Msomi Ajitosa Kugombea Udiwani


Wakuu wengi wa mikoa au wilaya ni wastaafu jeshini.

Lakini utakuta wanaitwa mkuu wa mkoa xyz Kanali mstaafu..... au meja general mstaafu.... Inaudhi kweli kweli
.
 
Wakuu wengi wa mikoa au wilaya ni wastaafu jeshini.

Lakini utakuta wanaitwa mkuu wa mkoa xyz Kanali mstaafu..... au meja general mstaafu.... Inaudhi kweli kweli.

Hata pale Bungeni kuna akina Profesa Mwandosya, Profesa Msola, Profesa Mwalyosi, nk. Lakini hawa watu walishaondoka vyuo vikuu, hawafundishi tena. Profesa ni mwalimu wa chuo kikuu vipi uko bungeni unajiita profesa?
 
Msomi my foot, if not just another fisadi in the making. Jamani msomi gani tena huyu, what lecturer can stoop so low - strike me pink, yaani udiwani kwa tiketi ya.... just look at him, yeah take a good good look !

Umesahau kwamba unit ya maendeleo ni mitaa ambayo iko chini ya madiwani? Ukiwa na wasomi (degree na kadhalika) basi angalau hiyo mipango miji itakwenda shule.

Mbona Morogoro mjini ina Meya Profesa na hamukusema kitu? Angalau Morogoro inaanza kupata mwelekeo kidogo.
 

Wajameni, huyu si kaka yangu wala mtoto wangu wala sina undugu naye, ni majina yetu tu yanafanana fanana.

Hata huvyo wote tunaishi Magomeni na ninamfahamu. Isitoshe ninamuunga mkono kama msomi kugombea udiwani.

Mtakumbuka nilipokuwa nikiijadili hotuba ya Raisi, nilizungumzia juu ya Halmashauri za miji. Na nilishauri kuwa masharti ya kigezo cha ELIMU kiwekwe katika kugombea UDIWANI. Kwani siku za nyuma madiwani wengi walikuwa ni vijana wa vijiweni.

Nashukuru kuwa kabla ya sheria hiyo kuwekwa, wananchi wameamua kujitosa wenyewe, sasa unafikiri hapo kuna wakijiweni tena atachukua fomu. Thubutu!!!!

Anayechukia neno WASOMI shauri yake, lakini kwa maoni yangu ni muhimu kwani hata Nyerere alichoshwa katika utawala wake kuona kuwa wanasiasa walikuwa watu mambumbu kwa kipindi kirefu. Na mara walipoingia kwa wingi wasomi hakujizuia, na akasema 'ONENI MLIKUWA MNASEMA CCM NI YA WAJINGA, SASA WAMEJAA WASOMI'.

Acheni wajitangaze ili wasomi wengi wingie kwenye siasa. Neno Dr, Prof, msomi yatakwisha yenyewe pale ambapo wasomi watakuwa bwetele. Kwani siku hizi nikitembelea nyumba za wasomi wengi, sioni Degree zikibandikwa ukutani kama ilivyokuwa kawaida ya akina 'NJOMILE´ katika miaka ya 80.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…