Mtoto wa Kitanzania alamba Shavu la kuigiza HOLLYWOOD

Bilionea Asigwa

JF-Expert Member
Sep 21, 2011
16,510
28,416
kENSwhBJ-LEUUTYsmvjim5_AjEU91eGI4yeRrhnzkrE6gADpS6YgKHkKXyrAbmNcxblWQU1ekyX7UfRNmBloaayWvhnvkj9GEjI_iYVJ-Q_-Mvm7yZ0j3-S-m2JPtB5E1fHNOXDUWMhcMNXtAg


Tasnia ya filamu Tanzania(Bongo Movie) inazidi kukua kwa kasi, si tu nyumbani hata nje ya nchi watanzania wanazidi kung’ara. Safari hii mtoto wa kitanzania aitwaye Evan Byarushengo amabahatika kupata nafasi ya kushiriki katika filamu ya kimarekani iitwayo THE REAL MVP: The Wanda Durant Story.

Filamu hii inajaribu kuonyesha jinsi mama wa mchezaji nyota wa mpira wa kikapu Kevin Durant alivyohangaika kuwakuza watoto wake mpaka kufikia kuwa mastaa. Evan anaigiza kama Kevin Durant akiwa mtoto wa miaka 7. Waigizaji wakuu wa filamu hii ni pamoja na Cassandra Freeman anayeigiza kama mama Evan; Pauletta Washington (mke wake Denzel Washington) ambaye anaigiza kama bibi yake Evan na wengine wengi.

Pamoja na kucheza filamu hiyo pia Evan amefanya audition nyingi kwa hiyo Mungu akipenda ataonekana kwenye matangazo ya kibiashara na filamu nyingine nyingi zaidi.

Source: Dewji Blog
 
Sasa kuna uhusiano gani Kati ya bongo movies na Mtanzania aliyezaliwa USA??? Si ajabu hata huyu hajawahi fika TZ
 
Back
Top Bottom