mimi ni mwanamke nina miaka 37 sasa hv. nimeolewa na nina watoto watatu. miaka 17,13 & 6yrs. nimeishi na mume wangu kwa miaka 18 sasa hivi. mume wangu ni maasai wa mjini sio wale wavaa lubega.
tatizo ni huyu baba nimembeba sana mpaka naona nimechoka na vile umri umeenda sijui nifanyeje. sio mwanaume muwajibikaji kabisa. hajui ada za waotto zinatoka wapi, chakula, maendeleo ndani ya nyumba, hajui chochote yeye ni kama mtallii. hata akiona pazia liko upande hatengenezi au chumba hakina bulb hajigusi. ni ww ndio ufanye. ada za waotto ndio kabisa akijatahidi sana kama ada ni laki 4 bac atatoa laki 2 tena kwa shida na kwa awamu. akikuta hela zako au pochi umeweka vibaya anaruka mpaka na hela zako. sio muwajibakaji hata tone yeye ni starehe na starehe na yeye. ni kwlei nimevumilia sana tokea mwanzo ila mbona naona kama siwezi tena? mzigo umenilemea na hana msaada wewe ndio ukimbizane waotto watakula nini, watasomaje, watavaa nini, nyumba inaitaji nini etc. ndoa ni kwa shida na raha. nimejenga nyumba mwenywe na kila kitu nimefanya mwenywe tena yeye ulikuwa ukimpa hela ndio anaenda kulewa, mpaka leo ana miaka 43 sasa hivi ni wa kurudi usiku wa manane. nimechoka kuvumilia jamani namuambia aondoke aniache maana nyumba ni ya watoto na ni nguvu yangu mwenywe hataki. ukipika chakula akikuta anakula hajui hata kinatoka wapi. juhudi zote za maendeleo na watoto ni mimi mwenywe. haya maisha yamenichosha sana jamani nifanyeje nimejikuta simpendi tena kabisa na sina hamu nae kabisa hata ya mapenzi. sina mpenzi wa nje bac tu nimeona huu ni mzigo ambao umefika mwisho. nataka nimuche nafanyaje na yeye ndio amekataa kutoka ndani ya nyumba kabisa? nimechoka kweli kwlei. toka kanioa ni ile miezi ya awali ndio alishawahi nitoa out. sikubmuki hata mara ya mwisho aliniambia mke wangu twende out ni lini, au tukaka kupanga maisha/maendeleo ya watoto au chochote ni lini. mimi ndio wakukimbizana na maendeleo ya shule ya watoto. kila siku nikuomba kulipa ada kwa instalment. nimekua ndio kama niko peke yangu yeye akija usiku na mtungi wake ni kelele na kulala. yuko kama vile anaishi guest. akija usiku saa zingine fujo na kelele. sikumbuki hata mara ya mwisho ameshawahi nipa laki ya matumizi au hata elfu 50 ni lini? akitoa hela ya chakula ni elfu 20 kama mara ya mwisho kanipa miezi 2 iliyopita. jamani hebu nishaurini nifanyeje?????? hata nikiwa na msiba kwetu hakanyagi wala haudhurii.