OCC Doctors
Senior Member
- Jul 20, 2018
- 114
- 172
'Linea nigra' (mstari mweusi"), ambao mara nyingi hujulikana kama mstari wa ujauzito, kwa kawaida unaoonekana kwenye tumbo. Ni mstari unaopita wima katikati ya tumbo kutoka eneo la chini hadi kwenye kitovu, lakini pia unaweza kujitokeza kutoka eneo la chini hadi juu ya tumbo. Kwa wanawake wajawazito, mstari huu unahusishwa na kuongezeka kwa homoni yenye kichocheo cha melanocyte iliyotengenezwa na kondo la nyuma (placenta), ambayo husababisha weusi wa mstari huo na ndio husababisha weusi wa chuchu kwa mjamzito. Linea nigra kawaida hupotea ndani ya miezi michache baada ya kujifungua.