Adverse Effect
JF-Expert Member
- Oct 8, 2017
- 3,518
- 8,968
Ndio kati ya waliobeba mabegi na kuondoka ili wasipelekwe mloganzila?Wodi iligeuka kua uwanja wa mabishano kati ya aliyetoa maelekezo hayo na wagonjwa.....wengi walilalama kwamba hawawezi kwenda kule kufa
Rip loving anko... Mloganzila has a story to tell View attachment 1195675
Unadhani ni kwa nini hospitali zingine hazilalamikiwi kuliko mlonganzila?Wanafunzi wa udaktari huanza mafunzo awali kwa kujifunzia cardavers( miili ya watu waliokufa ) halafu baada ya hapo hupata mafunzo darasani.
Wanapokuwa internships wanafunzi hao hufanya mafunzo na kazi huku wakiwa chini ya usimamizi maalumu wa madaktari walio senior kitaaluma kwao.
Dhana ya kwamba wanaotibu watu mloganzila ni wanafunzi haina mashiko ingawa dhana imejengeka kwa wengi.
Ukisomea ufundi makenika utajifunzia kwenye magari, ukisomea udaktari wa mifugo utajifunzia kwenye mifugo hali kadhalika kwa wanaosomea udaktari wa binadamu.
Mgonjwa akiwa ana hali mbaya anaonekana tuu, hata kama ni wa kufa hata kwa macho yasiyo ya kidaktari anaonekana tuu.Poleni.
Kuna aina ya magonjwa na stage zake, kifo ndani ya muda fulani ni 99.9%.
Bahati mbaya sana magonjwa hayo mengi ndio yamewekwa Mlongazila.
Tusiangalie tu kifo Bali kimetokana na ugonjwa gani.
Tafauti ya vifo kutokana na kulazwa kwa ajili ya kujifungua au kuvunjika mguu vs advanced forms za magonjwa ya moyo, ini na saratani zake ni kubwa mno.
Kama kuna mapungufu yatajwe bayana yaani tuwe specific kuliko kuwa jumuishi.
Tukumbuke MNH/ Mlongazila Mara nyingi wanapokea wengi walio katika advanced stages za ugonjwa baada ya wao binafsi kuchelewa kuchukua hatua au kucheleweshwa kupewa rufaa kutoka hospital za mikoa. Kifo hapo ni matokea ya vingi
Habarini wakuu,
Kwa nyakati tofauti ndani ya jiji la Dar nilikua nikisikia tuhuma mbali mbali zinazotupiwa kwa hii hospitali yetu kubwa ya kisasa na yenye sifa za kimataifa
Nimesikia mara kadhaa kwa watu kwamba ukimpeleka mgonjwa wako pale kama ni serious case basi ujue atapotea tu
Minong'ono hii inakuja kwa dhana kuu mbili ambazo serikali hasa wizara ya afya naomba ifanye uchunguzi ili kubaini ukweli wake na kuleta ufumbuzi
Dhana ya kwanza ni kwamba madaktari wengi wa pale ni madaktari wanafunzi ambao hufanya mazoezi kwa vitendo kwa wangonjwa.......
Dhana hii imepelekea wagonjwa wengi wanaopewa rufaa ya kwenda kule kuikacha hospitali hiyo na kurudi majumbani
USHUHUDA: wiki kadhaa zilizopita nikikua pale muhimbili kumuuguza mgonjwa wangu ambaye hata hivyo aliamriwa na madaktari afanyiwe upasuaji tumboni ili kuondoa uvimbe aliokua nao
Jambo la kushangaza ambalo pia ndilo limenisukuma kuandika mada hii ni baada ya ndugu yangu huyo pamoja na wagonjwa wengine kama kumi na tano waliokua wodini hapo kupewa rufaa ya kwenda hospitali ya mloganzila
Wodi iligeuka kua uwanja wa mabishano kati ya aliyetoa maelekezo hayo na wagonjwa.....wengi walilalama kwamba hawawezi kwenda kule kufa
Ghafla niliona wagonjwa hao wanafungasha mabegi na kusepa bila kwenda walikoamriwa
Dhana ya pili ni gharama kubwa ambayo inalalamikiwa hospitalini hapo ambayo pia inawafanya wagonjwa wapakimbie
Kwa kua haya ni maneno yanazungumzwa kwa wingi, naiomba wizara husika ichunguze jambo hili kwa makini
Nawasilisha
Hapana yeye alitokea Tumbi
mbona huisemi bugando nayo ni hivyohivyo tu wanafunzi ndio hupasua wagonjwa na kujifunza kwa mgonjwa maiti kila siku anaenda hospitali anaongea anacheka mara mnaambiwa amefariki
Pole sana mkuu, wizara husika wachukue hatua aisee tutaidhalilisha hospital hivi hivi
Hapo umenifumbua macho 🤨🤨🤨Bora wadhalilike lakini viumbe wa Mungu wabaki na haki yao ya kuishi ba siyo kuwapunguza kijanja.
Usishangae wakaja na lawama kwa vifaa vilivyofungwa hapo hospital.
Wanajamii mimi niko nje ya mada kidogo na nahitaji msaada. Nina tatizo la kutopata choo naweza kumaliza week mpaka siku 10. Sasa tatito linakuja pale nikipata choo naweza kuharisha mfurulizo siku mbili hadi nikinywa manji yanatoka kama yalivyo. Pili naharisha kama makamasi yakiambatana na damu. Asanten wakuu
Sent using Jamii Forums mobile app