Mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni

mwengeso

JF-Expert Member
Nov 27, 2014
9,227
6,670
Kilichotokea jana bungeni kwenye uchaguzi wa Wabunge wa Bunge la Afrika Mashariki (EALA) limeonesha kwamba vyama vya siasa vya upinzani vina viongozi wababaisha kuhusu demokrasia wanayodai haipo nchini.

Wakati CHADEMA inawasilisha majina 2 tu, na ya wanaume tu, yapitishwe bila kupingwa, CUF iliwasilisha majina ya CUF Maalim na CUF Lipumba.

Ni haohao viongozi wanataka tuwaamini kama watetezi wa demokrasia kwa kumkebehi, kumkashifu na kuchonganisha Rais Magufuli kwa wananchi waliomwamini na kumpa dhamana, kwa kura, kuongoza nchi hii.

Najiuliza, hivi hao viongozi wa upinzani wangepewa hiyo dhamana ya kuongoza nchi hii, wangeweza kweli kuunda safu ya kutatua matatizo sugu ya nchi hii, kama siyo kupata tiketi ya kuyafanya kuwa sugu zaidi!

Matatizo sugu ambayo Rais Magufuli, kwa utashi wake wa kisiasa (political will) na uthubutu wake binafsi anayashughulikia kuyatokomeza, kwa madaraka aliyo nayo Kikatiba, ni pamoja na:
1) Uozo uliotukuka Serikalini ikiwa ni pamoja na urasimu, uzembe, rushwa, ufujaji wa mali ya umma, na matumizi mabaya ya madaraka - silaha yake KUTUMBUA .
2) Kutamalaki kwa ufisadi - silaha yake ZIARA ZA KUSHITUKIZA
3) Vita dhidi ya buashara ya madawa ya kulevya - silaha yake KUWATAJA HADHARANI WAHUSIKA.

Mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni Rais Magufuli.

Na viongozi wa vyama vya siasa vya upinzani, hasa CHADEMA, mabingwa wa siasa za mitandaoni, vyombo vya habari, majukwaani na maandamano, tambueni UHARAKATI umepitwa na wakati. WAKATI UKUTA USIGOMBANE NAO.

Viongozi wa vyama vya siasa upinzani "Mfanye siasa kwa uhuru wa kujieleza Kikatiba. Ikosoeni Serikali kinaga ubaga, bila kuangalia aliyeko nyuma yenu, ilimradi mnafanya hivyo bila kuingiza uchochezi au maneno ya kashfa kwa viongozi wa Serikali" (Gazeti la Nipashe, Jumatani Aprili 5, 2017).
 
Kilichotokea jana bungeni kwenye uchaguzi wa Wabunge wa Bunge la Afrika Mashariki (EALA) limeonesha kwamba vyama vya siasa vya upinzani vina viongozi wababaisha kuhusu demokrasia wanayodai haipo nchini.

Wakati CHADEMA inawasilisha majina 2 tu, na ya wanaume tu, yapitishwe bila kupingwa, CUF iliwasilisha majina ya CUF Maalim na CUF Lipumba.

Ni haohao viongozi wanataka tuwaamini kama watetezi wa demokrasia kwa kumkebehi, kumkashifu na kuchonganisha Rais Magufuli kwa wananchi waliomwamini na kumpa dhamana, kwa kura, kuongoza nchi hii.

Najiuliza, hivi hao viongozi wa upinzani wangepewa hiyo dhamana ya kuongoza nchi hii, wangeweza kweli kuunda safu ya kutatua matatizo sugu ya nchi hii, kama siyo kupata tiketi ya kuyafanya kuwa sugu zaidi!

Matatizo sugu ambayo Rais Magufuli, kwa utashi wake wa kisiasa (political will) na uthubutu wake binafsi anayashughulikia kuyatokomeza, kwa madaraka aliyo nayo Kikatiba, ni pamoja na:
1) Uozo uliotukuka Serikalini ikiwa ni pamoja na urasimu, uzembe, rushwa, ufujaji wa mali ya umma, na matumizi mabaya ya madaraka - silaha yake KUTUMBUA .
2) Kutamalaki kwa ufisadi - silaha yake ZIARA ZA KUSHITUKIZA
3) Vita dhidi ya buashara ya madawa ya kulevya - silaha yake KUWATAJA HADHARANI WAHUSIKA.

Mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni Rais Magufuli.

Na viongozi wa vyama vya siasa vya upinzani, hasa CHADEMA, mabingwa wa siasa za mitandaoni, vyombo vya habari, majukwaani na maandamano, tambueni UHARAKATI umepitwa na wakati. WAKATI UKUTA USIGOMBANE NAO.

Viongozi wa vyama vya siasa upinzani "Mfanye siasa kwa uhuru wa kujieleza Kikatiba. Ikosoeni Serikali kinaga ubaga, bila kuangalia aliyeko nyuma yenu, ilimradi mnafanya hivyo bila kuingiza uchochezi au maneno ya kashfa kwa viongozi wa Serikali" (Gazeti la Nipashe, Jumatani Aprili 5, 2017).

Tatizo la kukosa protein ukiwa mdogo.Nipe Theluthi moja ya 2 halafu uniambie inawezekana vipi CDM kutoa theluthi moja y mbili??Kuiweka moja kwa moja maana yake.ni nusu.

Hesabu ni soma rahisi sana lakini linahitaji kutumia.CCM mmekurupuka mkidhani mnawakomoa CDM kumbe mnalikomoa Taifa.Upumbavu haulisaidii Taifa ubalidumaza.
 
Hizo ni nondo nilizowashushia, wanywa viroba watakuja na mitusi lakini ukweli unabaki ukweli

Eti nondo,nondo za akina Masogange ndiyo mnaziita nondo??

CCM kawadanganyeni Mateja Siyo watu wenye akili zetu.

Kama issue ya madawa Makonda marafiki zake wote ni drug lords pamoja na nyumba ndogo yake.

Kama issue ya Ufisadi Makonda anaongoza kwa kunyang'anya watu Mali zao na kufadhiliwa na GSM ambao ni wasafisha fedha.

Ukiongea habari ya usafiri Mwenyekiti mwenyewe ana Scandle ya Kivuko kibovu,Barabara mbovu, uhongaji wa Nyumba za Serikali kwa mahawara

Haya njoo na nondo sasa.

Kadanganye mateja wa UVCCM siyo sisi .
 
Yaani tangu hilo la jana litokee kila mwanauvccm anajitahidi kuanzisha uzi kuhusu siasa! daaaaa!
 
Tatizo Jf hakuna entry qualifications.kila Mwenye smart phone kama anajua kusoma na kuandika anajiunga! Pumba hizi zinaonesha huyu Ni darasa la saba B!
 
Tatizo la kukosa protein ukiwa mdogo.Nipe Theluthi moja ya 2 halafu uniambie inawezekana vipi CDM kutoa theluthi moja y mbili??Kuiweka moja kwa moja maana yake.ni nusu.

Hesabu ni soma rahisi sana lakini linahitaji kutumia.CCM mmekurupuka mkidhani mnawakomoa CDM kumbe mnalikomoa Taifa.Upumbavu haulisaidii Taifa ubalidumaza.

Usisome kwa kukariri.
 
Back
Top Bottom