MTO RUAHA

MTO RUAHA

KAKA NASOKI

Senior Member
Joined
May 25, 2016
Posts
191
Reaction score
212
jana nimeuliza mradi unaonyonya maji yote ya mto Ruaha na kuua Ruaha Natinal Park naona sipati majibu. TTB mpo? NEMC je? Miliasili ipo?
 
jana nimeuliza mradi unaonyonya maji yote ya mto Ruaha na kuua Ruaha Natinal Park naona sipati majibu. TTB mpo? NEMC je? Miliasili ipo?
Hivi kumbe bado mazingira ya mto Ruaha yanaharibiwa? Mie nilidhani hali yake imeshaboreshwa.
Kwa kweli mamlaka husika zinatakiwa kuchukua hatua stahiki mapema. "Uhai wa mazingira ni muhimu kwa uhai wetu".
 
jana nimeuliza mradi unaonyonya maji yote ya mto Ruaha na kuua Ruaha Natinal Park naona sipati majibu. TTB mpo? NEMC je? Miliasili ipo?

Kuna channels za umwagiliaji mpunga zimejengwa huko Pawaga, so zinafyonza kiwango kikubwa cha maji ya mto huo kabla hayajafika mbugani!!

Wakati ule wizara ya utalii ililalamika kuwa almost 70% ya maji yanapotelea huko!!

Lakini kumbuka mji wa Iringa na vitongoji vyake wanategemea maji ya Ruaha pekee, mfumo wote wa mabomba katika mji huo jua maji yametokea Ruaha mtoni!! Japo hii ni percent ndogo sana ya maji inayotumika.

Miaka ya nyuma kulikuwa kuna majadiliano ya wizara zipatazo nne kama sikose kuhusu huo mto na matumizi yake!! Umegusa wizara ya Utalii (Ruaha Mbuga), Wizara ya maji na umwagiliaji (Pawaga Sewage), Wizara inayo deal na Mazingira na Muungano (Ihefu) na Wizara ya Ujenzi kama sikosei ( kuna jenzi zinazotegemea huo mto).

Kila wizara inaona matumizi yake ni halali 😀😀😀
 
Back
Top Bottom