Msaada wa mawazo kuhusu ICT project for final year

Dah i wish ningejua kufanya programming hata kwa php tu. Nyie mnazungumzia python sahivi!
 
[emoji106] [emoji106] .
 
Huko chuoni mnasomaga php tu??

Huwa mnaboa sana na hizi comments za kukariri, kuponda PHP kisa mumeona wengine wakisema. Mimi nimetumia PHP miaka mingi na nina mifumo ya maana ikiwemo hata ya kiserikali ambayo inatumika hadi leo na mpaka sasa naitumia PHP bila kujutia.

Anyway mleta mada uskiomae tu mawazo ya aina ya mradi, kumbuka chuoni huwa wanafuatilia vitu vingi, bora ufanye simple project lakini uzingate kila kitu ipasavyo, documentation zako uziweke zikae, utolee maelezo ya ulivyoanza na inception report, halafu feasibility ukafuatia requirements gathering na analysis, hapa ndio madogo wengi huangukia pua hata huku nje, unakuta dogo katengeneza mfumo bila kutumia muda wake kuelewa tatizo lipi mfumo unatatua.

Utolee maelezo ya system design, chora workflow zote na use cases, zitolee maelezo yaliyosheheni. Ingia kwenye developement, onyesha ulivyozingatia good practices za systems engineering, jinsi umetumia design patterns zinazowezesha mfumo wako uwe extendable, scalable na kadhalika

Kumbuka pia tests ni muhimu sana, zitolee maelezo UAT na SIT na nyinginezo, pia kumbuka taarifa za user guide na technical guide. Elezea changamoto ulizobumbana nazo kama scope creep na ulivyozishughulkia, onyesha uelewa wako wa methodologies ulizotumia kama Agile.

Mfumo wako unaweza usiwe complex, uwe simple lakini wakufunzi wanachoangalia ni jinsi gani ulivyojiandaa kwa ajili ya soko na kama hutajenga mifumo inayoishia kuhangaisha walaji badala ya kuwasaidia.

Likija suala la ideas, waza kuhusu simple system ambayo inakwamua jamii na kuwa na output, impact na outcome yenye tija. Mfumo ambao hata vijijini utawafikia jamii bila kutegemea internet kwa sana, kwamba inaweza ikatumia SQLITE offline na baadaye sync ikipata internet.
Kuna kero nyingi sana vijijini, mtu unakatiza umbali kwenda kutafuta dawa ulizoandikiwa, na kila zahanati unakuta hamna zimeisha, sasa vipi ukatengeneza mfumo ambao kwa kutuma SMS moja, ninaweza nikajua wapi nina uhakika wa kupata dawa ninazosaka.
 
Duh!!
 
shukrani
 
Hey kiongozi, recently kuna mambo yanasemwa katika mitandao like unaweza kuwa programmer japo wa kiwango cha kati, je ili kuweza kufanya kama hayo uliyoyataja itatumia muda gani, sina background but najifunza python mwenyewe kama mwezi sasa, na naona ugumu mkubwa sana.
 

Haha sasa wanayosema watu mimi yana msaada gani? Nina maisha yangu, nakula, naishi, nalala vizuri, sina shida, hayo maneno ya watu yananipunguzia nini?

Programmer wa kiwango cha kati na juu ndiyo yukoje? Programming ni field pana sana, wapo waliobobea kwenye programming finance software, systems, web, networking, wengine maisha yao yote wanatengeneza compilers tu ukiwapeleka kwingine hawawezi, wengine data, e.t.c fields zipo zaidi ya elfu. Unatumia kigezo kipi kusema huyu ni wa kiwango flani? Hahaha watu mnapoteza muda kudiscuss kiwango cha mwingine badala ya kukaa mkafanya self improvement. Ndiyo maana wengi wanaishia kuomba misaada humu kila siku kua maisha magumu. Wabongo bna.

Umesoma Python mwezi, bado sana. Mwezi programming hautoshi, em rudi tena baada ya miezi mingine 23 alafu tuendelee kuongea. Usikate tamaa.
 
PAWAHOST.COM sasa inatoa offa kabambe kwa huduma mbalimbali,Kama ilivyoorozeshwa hapo chini:-
1. Utengenezaji wa Website kwa gharama kuanzia 150,000/=
2. Utengenezaji wa mifumo mbalimbali kama ya Kibiashara ,shule ,Hospitali 250,000/=
3. Utengenezaji wa Application Mbalimbali zinazoweza kuanzia 75,000/=
4. Utengenezaji wa forums na chatting websites 250,000/=
5. Website Kwa Ajili ya Kuuza Vitu Mbalimbali Online(Kama Amazon)=350,000/=

Pia tunatoa huduma ya Domain Reseller na Hosting kwa package zifuatazo:-
1 GB Disk Space
20GB Bandwidth
UNLIMITED Email Accounts
Free Data Backup
Free SSL Configuration per domain

Kwa package hizo za hosting zilizoainishwa hapo juu gharama ni kuanzia 60,000 Tu kwa Mwaka,Tupigie sasa kwa namba +255687 535650 ,Email :info@pawahost.com ,Website :www.pawahost.com
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…