Naomba mnisaidie kipengele cha kutakata katika bao la kete. Shida yangu ni kujua kipengele cha kutakata katika hatua ya kwanza ya mchezo wa bao. Je ikiwa unatakata ukatua kwenye jumba ni lazima kulala au unaruhusiwa kuzoa jumba na kuendelea kutakata ukipenda?
Mi si mchezaji wa bao lakini kuna app /Android game nimelitengeneza ambalo binadamu anacheza vs AI. Kwa sasa linatumia sheria ya uhuru wa "kulala" kwenye jumba au ukitaka unazoa jumba na kuendelea kutakata. Tazama hiyo picha, mfano nataka kutakata kuanzia chumba chenye kete mbili kuelekea kwenye jumba.
So, hapo nataka sheria ambayo inatumika sana (na wengi) ili nikipata muda nibadilishe sheria iliyopo. App bado inamapungufu mengi kwakuwa mchezo wenyewe huu unasheria nyingi na zinachanganya na kila sehemu wanakanuni zao, so napata changamoto katika kuliboresha.
Link ya Playstore.
A bao game of mancala family