Mpenzi wangu simuelewi jamani naomba ushauri wadau

Mpenzi wangu simuelewi jamani naomba ushauri wadau

charle

Member
Joined
Sep 17, 2011
Posts
9
Reaction score
0
Habari zenu ndugu zangu .

Mimi nina mchumba wangu ambaye tunapendana sana lakini tunapishana kwa kitu kidogo sana yeye yuko mbali na mimi yeye yuko Dar es salaam mimi nipo Mtwara kwa hiyo huwa tunawasiliana mara kwa mara kwa kutumia simu siku tunaweza kuongea kama mara tatu sio siri nampenda sana mpenzi wangu lakini anawivu sana.

Sasa jana kama mida ya saa nne usiku nimepigiwa simu na boss wangu kutoka Dar es salaam kunitaarifu kwamba nikafanye installation ya internet kwenye hotel moja hapa Mtwara tuliongea kwa kirefu kidogo.

Baada ya hapo nikampigia simu mpenzi wangu kwa muda mrefu lakini hakutaka hata kupokea simu yangu na mpaka leo hii nimempigia hataki kupokea kabisa.

Sasa sijui nifanyeje wadau nampenda sana mpenzi wangu lakini tatizo ndio hilo tu linalo msumbua infact bado hatujaoana lakini tumeshapanga malengo mpaka mwaka fulani ndo tuoane.

Naombeni ushauri wenu ndugu zangu.
 
kama ana wivu mpuuze na wivu siku ikifika mtaoana lakini madhali umeshajua ana wivu chapa kazi yeye muache wivu wake ilimradi uwe muaminifu tu.
 
Sasa kama mtu anashindwa kuelewa nature ya kazi yako kuanzia sasa huyu kweli ataweza kua mke mwenye kustahmili?
Haya kama unampenda sana mueleze kua kazi yako unaweza itwa hata saa8usiku chamsingi akuamini tuu mbona wewe unamuamini na yuko mbali..au afanye yeye tuuuu...
 
charlee hujui kujieleza ila nmekuelewa, huyo mkeo tarajiwa hapokei simu without reasons according to maelezo yako, ww mtafute via her friends, facebooks au any other means, labda kafa huwezi jua, mtafute kw
 
Kwa hiyo unahisi tatizo ni kuwa alikupigia wakati unaongea na boss wako hivyo hakukupata?

Mwambie akue bana, mwambie maisha bila kutafuta hayana maana na kuwa mbali na mpenzi wako sio lazima kufanya madudu.

Suluhisho la kweli litaanzia kwenu wenyewe Mkuu, ongea nae ataelewa tu unless aliwahi kukukamata na kidumu
 
hapana mkuu hakuwahi kunikamata na kidumu ila ilitokea kwamba mimi niko na simu mbili moja kwa ajili ya matumizi ya office tu na nyingine ni yakwangu mwenyewe binafsi sasa wakti naongea nae kwenye ile simu yangu mara simu ya office ikawa inaita ikabidi nimuambie samahani kunasimu ya office nataka kuongea na boss nikimaliza nitakupigia sababu hata kama hii yakwangu nikiiacha hewani nitakuwa nakusumbua wewe kuweka sikioni kwa muda mrefu kwa hiyo ilinibidi nikate ile simu na kuongea na bosi baada ya kumaliza nillimpigia simu ndo hakupokea tena sister alipigia leo mchana akamwambia yuko hospitali wakati yuko kwenyegari anaelekea chuoni anakosoma alipata kizungu zungu hiyo aliishiwa nguvu na kwenda hospitali ndo taarifa nilizo nazo kutoka kwa dada yangu ambaye yuko dar es salaam
 
huyo hana wivu isipokua anatafuta sababu ya kukuacha inaonekana kuna mtu anakusaidia kwa mtu mwenye akili timamu mtu ameshakwambia bosi anapiga nitakupigia baadae unachonunia nini fanya uchunguzi wa hiki ninachokwambia hio ni sababu inatafutwa sasa je angempata mtu kama mimi ofisini kukaa ni week 1 au mbili muda wote ni kuzunguka mikoa tofauti tofauti kama kweli anapenda si angekufa na presha.........kuna watu imeshawatokea kama yako hio ni sababu inatafutwa jaribu sana kumchunguza na usifall in love 100% ndugu utaumia ...wahenga walisema fimbo ya mbali..........
 
Watu wa aina hiyo wapo wengi sana eti wanadai asiyekuonea wivu hakupendi.

Nadhani ni utoto tu, akikua ataacha.
 
Kiukweli sina lingine zaidi ya kusema nimeshiba kwa ushauri niliopata sasa napata moyo na nishafahamu nini ninatakiwa kufanya mpaka sasa.Nawapenda sana ndugu zangu
 
nyama huliwa na mtu ila chuma ndo huliwa na kutu,atakumbuka tu tundu liko wapi
 
Niwekee namba zake nikusaidie kurejesha mawasiliano mapema iwezekanavyo.
 
Achana nae huyo amesha dakwa na mapedeshee wa Dar.
 
huyo hana wivu isipokua anatafuta sababu ya kukuacha inaonekana kuna mtu anakusaidia kwa mtu mwenye akili timamu mtu ameshakwambia bosi anapiga nitakupigia baadae unachonunia nini fanya uchunguzi wa hiki ninachokwambia hio ni sababu inatafutwa sasa je angempata mtu kama mimi ofisini kukaa ni week 1 au mbili muda wote ni kuzunguka mikoa tofauti tofauti kama kweli anapenda si angekufa na presha.........kuna watu imeshawatokea kama yako hio ni sababu inatafutwa jaribu sana kumchunguza na usifall in love 100% ndugu utaumia ...wahenga walisema fimbo ya mbali..........

wewe huujui wivu wewe, hata mtu akisma anaongea na mama yake utaona sio kweli
 
Sasa jamani maisha yaku stress,mwanamke nae aku stress ivi utapata wapi amani? mwambie ukweli kua hupendi tabia yake na kama umeshampa assurence kua she is the one and only ndio atakupanda akikushuka,jikaze kiume mpe kweli kua kazi yako ni ya 24/7 na sidhani akam atakutaka kama ukiwa huna hela sasa kama hamuendani jipange Kaka bora ya nusu shari kuliko shari kamili..
 
Back
Top Bottom