Msaada wako wa mawazo unahitajika hapa.

Msaada wako wa mawazo unahitajika hapa.

prax

Member
Joined
Mar 13, 2013
Posts
27
Reaction score
8
Habari wanajamvi,
Mimi ni mwanamke mwenye umri wa miaka 26.Miaka minne iliyopita nilikuwa na boyfriend ambae nilimpenda sana lakini kwa bahati mbaya katika safari yetu ya mapenzi ilidhihirika wazi kuwa hakuwa na mapenzi ya dhati kwangu kwa sababu nilikuja kugundua ana msichana mwingine.Kwa kifupi alinisumbua sana hadi ikafikia kipindi akaniambia nimpe space maana anaona kama ananiumiza na hawezi kumuacha huyo msichana mwingine.Niliumia sana,nikawa najaribu kumove on lakini nikawa nashindwa kwa sababu bado nilikuwa nampenda.
Baada ya muda kupita nikakutana na mwanaume mwingine,alikuwa ni mtanashati na mwenye tabia njema tu,kijana huyu niliwahi kusoma naye sekondari ila yeye alinizidi kidato kimoja mbele.Nadhani kutokana na upweke niliokuwa nao nilijikuta naanzisha naye mahusiano na kidogo kidogo nilianza kumpenda ingawa mawazo ya yule wa mwanzo yalikuwa hayajaniisha bado.Katikati ya mahusiano haya mapya niligundua pia huyu mwenzangu yuko katika mahusiano na msichana mwingine.Kwa jinsi nilivyokuwa na stress,sikutaka hata kumuuliza kwani nilijiona sikufanya jambo la kunipa afadhali bali kuniendelezea maumivu yaliyopita.Kwa hiyo nikaanza kumuacha kimyakimya kwa kupunguza mapenzi na mawasiliano pia ili niweze kutulia na kuweza kuanza upya.
Wakati napitia hayo yule boyfriend wa mwanzo alirudi kwangu akionyesha kujutia makosa yake,aniomba msamaha na kuahidi kwenda kujitambulisha kwetu tayari kwa kufunga ndoa.Sijui ni kwa ajili nilimpenda sana au umburula wangu nikajikuta nimemsamehe na kurudisha mapenzi kama mwanzo,huku nikitafuta sababu ya kumwacha yule mwanaume mwingine.Kiukweli nilimtafutia kila sababu ya kumwacha lakini ilishindikana kwani naye alibadilika akaonyesha mapenzi kwangu sana na akawa mkweli kuhusu mahusiano aliyokuwa nayo kwamba ni girlfriend wake ambaye hakuwa happy katika mahusiano yao ndiyo maana aliamua kuwa na mimi na kwa sasa amaeamua kumwacha kabisa ili awe na mimi.Kiukweli nikijikuta katika dilemma kubwa sana.
Nilishirikisha Mungu katika hili kwani nilijikuta nachoka kudate nao wawili kwa wakati mmoja (hata sijui kwa nini nilikuwa sikamatwi).Ninakiri kwamba nilichokuwa nafanya si kizuri ila nimeamua kuwa muwazi ili niweze kusaidiwa.Baada ya mwaka na nusu nikiwa katika hali hiyo,nilikuja kugundua huyu boyfriend wa mwanzo niliyemsamehe yuko kwenye mahusiano na mwanamke mwingine na wapo kwenye mchakato wa kufunga ndoa.Nilipomuuliza alinijibu wazi kuwa ni kweli na tuachane mazima.Niliumia na kulia sana,na ilinichukua muda mrefu kurecover ila mwisho wa siku ilinibidi nikubaliane na ukweli na maisha yaendelee.Nikabaki na huyu kaka ambaye kiukweli mapenzi yake kwangu hayajawahi kupungua,sasa mimi nikawa natumia efforts nyingi kumpenda.Cha kushangaza ni kwamba kadiri siku zinavyokwenda mapenzi yangu kwake ndo yanazidi kupungua.Ni karibu mwaka sasa sijielewi kabisa,sina feelings naye kabisa na yeye hata halioni hilo badala yake yeye kila kukicha ndio anazidihsa mapenzi kwangu.
Sasa ndugu zangu,kilichonileta kwenu ni kuomba ushauri na kujua kama kuna mwenye experince na hii scenario.Je nimwache niendelee na maisha yangu?Au niendelee naye labda kuna siku moyo wangu utafunguka kwake?Ananipenda na anataka kwenda kwetu kujitambulisha,lakini ndi hivyo hata sex si enjoy mpaka siku nyingine nasingia naumwa mradi tu nisikutane naye.Ungekuwa wewe ni mimi ungeendelea naye?Au hii imetokana na yule niliyempenda akanitenda?(ANGALIZO:HUYU NI RAFIKI YANGU ANAOMBA USHAURI).
 
Ameshazoea kuumizwa huyo, anataka wa kumliza, siku iz marafiki wanaomba sana ushauri. Aisee.
 
Mh! Hii Kesi Imekaa Kiutata Sana
Mi Nakushauri Muombe Sana Mungu Wako Akupe Njia Ya Kweli...Kwani Ianaonekana Bado Hujui Nini Unataka Kwa Sasa
inaonekana Umeathirika JKisaikolojia Hivyo Kukosa Kabisa Mapenzi Na Mwanaume(Hii Hari Ni Hatari Sana)
Fanya Hima Umuweke Wazi Mpenzio Na Umwambie Akupe Nafasi Ubaki Mwenyewe Mpaka Akili Itakapokukaa Sawa
Ahsante Jigo
 
kushi mara moja tu
kupanga ni kuchagua kama unafikiri kuna mwaka tena umri wako utakuwa miaka 26 utajuta
 
Sasa prax...

Mwambie huyo "rafiki" yako kuwa

Kwa kuwa amezoea kuumizwa....amuache huyo kaka

Ataishia kufanywa hawara mpaka akizeeka atamwagwa

Ukioendwa pendeka

Au amekulia kwenye nyumba ambayo baba daily anamuumiza mama ndio maana anayakumbatia mateso????

Huyo kaka wa pili kampenda afungue moyo wake ampende
 
Muone mtaalamu wa saikolojia.....na umshirikishe mungu ktk maamyzi yako
 
Usimuumize kijana wa watu na kumpotezea muda.
Yaelekea ameshapitia mengi. Name kitendo unachofanya Sasa so sahihi.

Ushauri wangu ,
Wewe ni mtu mzima, na yeye pia kaeni chini muongelee hili.
Mwambie kabisa hujisii jinsi yeye anavyojisikia kwako na usingependa
Kumpotezea muda wake , ungependa kumuacha aendelee na maisha yake bila wewe.

Halafu ushauri mwingine,
Kuwa mwanamke jasiri, usiache moyo wako ukupe majibu ya kila kit maishani..
Tumia akili zaidi Moyo unahuruma na unaweza kukufikisha usipopenda.
 
We mwenyewe hujielewi sasa sisi tusemaje jamani? Muache tuapate ampendae maana wake za watu mnaogongwa ovyo mtazidi kuongezeka mnoo. Ndo mambo kama yako, mke wa mtu chupido mkononi.
 
We mwenyewe hujielewi sasa sisi tusemaje jamani? Muache tuapate ampendae maana wake za watu mnaogongwa ovyo mtazidi kuongezeka mnoo. Ndo mambo kama yako, mke wa mtu chupido mkononi.

Mi kilichonichanganya zaidi ni huo mpokezano wa vikojoleo.........aisee.......kweli ukimwi hakuna.......
 
Kinachonishangaza ni wewe na rafiki yako kuwa na tatizo linalofanana....

Rafiki yaki naye kaanzisha uzi akitaka ushauri wa jinsi ya kukusaidia....
 
Mi kilichonichanganya zaidi ni huo mpokezano wa vikojoleo.........aisee.......kweli ukimwi hakuna.......

HAINAGA MAKOMBO ILE YAHEEEEEEEEEE! Ikioshwa kama mpyaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa!
 
Hebu na amshirikishe Mungu kwa mara nyingine tena.....ila dah inahitaji moyo uliyokufa ganzi kumshirikisha Mungu katika mambo ya uzinifu
 
Yaaani kuna watu 24/7 wanawaza mapenzi

Wewe huna hata ndoto ya kuja kumiliki Ipsum au Spacio jamani(Range HSE haitawezekana nina uhakika manake kichwa kimejaa kugegedana tuuuu)
 
HAINAGA MAKOMBO ILE YAHEEEEEEEEEE! Ikioshwa kama mpyaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa!

Natamani hayo uliyoyaandika hapo ingekuwa ni audio au video. Yaani kuna jamaa nimemmechisha na hayo maneno na jinsi ambavyo angeweza kuyatamka live....hahahhhaaa
 
Kinachonishangaza ni wewe na rafiki yako kuwa na tatizo linalofanana....

Rafiki yaki naye kaanzisha uzi akitaka ushauri wa jinsi ya kukusaidia....

hahahahah...uzi Upi Huo Chief?
 
Mimi sioni cha kukushauri maana yote yako mikononi mwako, halafu muache tabia ya kuwasingizia marafiki
 
Back
Top Bottom