Mradi wa DART ulishakufa kabla ya kuanza, zilizibaki ni harakati za MFA MAJI

kidadari

JF-Expert Member
Jul 26, 2012
8,647
9,601
Toka mradi wa dart umeanza kwa ujenzi wake kulikuwepo na changamoto nyingi zikionyesha dhahiri kuwa hakukuwa na matayarisho ya kutosha kabla ya kuanza rasmi mradi huo.

Yafuatayo ni mambo yanayoonyesha udhaifu huo.

Kuanza kwa mradi huu baada ya kutumika kwa nguvu za ziada ziara za kushukiza,kutumbuliwa kwa baadhi ya vigogo wa mradi huo, hii ina maana mradi huu ulikuwa bado kuanza ila umeanza kwa nguvu ya ziada.

Upana wa barabara unatia shaka kwa kile kinachoitwa mradi wa mwendo kasi ili hali upana wa barabara hizo haumruhusu dereva kutembea kwa 100km/hr huo ni mwendo kasi gani???

Ubora wa magari bila shaka yana kiwango kinachotiliwa shaka. Kwa ajali chache tena sio za kutisha magari haya yameshindwa kabisa kuonyesha ubora wake, hapa tunaona lifespan ya mradi huu utavyokuwa Mdogo! bora Eicher kuliko haya.

Sheria kibao na matamko yanayoashuria kujihami kwa watawala utadhani mradi huu ni Mkubwa kuliko yote nchinj hata ule wa gasi asilia, mara ibeni tairi za magari yanayokatiza barabara hizo, Sasa kuna sheria inayoletwa ukiingia barabara hizo fine ni 300,000 ila haisemi chochote endapo magari kasi yakigonga magari binafsi, wala kama gari ina comprehensive insurance. Hii ina maana gani? Unfair

Magari kasi hayana Breki? nimeshuhudia ajali kadhaa ambazo kweli gari moja dogo liliingia barabara ya mwendo kasi ila kwa kiburi dereva wa gari kasi hakuhangaika kufunga breki mpaka ajali inatokea. Hii itachangia uharibifu wa magari haya na kuathiri mradi huu!

Huu ni mradi wa serekali au mtu binafsi? Maana kama ni wa serekali tulitegemea namba za magari zisimeke STK au SU.

Hapa panatia shaka endapo ikitokea mgongano wa kimashali au kubadilika kwa utawala!

Ongeza changamoto nyingine.
 
Yaani ni kama kuna hujuma. Haiwezekani karibu kila wiki kuna tukio la ajali linalohusisha dart
 
Toka mradi wa dart umeanza kwa ujenzi wake kulikuwepo na changamoto nyingi zikionyesha dhahiri kuwa hakukuwa na matayarisho ya kutosha kabla ya kuanza rasmi mradi huo.

Yafuatayo ni mambo yanayoonyesha udhaifu huo.

Kuanza kwa mradi huu baada ya kutumika kwa nguvu za ziada ziara za kushukiza,kutumbuliwa kwa baadhi ya vigogo wa mradi huo, hii ina maana mradi huu ulikuwa bado kuanza ila umeanza kwa nguvu ya ziada.

Upana wa barabara unatia shaka kwa kile kinachoitwa mradi wa mwendo kasi ili hali upana wa barabara hizo haumruhusu dereva kutembea kwa 100km/hr huo ni mwendo kasi gani???

Ubora wa magari bila shaka yana kiwango kinachotiliwa shaka. Kwa ajali chache tena sio za kutisha magari haya yameshindwa kabisa kuonyesha ubora wake, hapa tunaona lifespan ya mradi huu utavyokuwa Mdogo! bora Eicher kuliko haya.

Sheria kibao na matamko yanayoashuria kujihami kwa watawala utadhani mradi huu ni Mkubwa kuliko yote nchinj hata ule wa gasi asilia, mara ibeni tairi za magari yanayokatiza barabara hizo, Sasa kuna sheria inayoletwa ukiingia barabara hizo fine ni 300,000 ila haisemi chochote endapo magari kasi yakigonga magari binafsi, wala kama gari ina comprehensive insurance. Hii ina maana gani? Unfair

Magari kasi hayana Breki? nimeshuhudia ajali kadhaa ambazo kweli gari moja dogo liliingia barabara ya mwendo kasi ila kwa kiburi dereva wa gari kasi hakuhangaika kufunga breki mpaka ajali inatokea. Hii itachangia uharibifu wa magari haya na kuathiri mradi huu!

Huu ni mradi wa serekali au mtu binafsi? Maana kama ni wa serekali tulitegemea namba za magari zisimeke STK au SU.

Hapa panatia shaka endapo ikitokea mgongano wa kimashali au kubadilika kwa utawala!

Ongeza changamoto nyingine.


Duh! Hao ndiyo Waafrika bhana, halafu tunalilia usawa kwenye hii Dunia wakati tumejaa negativity kuanzia unyaoni mpaka utosini, khaa nimechoka!!!
 
Huu ni mradi wa serekali au mtu binafsi? Maana kama ni wa serekali tulitegemea namba za magari zisimeke STK au SU.

Hapa panatia shaka endapo ikitokea mgongano wa kimashali au kubadilika kwa utawala!

Ili swali linahitaji jibu la nyongeza mheshimiwa
 
Huu ni mradi wa serekali au mtu binafsi? Maana kama ni wa serekali tulitegemea namba za magari zisimeke STK au SU.

Hapa panatia shaka endapo ikitokea mgongano wa kimashali au kubadilika kwa utawala!

Ili swali linahitaji jibu la nyongeza mheshimiwa
wakija hapa watajaa povu bila kutoa hoja! kama ungekuwa ni wa serikali sheria Kali zisingewekwa kama tulivyozoea
 
Duh! Hao ndiyo Waafrika bhana, halafu tunalilia usawa kwenye hii Dunia wakati tumejaa negativity kuanzia unyaoni mpaka utosini, khaa nimechoka!!!
sio hivyo ni changamoto zilizipo but Niambie huu mradi ni wa serekali au dili la mtu?
 
Yaani ni kama kuna hujuma. Haiwezekani karibu kila wiki kuna tukio la ajali linalohusisha dart
lakini ukiangalia kwa umakini hata Hao madereva wa dart wanafanya fujo njianj......rejea uda walivyokuwa na kiburi kipindi kile.
 
Wewe zile gari ikienda mbio unaona kifo live bila chenga hilo jina la mwendo kasi nimbwembwe tu ila ukweli nigari lisilokaa kwenye foleni na lina punguza karaha kwa kweli
 
Mleta mada ni kiazi, jua tu kuwa wewe ni kiazi, ukileta mada maana yake angalau umefanya uchunguzi kidogo ili kuondoa yale maswali na hoja zenye pumba, you didn't do that. Wewe ni kiazi sana!!
 
Kwa jinsi watu wa Kimara & Mbezi walivyopunguziwa kero ya usafiri nimeamua kuwasamehe dhambi zao wote wanaotuhumiwa kuhusu mradi.
 
lakini ukiangalia kwa umakini hata Hao madereva wa dart wanafanya fujo njianj......rejea uda walivyokuwa na kiburi kipindi kile.
fujo gani ?ushawahi kuyapanda au?wanafuata sana sheria na ndio maana walifanya training bila abiria wiki mbili q
 
Sijui serikali ifanye kitu gani mtoe pongezi, jitu linalalamika wakati Na yeye linapanda, jenga ya kwako basi tuone bwege wewe
 
Mreta mada hajafanya reseach ata kidogo kakurupuka mradi ni wa dart ambao ni mawakala wa serikali 49% na udart 51%
 
ulianza kukwama kwenye barabara zenyewe nakumbuka rc kandoro alishangaa sana siku ya kwanza bahati mbaya aliishia KUSHANGAA TU
 
Mtoa mada umeshaambiwa kama huna vigezo vya kuendelea kusoma pale udom tafuta chuo kingine na sio udom...haya mengine waachie wenye vigezo
 
lakini ukiangalia kwa umakini hata Hao madereva wa dart wanafanya fujo njianj......rejea uda walivyokuwa na kiburi kipindi kile.
Yap namaanisha madereva aidha wao wenyewe au kwa kushirikiana na wengine wanafanya hujuma. Yaani kuna ajali zingine unaona mtu anafanya kwasababu anajua hata ajali ikitokea hatakuwa na hatia kwa sababu yupo kwenye barabara yake. Inakuwa kama mabasi hayana breki.
 
Yap namaanisha madereva aidha wao wenyewe au kwa kushirikiana na wengine wanafanya hujuma. Yaani kuna ajali zingine unaona mtu anafanya kwasababu anajua hata ajali ikitokea hatakuwa na hatia kwa sababu yupo kwenye barabara yake. Inakuwa kama mabasi hayana breki.
Upo sahihi sana mkuu sababu hawa madereva wameaminishwa kuwa wao ndo wenye haki na huwa hawakosei hata ikitokea gari imeingia barabara ya mwendo kasi kimakosa hawachukui tahadhari yoyote
 
Back
Top Bottom