Kibo10
JF-Expert Member
- Aug 20, 2013
- 11,278
- 8,868
Rafiki zangu, na wana jamvi wenzangu tujadili juu ya kauli ambazo zina ishara mbaya kwenye uhusiano tena za utapeli mtukufu.
Wakati mwingine unaweza kumsikia mpenzi wako akikuambia maneno ya ajabu sana, lakini si wote wanaweza kuelewa maana yake ni nini"MFANO"Mwenzi ambaye hana mpango tena na wewe,A.K.A (kukuchoka) anaweza kuanza tabia ya kukuonea kinyaa.
Na Maneno ya kejeli kwake yakawa si suala la kujiuliza mara mbili tena.
Ni rahisi sana kukuambia bila aibu unanuka.
Ebwanae unanuka jasho sana, hebu kaoge kwanza, iwe mwanamke au mwanaume anaweza kukuambia hivyo.
Katika hali ya kawaida kabisa hiyo ni dharau,Tena inawezekana labda mlikuwa katika hatua ya kuelekea kwenye mahaba, lakini ulipomsogezea kinywa chako, ukakutana na maneno haya:
"Aaaah! Mh...unanuka mdomo bwana, sitaki.
Hizi si kauli njema na bila shaka anajaribu kukuonesha jinsi ambavyo umepungua thamani kwake.(kakuchoka)Huwezi kunuka kwa mpenzi wako, siku zote huwa unanukia, lakini kama ameona dosari yoyote na yeye kama mwenzi wako wa karibu ana wajibu wa kuhakikisha anatumia lugha nzuri kukurekebisha.
Lakini kwa kuwa hana mapenzi ya ukweli na wewe tena hana haja ya kuonesha mapenzi yake kwako,anakubwatukia atakavyo ukiona mishe hizo zimeanza kuchukuwa nafasi kwenye mahusiano jiongeze mapema iwezekanavyo kabla mtu mzima hujaumbuka.
Kuchokana kwenye mahusiano ni hatari........sana..sana..sana.
Wakati mwingine unaweza kumsikia mpenzi wako akikuambia maneno ya ajabu sana, lakini si wote wanaweza kuelewa maana yake ni nini"MFANO"Mwenzi ambaye hana mpango tena na wewe,A.K.A (kukuchoka) anaweza kuanza tabia ya kukuonea kinyaa.
Na Maneno ya kejeli kwake yakawa si suala la kujiuliza mara mbili tena.
Ni rahisi sana kukuambia bila aibu unanuka.
Ebwanae unanuka jasho sana, hebu kaoge kwanza, iwe mwanamke au mwanaume anaweza kukuambia hivyo.
Katika hali ya kawaida kabisa hiyo ni dharau,Tena inawezekana labda mlikuwa katika hatua ya kuelekea kwenye mahaba, lakini ulipomsogezea kinywa chako, ukakutana na maneno haya:
"Aaaah! Mh...unanuka mdomo bwana, sitaki.
Hizi si kauli njema na bila shaka anajaribu kukuonesha jinsi ambavyo umepungua thamani kwake.(kakuchoka)Huwezi kunuka kwa mpenzi wako, siku zote huwa unanukia, lakini kama ameona dosari yoyote na yeye kama mwenzi wako wa karibu ana wajibu wa kuhakikisha anatumia lugha nzuri kukurekebisha.
Lakini kwa kuwa hana mapenzi ya ukweli na wewe tena hana haja ya kuonesha mapenzi yake kwako,anakubwatukia atakavyo ukiona mishe hizo zimeanza kuchukuwa nafasi kwenye mahusiano jiongeze mapema iwezekanavyo kabla mtu mzima hujaumbuka.
Kuchokana kwenye mahusiano ni hatari........sana..sana..sana.