Msoto wa Waajiriwa

pwilo

JF-Expert Member
Joined
May 27, 2015
Posts
11,585
Reaction score
14,669
Nawasalimu kwa jina la jamhuri ya muungano wa Tanzania na EID njema kwa waislamu wote na watanzania wote tuliobahatika kuiona siku ya leo.

Leo nataka niongee na ndugu zangu waliojiriwa katika sehemu mbalimbali nchini kwetu maana hakuna watu wanapitia kipindi kigumu kama watumishi na wafanyakazi wengine waliojariwa kwasababu kikawaida mishahara huwa inatoka tarehe 22 mpaka tarehe 25 kila mwezi.

Ikumbukwe mwezi huu ulikuwa na sikukuu mbili ilianza ile ya PASAKA kwa ndugu zetu wa kristo halafu ikafuatiwa na EID ELFITIR kwa waislamu na kama unavyojua kipindi cha sikukuu matumizi yanakuwa makubwa sana hvyo kufanya wafanyakazi kuwa na kipindi kigumu sana mtaani na kula msoto mkubwa kutokana na sikukuu mbili kugongana kwa pamoja.

Labda niwakumbushe tu watumishi na wafanyakazi wote hayo maisha na msoto mnaopitia sasa hivi ndio maisha mtakayoishi baada ya kustaafu kwa hyo akili kichwani mwenu ila inakuaje mtu anafanya kazi miaka 10 lakini mshahara ukichelewa siku mbili tu wanaanza kulalamika inakuwaje hili wazee maana mshahara wa mwezi umeisha kabla haujatoka kwa madeni waliyonayo watumishi.

Kiufupi hichi kipindi ndio cha kujiandaa na kutafakari maisha yako kabla ya kustaafu maana watumishi mnajisahau sana ila inakuaje SERIKALI inashindwa kuwapa wafanyakazi wake angalau mkono wa sikukuu na badala yake wananunua magoli ya simba na yanga million 10 hivi nani alituroga watanzania tupo kama mazuzu vile.

Pesa zenu za NHIF,NSSF zinachotwa mpo tu zile ndio mlitakiwa muwe na uwezo wa kukopa kipindi kama hichi bila riba ili ziwasaidie ila wengine wanachota bila uoga halafu wahusika mnabaki tu kuishi maisha ya taabu na kulalamika na kusubiria siku ya mei mosi kupewa kofia na T shirt.

Poleni watumishi na wafanyakazi wote kwa msoto mnaopitia nyinyi na watu muhimu sana kwenye taifa letu siku mkijatumbua.

Alamsik na EID njema from my family to yours.
 
W
Wamekusikia mkuu
 
Aisee mbona unatusema bro.

What is salary is something which comes like a tortoise and goes away like a rabbit.
Ila asante kwa ushauri hamna kitu kizuri kama una business zako pembeni hata salary ikitoka hushituki..
 
Sasa na tusio na ajira rasmi tusemeje ndugu? Bora kenda kuliko kumi nena rudi
 
Sasa na tusio na ajira rasmi tusemeje ndugu? Bora kenda kuliko kumi nena rudi
Mkuu waajiriwa ndio wanaojisahau ila wanaopambana mtaani wanajua uhalisia wa maisha.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…