kwa swali la kwanza.
i. Ni muhimu sana kwanza wewe mwenyewe kuwa umefanya ushushu mapema katika hilo kampuni, kujua scale zao za mishahara na kwa levelo yako ya elimu. Ulipopigiwa tu simu ya kujiandaa na usaili ulipaswa uanze kudodosa kujua ABC.. za hilo kampuni na scale zao, namna linavyofanya kazi linahusika na nini etc. Otherwise unaweza jikuta hata ukiaambiwa ueleze unavyolifahamu hilo kampuni, labda ungeweza kukwama. Hivyo siku nyingine chunguza mapema shughuli za hilo shirika, na kujua hata average salaries kwa levelo yako ya elimu na uzoefu wako.
ii. Ukishindwa kupata taarifa za awali juu ya hilo shirika na scale mishahara yao, basi sasa unajiangalia wewe mwenyewe, uwezo wako, kipi hasa unajua katika hiyo nafasi uliyoomba. Ni muhimu sana kujua ni vitu gani katika tangazo walisema vitakuwa added advantage (ie labda una lesseni ya nkuendesha gari au unajua lugha za kigeni zaidi ya mbili, au uzoefu wa kufanya kazi sehemu hiyo mradi/shirika linapotaka kukupeleka etc). Ukiona unasifa nyingi wanazo zihitaji basi nawewe unaringa kidogo katika kutaja figure (mshahara), lakini pia ni muhimu kujiangalia levelo yako ya elimu, uzoefu, na kwa wakati huo unaofanya usaili je uko na kazi nyingine, au ndiyo hiyo chance imetokea kama bahati kuitwa na ulikuwa mtaani kwa miaka. Kama umekuwa mtaani kitambo sana na huna uzoefu basi taja figure ya kawaida tu kulingana na levo ya elimu yako na aina ya course/masomo uliyosomea, ie. Ukiacha fani za uinjinia, na afya, fani zingine kama unacertificate, unaweza omba gross ya laki 5, kama Unadiploma unaweza omba laki 7, kama una degree unaweza omba gross ya milioni 1 hadi 1.5 kwa kuanzia etc
SWALI LA PILI
Hilo swali huwa linalenga hasa, kutaka kujua strenght zako yaani ndipo pale juu nilieleza JE una kitu gani cha ziada?? Yaani kwa mfano mko watu 100, na wanataka mmoja, sasa why wawaache wale 99 na wakuchukue wewe. Hapo ndipo linapokuja JE sifa ulizo nazo zinaendana na sifa za tangazo lao?? Je walisema kuwa kama mtu anajua hiki na hiki huyo atakuwa assets/ yaani ndio yale mambo ya added advantage, ie wewe una sifa za ziada labda uko ujuzi na aina hiyo ya miradi, au uliwahi fanya kazi sehemu fulani mradi kama huo na ukaacha success 1, 2, 3...., au wewe labda unajua sana kuandika proposal, au unauwezo mkubwa wa kusolve migogoro hapo lazima ucite mifano ya mafaniko yako. Kikubwa lazima uhakikishe vitu utakavyo visema kama sifa za ziada kwako, lazima viwe vinamatch na malengo ya kazi uliyoomba.
Nadhani nimekusaidia kidogo, mengine wajuzi wataongezea
======