Sioni kama kuna sababu ya kuogopa kupokea simu. Ila unaweza kufanya haya yafuatayo:
1. Acha kabisa tabia za utani na yeye
2. Mkataze kupiga simu usiku
3. Akikupigia simu na kuanza mambo yake mwambie wazi kuwa wewe ni mume wa mtu na huna mpango wa kuwa na mahusiano nje ya ndoa kwa namna yeyote ile. Mpe makavu. Na kama ataendelea utaacha kupokea simu zake na pia utatoa taarifa kwa mkeo ambaye ni rafiki yake.
Mwanaume hupaswi kuwa muoga muoga, simu yako halafu unaogopa kupokea? Fikiria, ukiacha kupokea halafu akatumia simu ya mtu mwingine, ukipokea utakata? Au utajibu nini? Akina dada wanaweza kutumia technique hii ya kuacha kupokea simu ila kwa wewe kaka, no! Huu ni mtazamo wangu binafsi!