na kuchafua CV. Huyo mwanaume ana CV gani ya kuchafua? kama mke anaye...maisha kamaliza...Yeye bishosti?

Vile vile haina maana kumlaumu mwanaume pia kwa kuwa siyo aliyeomba ushauri. Na hatujuhi kwa umri alonao hata kama anajua kuna kitu kinaitwa JF. Lol.

msimlaumu huyu dada,na huyo mwanamume jee,ambae anajua anaelewana na mke wake pamoja na mtoto wake.inaonyesha ni mtu mzima kabisa,ila amekosa heshima.bi dada mrekodi,likija kubumbuluka,wewe ndio utaonekana mbaya
 

BJ uko mama?sijakuona muda mrefu mama!
 

Mi apenda huu ushauri mama!hakika hapa ni nyumba kubwa!thank u!
 
Humtaki kwa nini mnatumiana SMS? Au tuseme wewe una boyfriend na huyo boyfriend kuna jimama linamng'ang'ania na yeye anakwambia hamtaki..............Lakini wanatumiana SMS utaelewaje hiyo sarakasi?
 
Nyie wana wake mmekatwa vichwa mbona mnaviji mkasa vya kijinga,ww ndo umemfuata mwenyewe
 
inanikumbusha thread ya Majjid, ya kutongozwa-Jitathimin mwenyewe, umejiweka kimtego mtego mwenyewe mpaka BABA yakoanataka umzalie. Kazi ni kwako, sina cha kukushauri
 
mpe anachotaka, we unaona raha kumsumbua mtoto wa mwanamke mwenzio?
 
Nipo kamanda..majukumu mengi, si unaona maisha haya yanayobana aisee!! vp wewe?

pole sana...bt ndo ukubwa...i guess ulipokuwa mtoto uliambiwa kua uyaone...by that time mie nilifikiria ni maghorofa...kumbe kua uyaone maisha..tena yalivo magumu!!!
 

Peleka polisi huyo,watamtngisha hatarudia tena
 
Mpaka akwambie umzalie mtoto inawezekana mmeshaonjana tayari kanogewa na anataka umzalie mtoto.Kwa ninavyojua mwanaume hawezi kukutaka siku ya kwanza na kuanza na neno la umzalie mtoto kabla hajakuonja.
huo ndo utakuwa ukweli wenyewe!achana na mume wa mtu,ni sumu kali!ili mtu akutongoze,wewe umejenga mazingira ya kumruhusu akutongoze,nina hakika ungekuwa rafiki mkubwa wa mwanae na kumheshimu mkewe kama unavyodai,ungejiheshimu kwa huyo mwanaume na asingekutaka.
 
Shosti,ivi ulimpaje nafasi mpaka akakuzowea kiasi hicho? inamaana hajuai kama wewe una bwana? au hao watoto alomzalia mkewe sio watoto ni nyani? halafu kwanini unajenga mazowea nae kupita kiyasi yani kama hujaenda kazini kwake anakuja yeye ebu fikiri siku mkewe anakukuta kabla hujamwambia atakuonaje? ebu eleza yote usitubanie mficha uke hazai....
 
Halafu nimeshaona tabia za kina dada wengi,Rafiki yake akimtambulisha kwa boydriend wake basi huyo dada huanza kutafuta jinsi ya kumpata huyo boyfriend wa rafiki yake siku akikutana na boyfriend wa rafiki yake akiomba mchezo anapewa kiurahisi sijui ni kwa nini inakuwa hivyo.
 
hajawahi kunigusa kimwili..
Haiwezekani.Basi inawezekana wewe ulianza kujenga naye mazoea mabaya au ulipomwona anakuzoea nawe ukamzoea ukampa hiyo nafasi mpaka mkafikia hapo mlipo.Wanaume wengi ni wajanja sana ukiwapa nafasi kukuzoea tu wakikuomba mchezo lazima utakubali siku moja maana wanawake mna huruma sana kwenye hayo mambo,labda uwe mtu uliyeshika dini yako vizuri sana.
 
Ananitumia sms na kunambia kila kitu kuhusu matatizo yake na mkewe ndo mana sms nazo sijazifuta

owkeyyyyyy! Sasa fanya hiviiiiii
Mwambie hutaki kuwa na mahusiano naye na uache kuwasiliana naye. Mtahadhalishe kuwa kama akiendelea utamweleza mkewe na utamuonyesha hizo msg. Mambo yakizidi mweleze mkewe kwa nia njema ili kusaidia kuilinda ndoa yake.
 

Ushauri mzuri lakini mwenyewe anayeshauriwa anaonyesha bado anainterest na mume wa mtu!
 
Hivi wewe Happiness win unawajua wanaume au unawasikia yaani kawaida ya mwanaume kuwaka tamaa kwa mwanamke yeyote anayekutana naye hata rafiki wa dada yake, rafiki wa mama yake, rafiki wa mkewe na wengine wasio ndugu ni jambo la kawaida. Tena wakati mwingine anaweza kuja rafiki wa mke wake nyumbani kuwatembelea na baada ya kuaga ameondoka, mwanaume anaweza kujifanya anaenda kukutana na rafiki yake kumbe anaenda kumfuatilia rafiki wa mkewe na kumtaka kimapenzi. Tunachotofautiana kati ya mwanaume mmoja na mwingine ni kiwango cha kudhibiti tamaa. Mwingine tamaa ikiwaka tu anataka kuitimiza kama ilivyokuja mwingine anasema hapa huyu ni fulani namheshimu na kukataa kuburuzwa na matamanio, tofauti iko hapo basi.
Kwa hiyo, anachosema Sikati Tamaa ni kweli wanaume wako hivyo na wengine mnaweza kukutana siku hiyohiyo mpaka akamtokea mwanamke na kumtongoza na siku hiyohiyo wakafanya uzinzi sembuse yule ambaye wanafahamiana, hapo ni rahisi zaidi. Anaanza oooh rafiki yako hivi, ooo rafiki yako vile, mpaka anaingiza mambo yake anayotaka.
Sikati Tamaa wakuache bwana wasioamini uliyosema achana nao, wewe pambana na huyo kisonoko hakikisha hakunyimi raha wala amani yako, BE A WOMAN WHO KNOWS WHAT SHE WANTS
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…