Mkuu wa Mkoa kuhamasisha umma kufuatilia makabidhiano ya ripoti ya pili ya Mchanga wa Dhahabu!

vicdala55

JF-Expert Member
Sep 24, 2010
1,009
1,638
Kuna juhudi kubwa zinafanyika kuwahamasisha Wananchi kesho waache shughuli zao na kukaa mbele ya luninga kufuatilia matangazo ya moja kwa moja ya makabidhiano ya ripoti ya pili ya tume iliyoundwa juu ya sakata la mchanga wa Dhahabu!
Mkuu wa mkoa mmoja usiku huu ametoa gari la matangazo linapita mitaani kuhamasisha umma kufuatilia tukio hilo bila kukosa!
Sina tatizo na juhudi hizi za Mkuu wa mkoa, tatizo langu ni nini hasa malengo ya jitihada hizi?
Yapo maswali mengi yanajitokeza, kwa nini jitihada hizi hazipo kwenye kuwataka Wananchi wafuatilie mijadala ya bungeni?
Kwa nini jitihada hizi zisifanywe kwa kuwataka Wananchi waulizie ilipo mikataba mbalimbali iliyopelekea Taifa kupata hasara kubwa katika sekta mbalimbali?
Kwa nini Wananchi wanatakiwa waache kazi zao kufuatilia makabidhiano ya ripoti hii badala ya umma kuelezwa ni kina nani waliolifikisha hapa Taifa hili?
Je, maelekezo haya yametolewa kwa wakuu wote wa mikoa? Kama jibu ni ndiyo, lengo hasa ni lipi?
Je, kuna nini 'special' katika ripoti hiyo?
Je, hii ripoti tayari inajulikana kwa wakubwa kiasi cha kutaka umma uhamasishe kuifuatilia?
Siamini serikali inaweza kufanya uhamasishaji mkubwa kiasi hiki pasipo kujua kilichomo ndani ya ripoti!
Lkn swali muhimu kabisa ni hili, Je, kipi muhimu kwa Umma kukijua kati ya ripoti hii na mikataba inayoleta matatizo yote haya?
 
Wala haiitaji kuhamasisha bali huku mtaani watanzania wanasubiri kwa hamu kubwa kusikia hiyo report ya Tume ya pili ya makinikia.

Wengi wao wanasema Sasa Kuna Rais asiyetaka mzaha wala masihara na wanaoiharibu nchi ya Tanzania kwa kushirikiana na wawekezaji wasio waaminifu.
 
Kuna juhudi kubwa zinafanyika kuwahamasisha Wananchi kesho waache shughuli zao na kukaa mbele ya luninga kufuatilia matangazo ya moja kwa moja ya makabidhiano ya ripoti ya pili ya tume iliyoundwa juu ya sakata la mchanga wa Dhahabu!
Mkuu wa mkoa mmoja usiku huu ametoa gari la matangazo linapita mitaani kuhamasisha umma kufuatilia tukio hilo bila kukosa!
Sina tatizo na juhudi hizi za Mkuu wa mkoa, tatizo langu ni nini hasa malengo ya jitihada hizi?
Yapo maswali mengi yanajitokeza, kwa nini jitihada hizi hazipo kwenye kuwataka Wananchi wafuatilie mijadala ya bungeni?
Kwa nini jitihada hizi zisifanywe kwa kuwataka Wananchi waulizie ilipo mikataba mbalimbali iliyopelekea Taifa kupata hasara kubwa katika sekta mbalimbali?
Kwa nini Wananchi wanatakiwa waache kazi zao kufuatilia makabidhiano ya ripoti hii badala ya umma kuelezwa ni kina nani waliolifikisha hapa Taifa hili?
Je, maelekezo haya yametolewa kwa wakuu wote wa mikoa? Kama jibu ni ndiyo, lengo hasa ni lipi?
Je, kuna nini 'special' katika ripoti hiyo?
Je, hii ripoti tayari inajulikana kwa wakubwa kiasi cha kutaka umma uhamasishe kuifuatilia?
Siamini serikali inaweza kufanya uhamasishaji mkubwa kiasi hiki pasipo kujua kilichomo ndani ya ripoti!
Lkn swali muhimu kabisa ni hili, Je, kipi muhimu kwa Umma kukijua kati ya ripoti hii na mikataba inayoleta matatizo yote haya?
Hiyo itakuwa inajulikana angalau kwasasa kuongozwa kwa matamko kumepungua baada ya kuwa kemea Watanzania kale kaugonjwa kasiko kuwa na dawa kapo sana 'kaugonjwa ka kusahau'
 
Hiyo yote ni kufunika bajeti kivuli ya upinzani,
Aayo bila Shaka itawasilishwa siku ya kesho..
So ni kuwatoa kule na kiwaleta mchangani.
We hiyo bajeti kivuli itatusaidia nini. Kwwnye mambo siriaz unaleta mchezo wa kitoto. Khaaaaa !
 
Si wawaalike wanaowashutumu na kuwapa nafasi ya kuuliza pamoja na waliotia sign mikataba.
 
Back
Top Bottom