Mtandao gani zaidi ya jamii forums?

Mtandao gani zaidi ya jamii forums?

Status
Not open for further replies.

newazz

JF-Expert Member
Joined
Mar 28, 2009
Posts
932
Reaction score
941
Imejidhihirisha yenyewe kwenye kipindi hiki ambacho JF ilikuwa kwenye matengenezo.

Watu wamekosa kitu fulani . Ni nini hasa walichokosa?

Ni kule kujua habari ambazo pengine hazipatikani kwenye vyombo vingine vya habari?

Tetesi.

Kujua nini kinaendelea sehemu mbalimbali duniani au hata nchini.

Sehemu ya kukutana na marafiki .

Sehemu ya kubarizi.

Kweli nguvu ya mtandao ni kitu kingine.

Kuna ule uhakika kwamba , nikiingia JF nitapata habari na sitahangaika huku na kule, bali yote yapatikana hapa JF.

Kweli kuna mambo yasiyofurahisha ya watu kutumia propaganda kubeza , kuponda wengine na sehemu ya kujifunza.

Yote kwa yote, JF inabakia sehemu ambayo unaweza ukapata mengi , kama kianzio halafu ukiendelea na utafiti wako binafsi utapata kile unachohitaji. Unaweza ukapima pumba ni zipi na mwisho wa siku ukapata kitu kizuri.

Hongera kwa maono washika maono wa JF, na wachangiaje wengine humu ambao wanafanya JF kuwa mahali sahihi pa kujifunza na kupata habari. Ujuzi wa kutoa, kujenga hoja, vyote vinapatikana hapa JF.
Changia JF ni nini hasa kwako, ulichokosa katika kipindi chote. Naamini mrejesho wenu utatumika kuifanya JF kuwa forums bora zaidi na hata watu kuuliza ni mtandao gani bora zaidi ya JF?
 
hahahaha waliifunga jf kidogo ili kupima upepo... duuh hali ilikuwa tete mara tutakuwa hewani baada ya masaa 48 cha kila nusu saa nikawa naingia kucheki kama wapo hewan
 
Na imewezesha wengine kuwa Bibi na Bwana.....mi naushahid wa wanandoa waliojuana kupitia JF Private msg na mpaka sasa wamekuwa mume na mke na mtoto mmoja...So JF Inabid ianzishe jukwaa la USHUHUDA watu waje wasimulie jinsi JF ilivyo wasaidia maishan .Duh JF bana hata mimi nimepata marafiki kadhaa wa katumiana salamu kupitia JF....
 
Dunia imehamia huku, jukwaa hili ni muhimu kwa maana ya kupata taarifa na uzoefu nje ya uwanja wa watu unaowajua.
 
Na imewezesha wengine kuwa Bibi na Bwana.....mi naushahid wa wanandoa waliojuana kupitia JF Private msg na mpaka sasa wamekuwa mume na mke na mtoto mmoja...So JF Inabid ianzishe jukwaa la USHUHUDA watu waje wasimulie jinsi JF ilivyo wasaidia maishan .Duh JF bana hata mimi nimepata marafiki kadhaa wa katumiana salamu kupitia JF....

Hapa umenena Mkuu!
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom