Kurzweil
JF-Expert Member
- May 25, 2011
- 6,622
- 8,397
Kwa mujibu wa hii video, Mwekezaji raia wa Denmark analalamika kuhujumiwa na Mtu aliyemtaja kuwa ni Twaha Mfaume Kawawa.
Jamaa aliwekeza kwenye sekta ya kilimo kwa miaka 5 na kuajiri Watanzania, anakiri walifanya kosa kubwa kukubali kuwa na ubia na Mtanzania.
Mtoto wa Kawawa alitaka kugombea hivyo akaomba fedha kutoka kwenye Kampuni lakini walipomkatalia alichukua hela kwa nguvu
Walipoona amekuwa tatizo walimuomba arudishe hisa alizopewa bure kisha alipwe Milioni 8. Anaeleza kuwa ametumia jina la Kawawa kupenya Uhamiaji, Mahakamani na TRA kumhujumu mwekezaji huyu.
Mwekezaji huyu anaomba msaada wa Rais Magufuli ili aweze kurejea na kuuokoa mkopo wake aliouchukua kutoka benki moja huko kwao Denmark.