Wolle Melkas Fernando
JF-Expert Member
- May 4, 2016
- 279
- 389
Mpina kuvaa Tshirt yenye picha ya hayati Magufuli anaweza kuwa ni 'Right Person in the wrong Party'
Luhaga Mpina ni mgombea Urais kwa Chama Cha ACT wazalendo. Tangu akiwa Mbunge Mpina ni mtu aliyejitanabahisha kuwa ni mfuasi wa falsafa za uongozi wa Magufuli.
Sidhani Mpina kama amepata muda wa kusoma itikadi na falsafa za Chama chake kipya Pamoja na kupitia misimamo ya viongozi wake wa Chama kuhusu utawaka wa Serikali ya awamu ya Tano mbayo iliongozwa na Dr. Magufuli.
ACT ni Moja ya Chama kilichokuwa mstari wa mbele kupinga vikali misimamo ya Magufuli na namna yake ya Uongozi.
Ni ACT hiyo hiyo iliyokuwa ikipinga msimamo wa Magufuli kuwachukulia hatua Mafisadi Kwa kusema Serikali ya Magufuli ilikuwa inakiuka Haki za Binadamu.
Ni ACT hiyo hiyo ambayo ilipinga vikali zoezi la Serikali ya Magufuli kuwaondoa wafanyakazi waliokuwa wameajiriwa kwa mbinu za kughushi vyeti vya taaluma ambapo lengo la Magufuli lilikuwa ni kuboresha weledi na ufanisi wa utendaji wa kazi Katika kuwahudumia Wananchi.
Ni ACT hiyo hiyo iliyopinga msimamo wa Magufuli wa kutokusafiri nje mara kwa mara kwa lengo la kubana matumizi.
Na hata baada ya Kifo Cha Magufuli, Kiongozi wa ACT Wazalendo Zitto Kabwe ambaye pia ni muasisi wa hicho chama alinukuliwa akisema "Kama Kuna watu walimpenda sana, na wao waende kaburini wakazikwe naye"
Leo hii Mgombea Urais wa ACT mwenye itikadi za uongozi wa Magufuli aliyepigwa vita na Chama hichohicho, amevaa T-shirt yenye picha ya Magufuli.
Hii kwetu sisi Wahafidhina inatupa tafsiri kwamba Mpina anaweza kuwa ni mtu Sahihi aliyepotea Chama. "Right Person in The Wrong Political Party"
Luhaga Mpina ni mgombea Urais kwa Chama Cha ACT wazalendo. Tangu akiwa Mbunge Mpina ni mtu aliyejitanabahisha kuwa ni mfuasi wa falsafa za uongozi wa Magufuli.
Sidhani Mpina kama amepata muda wa kusoma itikadi na falsafa za Chama chake kipya Pamoja na kupitia misimamo ya viongozi wake wa Chama kuhusu utawaka wa Serikali ya awamu ya Tano mbayo iliongozwa na Dr. Magufuli.
ACT ni Moja ya Chama kilichokuwa mstari wa mbele kupinga vikali misimamo ya Magufuli na namna yake ya Uongozi.
Ni ACT hiyo hiyo iliyokuwa ikipinga msimamo wa Magufuli kuwachukulia hatua Mafisadi Kwa kusema Serikali ya Magufuli ilikuwa inakiuka Haki za Binadamu.
Ni ACT hiyo hiyo ambayo ilipinga vikali zoezi la Serikali ya Magufuli kuwaondoa wafanyakazi waliokuwa wameajiriwa kwa mbinu za kughushi vyeti vya taaluma ambapo lengo la Magufuli lilikuwa ni kuboresha weledi na ufanisi wa utendaji wa kazi Katika kuwahudumia Wananchi.
Ni ACT hiyo hiyo iliyopinga msimamo wa Magufuli wa kutokusafiri nje mara kwa mara kwa lengo la kubana matumizi.
Na hata baada ya Kifo Cha Magufuli, Kiongozi wa ACT Wazalendo Zitto Kabwe ambaye pia ni muasisi wa hicho chama alinukuliwa akisema "Kama Kuna watu walimpenda sana, na wao waende kaburini wakazikwe naye"
Leo hii Mgombea Urais wa ACT mwenye itikadi za uongozi wa Magufuli aliyepigwa vita na Chama hichohicho, amevaa T-shirt yenye picha ya Magufuli.
Hii kwetu sisi Wahafidhina inatupa tafsiri kwamba Mpina anaweza kuwa ni mtu Sahihi aliyepotea Chama. "Right Person in The Wrong Political Party"