Mliopitia mlifanyaje?

Kiminyio 01

JF-Expert Member
Joined
Aug 3, 2018
Posts
1,399
Reaction score
2,035
Nawasalimu

Nina mambo mawili ningelipenda kupokea ushauri kutoka kwenu wana jamvi.

Binafsi napenda kujitolea kwa ajili ya wengine, kwa vyovyote vile na endapo sitakua na kitu nitamuombea kimoyoni moyoni Mungu akampe heri kile na kule anapoenda kukamilisha.

Pamoja na msaada wangu na kujitoa kwa ajili ya wengine ninapokwama, msaada wa karibu kwangu unakua mzito sana kupewa. Je, hili suala hat ninyi hua mnakuta na nalo?

Mara nyingi fedha yangu hupotea katika matumizi nisiyoyaelewa; mambo yangu hayakamiliki. Nafanya saving, nimejiingiza ktk vicoba 'ninafanya biashara vyote navyofanya, am nothing.

Wakati wanajamvi mnapitia situation kama hizi mlipitaje na kukabiliana na challenges?

Napitia comment zenu, ahsanteni.
 
Jitahidi kuachana na utoaji usio kuaidia hata kama unapenda. Wema usizidi uwezo.
2. Umesema unafanya matumizi usiyoyaelewa ili hali unasave acha matumizi yasiyo ya lazima. Save na wekeza kwenye uzalishaji.
3. Hivyo vikoba jaribu kupunguza baki na kimoja cha maana au achana navyo ukishapata mtaji wa biashara.
4. Focus kwenye biashara ya maana ambayo utaisimamia seriously. Tunza hesabu na acha matanuzi.Kuza biashara utafanikiwa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Weka kumbukumbu kwa kuandika, kila unachopata na unachotoa. Jipe muda halafu upitie na kuangalia wapi ni chanzo kizuri cha mapato na wapi ni kwenye matumizi makubwa au yasiyo ya lazima. Jirekebishe kutokana na uliloliona, jitahidi kuweka akiba na kuwekeza zaidi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nakazia tuu Main points za wachangiaji wa juu..
1. Mjali anaekujali/Mjali anae jalika,
2. Wema usizidi uwezo,
3. Epuka Matumizi makubwa yasio ya lazima(wekeza)
 
Kumbuka kumtolea Mungu pia omba kuvunja roho wa chumaulete anafanya kazi kwa njia za ajabu kama ulivyotaja. Vunja hii roho.
 
Badilika hivo ulivyo hupaswi kuwa hivo...
 
hapo kwenye kijitolea kwa wengine wakat wewe hupat msaada toka kwao ndio kosa lilipo

my friend ukitaka kufanikiwa kua na roho mbaya tu mjali anaekujal asiekujal tupa mbali.
Roho mbaya nayo ni kipaji ujue. Mimi kuna mama mmoja alinifanyia ukatili sana ukatili sana. Yaani ni unyama na ilikuwa mwaka jana kipindi cha ramadhan kama hiki.
Mwaka huu kafiwa na mume wake nikajikuta tu namsaidia na nikajikuta tu kiasi fulani cha akiba yangu nimempa halafu nilivyokuwa kenge ile akiba nikampa nusu na nusu nikabaki nayo.
Baadae sana nikasema mimi si ndo nilisema huyu mtu hatogusa sent 5 yangu tena?


mama wawili
 
Mama Wawili!!
 
Reactions: amu
Roho nzuri huwa inalipa, siyo lazima leo! Saidia unapoweza. akili isikupeleke kwenye ushirikina, hapo utakuwa umepotea kimoja. Tulia fikiria matumizi yako yasiyofaa, tunza kumbukumbu vizuri, ongeza bidii, kila la heri! Miungu yupo usimsahau asilani.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hata mimi napitia hali hiyo Ila bibi yangu alisema usichoke kujitoa kwaajili ya wengine

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mm hua nasaidia sana watu ila pia hua sipati misahada ninapo kwama hua sijui sababu na wale nilio wasaidia hua hawapo tena karibu ktk kpnd hiko hua najitahidi ku act roho mbaya ila nashndwa kabisa sometymz nakua na huruma sana ila hua sieleweki wala kuonewa huruma na hata nikijitahd ku act tofauti nashndwa sijui ni ugonjwaaa ina nipa shida sana hii
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…