Msaada wa dawa za warts

Msaada wa dawa za warts

baba mausingizi

Senior Member
Joined
Jun 15, 2016
Posts
189
Reaction score
120
Niingie tu kwenye mada nasumbuliwa na vidude vinaota kwenye ngozi nimeenda hospital wanasema zinaitwa warts sijui kama sijakosea na kilikuwa kimoja kwa sasa vinafika kumi na mbili, dokta alisema vinatakiwa vichomwe.

Je, hakuna njia nyengine mbadala? Msaada mwenye kujua.
 
Nilikuwepo navyo hivyo kwenye vidole vya mikono haviumi lakini vinakera sa vingi vingi vikubwa na vidogo vinachipukia.

Pona yangu nilipataga ajali katika kutibiwa majeraha zile sindano na madawa nikashangaa na vyenyewe vimepotea vyote mwaka wa saba huu.
 
Niingie tu kwenye mada nasumbuliwa na vidude vinaota kwenye ngozi nimeenda hospital wanasema zinaitwa warts sijui kama sijakosea na kilikuwa kimoja kwa sasa vinafika kumi na mbili, dokta alisema vinatakiwa vichomwe.

Je, hakuna njia nyengine mbadala? msaada mwenye kujua.
Hello habari yako? pole kwa hayo maradhi yanayo kusumbuwa nitafute kwa wakati wako ili nipate kukutibia maradhi yako upate kupona.
 
Nilikuwepo navyo hivyo kwenye vidole vya mikono haviumi lakini vinakera sa vingi vingi vikubwa na vidogo vinachipukia.
Pona yangu nilipataga ajali katika kutibiwa majeraha zile sindano na
madawa nikashangaa na vyenyewe vimepotea vyote mwaka wa saba huu.
Duh
 
TUMIA Mexican Poppy (Argemone mexicana (Papaveraceae)). Tumia utomvu wake kupaka kwenye hilo eneo lenye tatizo mara 3 kwa siku.
Capture.PNG
 
Niingie tu kwenye mada nasumbuliwa na vidude vinaota kwenye ngozi nimeenda hospital wanasema zinaitwa warts sijui kama sijakosea na kilikuwa kimoja kwa sasa vinafika kumi na mbili, dokta alisema vinatakiwa vichomwe.

Je, hakuna njia nyengine mbadala? msaada mwenye kujua.
Habari!
Pole kwa kuumwa.
Dawa zipo kuanzia za kupaka, kupunguza kwa baridi, kupunguza kwa umeme, kukata nk.

Warts ni suala ambapo unapata diagnosis sahihi kupitia kuona kitu husika. Pia, njia gani utumie hutegemea na kiasi/ukubwa vs wingi na eneo.

Hivyo, kama uko sehemu ambayo kuna kituo cha afya ni vyema kupata ushauri kutoka kwa mtoa huduma ya afya kulingana na hali ilivyo hasa ikibidi kama unaweza kumpata daktari bingwa wa ngozi.
 
Habari!
Pole kwa kuumwa.
Dawa zipo kuanzia za kupaka, kupunguza kwa baridi, kupunguza kwa umeme, kukata nk.

Warts ni suala ambapo unapata diagnosis sahihi kupitia kuona kitu husika. Pia, njia gani utumie hutegemea na kiasi/ukubwa vs wingi na eneo.

Hivyo, kama uko sehemu ambayo kuna kituo cha afya ni vyema kupata ushauri kutoka kwa mtoa huduma ya afya kulingana na hali ilivyo hasa ikibidi kama unaweza kumpata daktari bingwa wa ngozi.
Asanteee mkuu
 
Mi niliambiwa huu mmea nkawa natumia utomvu wake ilinisaidia.
JPEG_20220928_191835_976750985.jpg
 
Back
Top Bottom