Mo anatengeneza mgogoro mwingine Simba

mo29

JF-Expert Member
Joined
Nov 21, 2025
Posts
384
Reaction score
518
Tayari Mo Dewji amepeleka mapendekezo kwenye bodi ya udhamini kutaka kujenga uwanja kwe uwanja wa Bunju. Simba imepata katiba mpya ambayo inataka mchakato wa uwekezaji uanze upya baada ya logo ya Simba ithaminiwe upya kupata thamani halisi ya Simba.

Pia imeondoa neno mwekezaji na kuwa wawekezaji. Mwenyekiti wa Simba ndio kuwa mwenyekiti wa Bodi.
Badala ya Mo Dewji kusubiri mchakato ukamilike tayari amepeleka mapendekezo kwenye bodi ya udhamini ya kutaka kujenga uwanja kwa masharti ambayo hayajawekwa wazi.

Kuna hatari akajenga uwanja ambao utakuwa kama uwanja wa Arusha kwa kuweka gharama ambazo haziendani na uhalisia ili awe na nguvu ya kuwacontrol pale mchakato ukianzA.

Wito wangu kwa mo Dewji asubiri mchakato ukamilike kwani kwa mujibu wa katiba mpya kiwanja cha Bunju na jengo la Msimbazi ni mali za wanachama haziguswi.
 
Mo hajawahi kuwa tatizo.
Tatizo la Simba lilikuwa ni Yanga kufanya vizuri baasi.
Siku Yanga na Simba zinaondolewa champions league na kelele za mangungu atoke zikafa rasmi.
 
"Simba
Mo Arena"
ndio jina zuli la uwanja

Uwanja mwingine unaweza kuitwa "Simba Mangungu Arena"

Jina la Simba linatakiwa kuwa mwanzo kwakuwa ndio Jina la Club:

Simba inaweza kuwa na Arena nyingi tu:

Mo Simba arena hapo inaonesha uwanja ni wa mtu binafsi:
Simba ni kubwa kupita mwekezaji ambaye anaweza kujiondoa hapo baadae na kufanya mambo mengine, huku simba ikiendelea kuwepo sambamba na wawekezaji wengine
 
Arsenal walipojenga uwanja na kuuita Emirates waliingia mkataba wa miaka mitano wakilipwa.
Mo amepewa jina bila kulipia chochote, mpira wa sasa hivi ni biashara wakati anapotoa pesa simba kila senti anahesabia na bado anakwambia anapata hasara huku simba inamtangaza bure
 
Leo Magori ameongea na waandishi wa habari ingawa lugha sahihi amewahutubia.
Moja ya mambo aliyozungumzia ni swala la mo kutaka kujenga uwanja, kubadiliaha matimizi ya pesa za mdhabuni za kujengea uwanja na kupeleka kwenye matumizi mengine na mchakato wa kuingiza wanachama wapya.
Kwa mujibu wa katiba mpya ilutopitishwa na msajili bodi iliyopo ni batili lakini inawezekana wanatumia busara kufanya utekelezaji wajati ligi inaendelea.
Katiba mpya imetamka wazi kiwanja cha Bunju na jengo la Msimbazi ni mali ya Simba na lisihusishwe jwenye uwekezaji.
Mo amekuwepo Simba toka mwaka 2018 na moja ya sababu ya yeye kushindwa kuwajengea Simba uwanja ni kutokamilika kwa mchakato wa uwekezaji. Baada ya kutolewa mwongozo mpya wa nini somba ifanye nilitegemea angeheshimu mamlaka na katiba ya Simba.kwanini ana haraka ya kuanza kuingia mikataba kabla hata tathimini ya logo ya simba haijafanyika?
Swala la wanachama si la bodi ya simba bali simba kupitiia mwenyekiti wao ndio wanatakiwa wasimamie.
 
Umesahau Jayrutt nae hataki kubaki nyuma
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…