Mloganzila kunani paleeee mbona...

Wanafunzi wa udaktari huanza mafunzo awali kwa kujifunzia cardavers( miili ya watu waliokufa ) halafu baada ya hapo hupata mafunzo darasani.
Wanapokuwa internships wanafunzi hao hufanya mafunzo na kazi huku wakiwa chini ya usimamizi maalumu wa madaktari walio senior kitaaluma kwao.

Dhana ya kwamba wanaotibu watu mloganzila ni wanafunzi haina mashiko ingawa dhana imejengeka kwa wengi.

Ukisomea ufundi makenika utajifunzia kwenye magari, ukisomea udaktari wa mifugo utajifunzia kwenye mifugo hali kadhalika kwa wanaosomea udaktari wa binadamu.
 
Poleni.
Kuna aina ya magonjwa na stage zake, kifo ndani ya muda fulani ni 99.9%.
Bahati mbaya sana magonjwa hayo mengi ndio yamewekwa Mlongazila.
Tusiangalie tu kifo Bali kimetokana na ugonjwa gani.
Tafauti ya vifo kutokana na kulazwa kwa ajili ya kujifungua au kuvunjika mguu vs advanced forms za magonjwa ya moyo, ini na saratani zake ni kubwa mno.
Kama kuna mapungufu yatajwe bayana yaani tuwe specific kuliko kuwa jumuishi.

Tukumbuke MNH/ Mlongazila Mara nyingi wanapokea wengi walio katika advanced stages za ugonjwa baada ya wao binafsi kuchelewa kuchukua hatua au kucheleweshwa kupewa rufaa kutoka hospital za mikoa. Kifo hapo ni matokea ya vingi
 
Unadhani ni kwa nini hospitali zingine hazilalamikiwi kuliko mlonganzila?

Cc Unforgetable
 
Mgonjwa akiwa ana hali mbaya anaonekana tuu, hata kama ni wa kufa hata kwa macho yasiyo ya kidaktari anaonekana tuu.

Sasa tuambie kwa nini hii mlogamzila inalalamikiwa sana? Kuna tatizo gani pale?


Cc Unforgetable
 
Mloganzila kunakufa watu km inzi. Na ni wazembe na wanyanyasaji kupindukia mbali na hizo gharama kuwa kubwa. Mgonjwa amekufa saa 7 mchana maiti inaachwa wodini hadi saa 12 usiku. Nilishawahi kuona mgonjwa aliyekufa usiku wa manane kulingana na taarifa aliyonipa mgonjwa wangu kuachwa mochwari hadi asubuhi wakati wa kuwaona wagonjwa. Watoto wa marehemu walipokaribia kitanda cha mama yao kumfunua wanakuta alishapoa mdaaa
Tena usiombe mgonjwa wako awe ameandikiwa kipimo yani usipokifwatilia mwenyewe utaisoma namba. Kinaweza kuchukua wiki nzima.
Mbali na specialists ambao wanafika pale kwa nadra sana ni kweli wanafunzi ndio wanatibu watu na kupita round.
Binafsi nimeona kwa macho yangu. Kuhusu mloganzila huniambii kitu paligeuka kuwa kuwa home
 

mbona huisemi bugando nayo ni hivyohivyo tu wanafunzi ndio hupasua wagonjwa na kujifunza kwa mgonjwa maiti kila siku anaenda hospitali anaongea anacheka mara mnaambiwa amefariki
 
Hili tatizo pengine lipo mahala pengi nchini

Mungu tu atunusuru
mbona huisemi bugando nayo ni hivyohivyo tu wanafunzi ndio hupasua wagonjwa na kujifunza kwa mgonjwa maiti kila siku anaenda hospitali anaongea anacheka mara mnaambiwa amefariki
 
Pole sana mkuu, wizara husika wachukue hatua aisee tutaidhalilisha hospital hivi hivi


Bora wadhalilike lakini viumbe wa Mungu wabaki na haki yao ya kuishi ba siyo kuwapunguza kijanja.

Usishangae wakaja na lawama kwa vifaa vilivyofungwa hapo hospital.
 
Kama Hospitali ni ya Rufaa kwa nini wasipelekwe Madaktari bingwa? Basi lawama ielekezwe kwa Wizara ya Afya.
 
Bora wadhalilike lakini viumbe wa Mungu wabaki na haki yao ya kuishi ba siyo kuwapunguza kijanja.

Usishangae wakaja na lawama kwa vifaa vilivyofungwa hapo hospital.
Hapo umenifumbua macho 🤨🤨🤨
 
Wanajamii mimi niko nje ya mada kidogo na nahitaji msaada. Nina tatizo la kutopata choo naweza kumaliza week mpaka siku 10. Sasa tatito linakuja pale nikipata choo naweza kuharisha mfurulizo siku mbili hadi nikinywa manji yanatoka kama yalivyo. Pili naharisha kama makamasi yakiambatana na damu. Asanten wakuu

Sent using Jamii Forums mobile app
 

It’s either amoeba or typhoid nenda hospital mkuu


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna jini mahaba lina penda ku do na marehemu

Sent from my SM-A105G using Tapatalk
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…