Msaada engine 1NZ-FE

Msaada engine 1NZ-FE

shegacool2015

JF-Expert Member
Joined
Feb 6, 2014
Posts
394
Reaction score
133
Jamani habari zenu, naomba msada, gari yangu spacio engine 1NZ inatatizo la kukata kuwaka nikiwasha asubuhi battery haiwashi mpaka ni boost, nimenunue battery ya maji N40 lakini tatizo linaendelea, sometimes inawaka kipindi kingine inakata.

Nilipo nunua battery wamepima wananambia battery nzima ila wakipima wanasema tatizo ni alternator kwakua output yake ni 13.2 in ashuka 13.09, kumpelekea Fundi kapima na yy then kasema alternator iko weak niyakutengenezwa, bada ya kuifungua kacheck then kasema anaona ni nzima japo inatoa output ndogo inawezekana ndio mfumo wake,

kwa hioo ninue battery kubwa Kama N50 niweke tatizo litaisha...sasa hapa kama sijaelewa vizuri, naomba ushauri kwa wanao elewa vizuri.....
 
Kama upo Dar Nenda ofisi za chloride exide pale Millennium business Park shekilango. Wanauza batteries ila pia wanatoa ushauri kuhusu matatizo yaliyo battery related. Mimi walishahi kuniambia gari yangu inahitaji battery kubwa zaidi N50 kwakua ni cc 2000.

Ila kwa spacio N40 should be enough. I know several people wenye spacio na hawajahitaji kuweka battery kubwa.
 
Ukiona hupati ufumbuzi nenda mtaa wa lindi kwenye used engines,ununue alternator pale uone kama itaendelea kusumbua au fungua starter ichekiwe huenda ikipata baridi kunakua na mgando fulani unaozuia starter kuzunguka kwa urahisi hadi ipate joto
 
Mzee kama ni Spacio old model tatozo itakua ni brash , mm ilishawahi kunitokea. Yaani gari kama hutumii itawaka.lakini ukiitembelea ingine ikiwa imoto haiwaki.
 
Mzee kama ni Spacio old model tatozo itakua ni brash , mm ilishawahi kunitokea. Yaani gari kama hutumii itawaka.lakini ukiitembelea ingine ikiwa imoto haiwaki.

Ni new model, inawaka ikiwa yamoto...
 
Hilo tatizo ni alternator, nenda kapime hio gari ujue tatizo nini halafu upate fundi asome code zake thn urekebishe tatizo. Hao mafundi njaa siku hizi hakuna mtu makini anaewapa gari
 
Hukututajia engine CC, maana hapo ndipo ingekuwa starting point ya kujua kwa nini betri yako haiwashi hiyo gari.

Cha zaidi, kama betri inashindwa kuwasha gari kuna matatizo makuu 2 au 3, moja betri ni ndogo kwa engine (hii itajionyesha haraka wakati betri itakapoanza kuchoka) mbili Betri imekufa na tatu alternator ni mbovu haichaji betri vizuri.
 
Mpigie huyu fundi atatatua tatizo lako na kukupa ushauri 0714 426 636
 
Back
Top Bottom