Mkurugenzi wa Muhimbili, Dr. Delilah aongoza huduma za uchunguzi na matibabu ya kibingwa Kilosa, Morogoro

Mkurugenzi wa Muhimbili, Dr. Delilah aongoza huduma za uchunguzi na matibabu ya kibingwa Kilosa, Morogoro

Kayugumis

Senior Member
Joined
Jun 6, 2022
Posts
140
Reaction score
126
Katika kuhitimisha siku mia za uongozi wa Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan ambaye alielekeze huduma za matibabu ziwafikie wananchi popote walipo, Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili, Dkt. Delilah Kimambo, ameendelea kuwa kiongozi wa mfano kwa kusimamia na kutekeleza maagizo hayo kwa kufanya kambi maeneo mbalimbali nchini ambapo kwa sasa kambi hiyo imetia nanga Wilayani kilosa.

Kambi hiyo ya uchunguzi na matibabu ya kibingwa bobezi inayofanywa na Hospitali ya Taifa Muhimbili kwa kushirikiana na Vodacom Foundation Tanzania imeanza leo Machi 10, 2026 ambapo huduma za uchunguzi wa saratani ya shingo ya kizazi na matiti, saratani ya tezi dume, magonjwa ya uzazi na kina mama, masikio, pua,koo meno na magonjwa ya Watoto zinafanyika bila malipo.
649630042_18114591559727681_521734588123992686_n (1).jpg
 
Back
Top Bottom