MSEKWA: Hatuhitaji KATIBA MPYA

amakyasya

JF-Expert Member
Joined
Jun 26, 2013
Posts
3,480
Reaction score
918
Asema "Sababu zilizolazimisha kuundwa mara mbili tangu uhuru kwa sasa hazipo"
Source : MWANANCHI gazeti la leo jtano june, 25, 2014
 
hawa ccm tulishasema wamefikia kikomo cha kufikiri, si wazee si vijana, akili zao wote sawa,
 
Nilivyomsikia Rais wangu alivyofungua Bunge nikajua hakuna kitu hapa, lakini ni vizuri akajitahidi kuacha kumbukumbu nzuri ya katiba na ujenzi wa barabara ya Arusha Musoma.
 
Kwa vile wanataka kutawala milele hawaoni sababu ya katiba mpya? Kwa vile wao wako huko juu na hawajui au hawaoni tulio chini tunavyoteseka kwa sababu ya katiba isiyokidhi? Wenyewe wangeifuata katiba iliyopo ingekuwa afadhali lakini wapi watu wanateswa, wanapigwa mabomu, wanavunjiwa makazi yao bila fidia wao wanaangalia. Wananchi wanalalamikia muundo wa muungano wao kimya! Mfumo mbovu wa serikali wa mawaziri kuwa wabunge wao wanauona sawa ili mawaziri wasiwajibishwe na mengine mengi tu as per Tume Ya Rasimu Ya Warioba!
TZ tunataka katiba mpya itawaamsha viongozi waliolala au wasiojitambua.
 
Ndungu watanzania wote mwenye macho haambiwi ona, ukawa waliwambia ccm wanavuluga upatikanaji wa katiba mpya sisi tunabisha! Sasa hiyo kauli ameongea wazi kuwa hawataki katiba mpya. Kweli katiba sio hitaji la watanzania? Tuyafanyeje haya majangili yanayo tumia pesa nyingi kwa katiba hewa?
 
Nchi hi watanzania tumezubaa mpaka basi,huyu mpuzi hakuwa na haki ya kupanua mdomo kusema hayo. Tumpe adhabu gani yeye na wahuni wenzie?
 
Kama uzee unafanya mtu kuwa hivi, bora ufe mapema kuliko kujidhalilisha kiasi hiki. Daima huwa nasema vijana kuwaachia wazee uongozi na kufanya maamuzi ni kama kukumbatia virus kwani hawa wazee hana dreams tena.

Mzee msekwa tunakuheshimu sana, bora ukae kimya kuhusu swala la katiba mpya. Istoshe wewe haitakuhusu sana maana umeshafika jioni, unachofikiria ni utalalaje?
====================================



Chanzo;Mwananchi
 
Hoja ya Mzee Msekwa inautata mkubwa na inaashiria changamoto kubwa ya kupata Katiba inayofaa kwa nchi yetu. Umuhimu wa kuwa na Katiba Mpya unaeleweka na kila mtu na ndiyo maana watu walijitokeza kwa wingi kushiriki kutoa maoni nakadhalika. Yaelekea kwa kuwa rasimu iliyotolewa haiwapendezi wengi walio kwenye madaraka aidha uwezekano wa kufanya marekebisho makubwa sana unaonekana mgumu, kwa hivyo pole pole hoja inaanza kujengwa ya kuwa hakuna haja ya kuwa na Katiba Mpya. Kwa maana nyingine inafanana na ule usemi "kwa kuwa sisi hutukupata basi hakuna atakaepata" Hii kwa kweli ni aibu na fedheha kubwa. Ingefaa wote wanaohusika wakatafakari na kukubali kuangalia maslahi ya nchi kwa miaka mingi ijayo na tuache ubinafsi.
 
Waafrika ni wabinafsi sana. Yaani yeye keshapata anaona wengine hawastahili kupata. Maana kiukweli, kwa mfumo wa kikatiba uliopo, ni kwamba mtoto wa maskini ataendelea kuwa maskini milele, mfumo umejaa kulindana na kuogopana. Wanaolindwa ni Magamba na wanaoogopwa ni magamba ambao jeshi, polisi magereza mahakama vyote vyao. Vyote hivyo vinafanya kazi dhidi ya wanyonge na maskini. Katiba mpya walao imeshaonesha mwanga kidogo, lakini kwa sababu wanyonge hawana haki mijitu kina msekwa na wenzake wanafanya juu chini kuhujumu hatua muhimu ya kumuinua mwananchi mtanzania.

Ee Mungu tuepushe katika vishawishi, tusije watenda hawa wazee kitu mbaya...
 
hata mimi naunga mkono wa kutoandika katiba mpya bora hizo hela ingetumika kuboresha huduma za maji elimu afya na kilimo
 
Na bado alitowa maoni yake kwa tume ya warioba? mbona hakuyasema haya? Au ndio kaoteshwa leo?

 
Huyu mzee kigeu geu. Hana tofauti na H Mwakyembe. Ukitumikia CCM ni sawa unatumikia shetani maana inabidi ufuate usicho amini na ukane unachoamini.
 
Ingekuwa Kenya sijui kama huyu mzee angerudi nyumbani kwake salama bila kupata bakora mbili tatu -- yaani watu wameshatumia karibia billion 300 then mtu unakuja na kauli ya kejeli namna hii kweli?

Watanzania tuwe makini mno na wazee wa namna hii!! wanaweza kuhatarisha amani ya nchi yetu wakati wowote.
 
Huyu mzee kigeu geu. Hana tofauti na H Mwakyembe. Ukitumikia CCM ni sawa unatumikia shetani maana inabidi ufuate usicho amini na ukane unachoamini.
Tunaweza kuyadharau haya mawazo kwa sasa lakini kama alivyosema Mh. Komba juu ya kuingia msituni, ni wazi wasimamizi wa machafuko kwa jina la kulinda amani wapo wengi. Vijana kuuweni macho.

 
huyu mzee ameshafaidi pesa nyingi kutoka kwenye serikali ya ccm haoni umuhimu wa katiba mpya mbona hakusema mapema amesubiri mpaka wameshatumia karibu billioni 200 ndo anaibuka huu ni unafiki mkubwa
 
huyu mzee ameshafaidi pesa nyingi kutoka kwenye serikali ya ccm haoni umuhimu wa katiba mpya mbona hakusema mapema amesubiri mpaka wameshatumia karibu billioni 200 ndo anaibuka huu ni unafiki mkubwa

wewe taja kitu maalum ambacho katiba itanufaisha taifa.ukweli ni kuwa katiba ni mradi wa watu katika harakati za kisiasa majukwaani.mtanzania hanufaiki chochote.hili suala lifutiliwe mbali tuendelee na mambo ya maana.hata hii habari ya vitambulisho vipya vya kura ni ulaji tu.tukamilishe vitambulisho vya kitaifa na vitumike hata kwenye uchaguzi
 
hata mimi naunga mkono wa kutoandika katiba mpya bora hizo hela ingetumika kuboresha huduma za maji elimu afya na kilimo

Kwa heshima kabisa namuomba mwenye nchi asitishe hili zoezi la katiba mpya.hiki ni kichaka cha kutuchanganya na kuharibu fedha za serekali.hakuna manufaa yeyote kwa nchi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…