Mtoto wa Museveni, Muhoozi: Namfuta Bobi Wine kushiriki kwenye shughuli zozote za Kiuchaguzi nchini Uganda

Mtoto wa Museveni, Muhoozi: Namfuta Bobi Wine kushiriki kwenye shughuli zozote za Kiuchaguzi nchini Uganda

McLaren

JF-Expert Member
Joined
Feb 19, 2025
Posts
889
Reaction score
2,863
Wakuu,

Mkuu wa Majeshi Uganda, Muhoozi Kainerugaba, ameibua mjadala mkubwa baada ya kuandika ujumbe kwenye mtandao wa X akidai kuwa ana mamlaka ya kumzuia Robert Kyagulanyi Ssentamu, maarufu kama Bobi Wine, kushiriki tena katika chaguzi za Uganda.

Kupitia ujumbe huo uliowekwa mtandaoni Januari 22, 2026, Kainerugaba alisema kuwa haijalishi kama Kyagulanyi yupo ndani au nje ya nchi, yeye kama CDF anaweza kumzuia kushiriki shughuli zozote za uchaguzi kwa kile alichokiita maslahi ya usalama wa taifa na manufaa ya nchi.

photo_2026-01-23_08-34-06.jpg


photo_2026-01-23_08-34-02.jpg
 
Uganda na tanzania tunaongozwa na vichaa wavaa suti na ushungi...
 
Uganda na tanzania tunaongozwa na vichaa wavaa suti na ushungi...
Inawezekana kabisa hata raia hatuna akili timamu 🤔 ikawaje tukubali kuongozwa na vichaa?
 
Uganda na Tanzania tunapngozwa na jeshi. Kwa sababu tanzania asilimia 70 ya viongozi wakiwemo mawaziri ni usalama wa taifa.
 
Back
Top Bottom