MOROGORO: CHADEMA kuliburuza Jeshi la Polisi Mahakamani

Kurzweil

JF-Expert Member
May 25, 2011
6,621
8,411
Chama cha demokrasiana na maendeleo (CHADEMA) wilaya ya Morogoro kimekusudia kuliburuza Mahakamani Jeshi la Polisi wilayani humo kupinga hatua ya jeshi hilo kukinyima uhuru wa kampeni za uchaguzi mdogo wa udiwani wa kata ya kiwanja cha ndege kwa kutumia mabomu ya machozi na kuwakamata hovyo wanachama wa Chadema.

Akitoa tarifa kwa vyombo vya habari katibu wa Chadema mkoa wa Morogoro Bwana.Samwel Kitwika amesema chama kimefikia uamuzi huo kufuatia jeshi hilo kuonekana kuegemea upande mmoja wa chama huku akiitaka tume ya taifa ya uchaguzi kusimamia kwa uhuru na haki uchaguzi huo.

Mbunge wa viti maalumu mkoa wa Morogoro Mheshimiwa Devota Minja amewataka wananchi wa kata ya kiwanja cha ndege kuwa watulivu wakati wakijiandaa kuchagua kiongozi atakayewaongoza kwa manufaa ya wakazi wote wa kata hiyo.

Chanzo: ITV
 
Ikumbukwe bwana Mkubwa alshapga marufuku siasA adi 2020, kwaiyo police tusiilaumu sana jaman wanatekeleza agizo la malaika
 
Inshu iliyopo sasahiv ni mkakati wa kutokomeza chama cha cha Chadema kisiwepo katika ulingo wa siasa Tanzania ushahidi WA hili ni pale viongozi wa chadema wanaposhambuliwa kufungwa
 
Kumbania mtu haki yake ya kufanya kampeni ni kumpigia mtu huyo kampeni bila kujua!! Wapiga kura wameona na wameelewa!
 
Halafu mtu anasimama anatoa povu mimi ni wa wote, nawapenda wote, thubutu unafiki haujifichi. Halafu eti upigwe bomu kesho anakuambia umuombee. Ila ni bora hasemi aombewe dua ipi maana angesema dua njema ingekula kwake acha aombewe tu kulingana na matendo yake.
 
Wapinzani tuna hali ngumu sana sasa hivi. Hata tukienda Mahakamani nina wasiwasi ikawa sio suluhisho.
 
Chama cha demokrasiana na maendeleo (CHADEMA) wilaya ya Morogoro kimekusudia kuliburuza Mahakamani Jeshi la Polisi wilayani humo kupinga hatua ya jeshi hilo kukinyima uhuru wa kampeni za uchaguzi mdogo wa udiwani wa kata ya kiwanja cha ndege kwa kutumia mabomu ya machozi na kuwakamata hovyo wanachama wa Chadema.

Akitoa tarifa kwa vyombo vya habari katibu wa Chadema mkoa wa Morogoro Bwana.Samwel Kitwika amesema chama kimefikia uamuzi huo kufuatia jeshi hilo kuonekana kuegemea upande mmoja wa chama huku akiitaka tume ya taifa ya uchaguzi kusimamia kwa uhuru na haki uchaguzi huo.

Mbunge wa viti maalumu mkoa wa Morogoro Mheshimiwa Devota Minja amewataka wananchi wa kata ya kiwanja cha ndege kuwa watulivu wakati wakijiandaa kuchagua kiongozi atakayewaongoza kwa manufaa ya wakazi wote wa kata hiyo.

Chanzo: ITV
Kesi ya nyani unampelekea ngedere!
 
Inshu iliyopo sasahiv ni mkakati wa kutokomeza chama cha cha Chadema kisiwepo katika ulingo wa siasa Tanzania ushahidi WA hili ni pale viongozi wa chadema wanaposhambuliwa kufungwa
Me nilizani Unafunguka Huo Mkakati Kumbe Mwenyewe Unaishi kwa Matukio2
 
Back
Top Bottom