MWANDENDEULE
JF-Expert Member
- May 24, 2015
- 5,122
- 10,302
Salam kwenu nyote!
Ndugu naomba msaada wa kimawazo juu ya kozi hizi za biashara: ACCOUNTANCY na BUSINESS ADMINISTRATION katika suala zima la ajira; ni ipi kati yake iliyo rahisi kupata ajira, na ipi nzuri kui-apply katika biashara binafsi.
Naombeni msaada wenu wataalam na wazoefu wa kozi hizi kuna mdogo wangu kasema nimfanyie application kwa kozi moja kati ya hizo ngazi ya cheti. mimi napenda baadae aitumie knowledge atakayopata katika biashara zake binafsi badala ya kuajiriwa na mtu ama kampuni.
Businesa administration ni nzuri
Chagua ukawa maisha yako yote ili tukitoe chama cha sisiem madarakani
CCM itang'oka tu hata kabla ya October 25 na hilo nalipigania sana lakin hebu tusaidizane katika hili la kozi kwanza.
BUSINESS ADMINISTRATION itakuwa ndo chaguo zuri maana hata accountancy ipo ndani yake, ila ukifika mbeleni unaweza specialize katika kitu kingine utakachoona kina faa.
kwa kujiajiri, business administration itakusaidia sana inakila kitu mjasiria mali anahitajika ajue
kila la heri.
Kwa ngazi ya Cheti, kama anajua hesabu na yuko serious, bora asome accountancy. Itamsuidia atakapotaka kujiendeleza. Business Administration is too wide, ndio maana at degree level inakua na specialisations kama accountancy, procurement, banking and finance. Mtu aliesoma certificate ya accountancy anaweza kufanya Business administration at degree level kwenye yeyote kati ya hizo specialisations.
Nimesoma CBG alaf nimechaguliwa business administration hii inetokea baada ya kumuachia mtu anifanyie application nilipokua jkt...Kwa ngazi ya Cheti, kama anajua hesabu na yuko serious, bora asome accountancy. Itamsuidia atakapotaka kujiendeleza. Business Administration is too wide, ndio maana at degree level inakua na specialisations kama accountancy, procurement, banking and finance. Mtu aliesoma certificate ya accountancy anaweza kufanya Business administration at degree level kwenye yeyote kati ya hizo specialisations.
Haina shida kabisa. Mwaka wa kwanza utaonekana mgumu kidogo, sababu mtasoma Financial Accounting. Ila kama ukiweka muda wako vizuri Accounting kwa level ya chuo haina shida saana, na haifai kiogopa. Ila kama ukiona ina kusumbua, mwaka wa pili unaweza kuchagua specialization nyingine kama Marketing au Procurement ambazo hazina accounting. Sijui umechaguliwa chuo, maana kuna vyuo BBA unaspecialise tangu mwaka wa kwanza. Ila kama sio chuo kama hicho, basi mwaka wa pili utajua uelekeo.Nimesoma CBG alaf nimechaguliwa business administration hii inetokea baada ya kumuachia mtu anifanyie application nilipokua jkt...
Msaada wa ushaur nikisoma haita nisumbua?
Nimechaguliwa MUST mkuuHaina shida kabisa. Mwaka wa kwanza utaonekana mgumu kidogo, sababu mtasoma Financial Accounting. Ila kama ukiweka muda wako vizuri Accounting kwa level ya chuo haina shida saana, na haifai kiogopa. Ila kama ukiona ina kusumbua, mwaka wa pili unaweza kuchagua specialization nyingine kama Marketing au Procurement ambazo hazina accounting. Sijui umechaguliwa chuo, maana kuna vyuo BBA unaspecialise tangu mwaka wa kwanza. Ila kama sio chuo kama hicho, basi mwaka wa pili utajua uelekeo.