Msaada: Nimetapeliwa kupitia mtandao!

Kiukweli njaa imezidi Jana tu imenipigia hiyo mitapeli inajitambulisha inatoka tigo makao makuu niakamuuliza kuna shida gani jamaa akaniuliza leo umetoa au kupokea pesa nikamwanbia nimepokea na kutoa pesa kidogo akauliza kwahiyo huna pesa kwenye CM nikamwambia ipo akauliza kama ngapi nikamwambia yanini akaanza oh kuna mtu katumiwa pesa kimakosa nikamuukiza yananihusu nini mimi akasema niusalama wa account yako nikamwambia me matapeli hawezi kunitapeli kilahisi vire kusikia neno tapeli kaikata CM faster ni Jana tar 5 mwezi wa 3
 
Pole sana. Hiyo biashara ina changamoto sana hasa kwa vijana wanaoajiriwa kuiendesha. Mara nyingi wanadanganywa kuwa kuna kamisheni inatakiwa kuwa activated nao wanaingia tamaa kuwa ikiingia basi wanaikomba bila wewe kujua. Basi wanaanza kuelekezwa waingieze codes mwisho wa siku wanahamsha pesa kutoka katika mitandao yote kama ni M pesa, Airtel Money au Tigo Pesa. Wewe jipange upya tu ukiaanza kufuatilia hayo utapoteza muda bure hata wewe kama wakala mtu akitoa pesa kwako huwezi kusaidia kumtambua hata kama amesaini kwa kuwa matapeli wanasajili namba nyingi za kufanyia kazi kwa majina bandia na vitambulisho bandia. Umeshapigwa basi usipoteze muda wako!
 
Pole sana Mkuu ilishawahi kunikuta hiyo, lkn sio kwa style hiyo. Kuhusu polisi nakushauri achana nao, na naweza kusema kwa kiasi kikubwa polisi wanachangia huu wizi uendelee. Mimi baada ya Pesa zangu kuhama. Nilifuatilia mpaka nilijua simu 10 anazowasiliana Mara kwa Mara. Nilipata hadi eneo alikozitolea. Tatizo ilikua polisi tu twende tigo wakaombe kuwasha GPS ili kumtrace yuko wapi. Polisi wakawa wanataka niwape laki 3 ya mafuta sijui, wakati Mimi nimeshapata hasara ya milioni moja.
 
Asante mkuu,, ushauri mzuri

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nashukuru mkuu,,, nmeshajeruhiwa lakini nadhani ni muda wa kupambana na hawa watu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Haya ameyasema muheshimiwa Rais juzi,kuwa kwenye jeshi la Polisi kuna udhaifu mkubwa,angalia comments za watu hapo juu,kila mmoja baada ya kujua kesi iko polisi wanashauri aachane na hilo jambo asonge mbele na misha yake...
Teknolojia ni kubwa lakini jeshi letu halijawa tayari kuitumia

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hapana hujatapeliwa bali umechomoa!
 
Kwa hiyo hukuwakamata?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Polisi utapata msaasa na wahalifu watakamatwa usiwe na shaka
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…