Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mpanda vijijini (Tanganyika) ni jipu, mamlaka zimfuatilie

KingJoh

Member
Oct 20, 2019
12
11
Ni matumaini yangu kuwa Mungu yu pamoja nanyi akiwalinda ili kutekeleza majukumu ya kila siku.

Nadhani ni vyema nikienda moja kwa moja kwenye mada.

Itakumbukwa kuwa, hapo jana wakati Mh Rais akiwaapisha Mawaziri na Manaibu, aligusia kuhusu mambo ya hovyo yanayoendelea katika Halmashauri ya Geita na Manispaa ya Mpanda yamkini yakiongozwa na Wakurugenzi wenyewe. Hii ni hatua nzuri sana na nipongeze kwa Serikali inayoongozwa na Dkt. John Pombe Joseph Magufuli kuliona hilo.

Lakini nipende kutoa taarifa ya kuwa, kuna Halmashauri inaitwa Mpanda Vijijini au Tanganyika, kuna uozo uliopitiliza kufikia kiwango kwamba, wananchi wanahisi Mkurugenzi anatumia dawa wakiangalia wengine wakitumbuliwa kwa makosa madogo kuliko yeye unayoyafanya lakini bado hajaingia anga za Mh Rais.

Niseme tu ukweli mkurugenzi huyu anayeitwa Romuli ni jipu na ndiye mpinga maendeleo NO1 kwa wilaya ya Tanganyika.

1. Ikumbukwe kuwa Waziri Mkuu aliutembelea mkoa wa katavi mwaka huu, na akapita eneo la karema akikagua maendeleo ya ujenzi wa bandari ya karema. Alipata fursa ya kuwahutubia wananchi wa maeneo ya karema na moja ya point aliyoisema, ilihusu kujengwa kwa shule ya sekondari isengule kwa kutumia hela zilizopatikana kwa kuuza magogo ambayo yalitaifishwa na serikali na ilitarajiwa ujenzi wa hiyo shule sambamba na ujenzi wa hospitali na fedha tukaambiwa zipo. Cha kushangaza, miradi hiyo wala haiendelei kwa kile kinachodaiwa kuwa hela imeshapigwa na wajanja wa mjini wakiongozwa na mkurugenzi.

2. Mkurugenzi amekuwa akifanya re-allocation hela za watumishi kwa matumizi ya kipuuzi kabisa. Kwamfano, kuna hela ya kujikimu ilitumwa na serikali kwa ajili ya walimu intake ya mwaka jana mwezi wa nne kama sikosei, mkurugenzi alizichukua na kuzinunulia mafuta ili afanye ziara zake ambazo ofcoz znaweza kuwa na tija lkn tatizo ni, hakuonai
huruma kwa hao walimu ambao walikuwa katika hali mbaya kiuchumi?? Lkn pia, kuna walimu wameajiriwa mwaka 2017 mwezi wa nne, mpka leo hawajapewa hela za kujikimu ambazo wengine nchi hii wameshalipwa, kwanini halmashauri hii?

3. Kuna miungu watu kwny idara ya fedha pale halmashauri wakikingiwa kifua na mkurugenzi. Ni wadada wawili ambao wamekuwa na majibu mabaya sana kwa watumishi. Unakuta mwl mkuu anafuatilia hela kwa ajili ya shule, anatumia siku nne kukamilisha process na ukiangalia hakuna sababu ya msingi coz, halmashauri zinngne ambazo zipo karibu hawatumii muda wote huo. Kwnn halshauri hii?

4. Conclusively, hakuna alilolifanya kwa utawala wake.

Niiombe serikali, halmashauri hii, inatakiwa kukaguliwa pia na kwa mimi ninavyoona, hii ndio halmashauri yenye madudu kuliko halmashauri zote nchini.

Waziri nitafurahi sana kama utaipitia hii
 
Vp ule mwalo wa ikola unapiga kazi..kitambo sana sijaingia kipande icho..sekondar isengule ilikua jambo muhimu mana isengule nikaribu zaid na ikola naviijiji vya ndani ndani uko
 
Mkurugenzi na mkuu wa wilaya Tanganyika ni Kama paka na panya... Ila DC anapiga kazi tatizo limkurugenzi naskia anavimba ile mbaya!

Nimekaa Kibo miez Kama4 hiv kwa ndugu ... daa maskendo ya mkurugenzi ni hatar!
 
Mkurugenzi na mkuu wa wilaya Tanganyika ni Kama paka na panya... Ila DC anapiga kazi tattizo limkurugenzi naskia anavimba ile mbaya!
Nimekaa Kibo miez Kama4 hiv kwa ndugu ... daa maskendo ya mkurugenzi ni hatar!
mkurugenzi yuko sahihi sana katika baadhi ya maamuzi yake mkuu wa wilaya ana matatizo sana

akikosana na mtu kutokana na chuki za kibwege anataka kumuamisha (tangu lini mkuu wa wilaya akamuamisha mtu) mfano alishinikiza afisa ushirika aliye mjuvi akahama wilaya ya tanganyika na kuleta afisa ushirika asije mzuri (kwa vile anamsikiliza na kumtii)

Alitaka muhamisha afisa ugani kata ya Tongwe na kumleta dogo rafiki yake ili kufanikisha upigaji katika zao la pamba

mkuu wa wilaya ana makando kando kibao, sema vile mkurugenzi sio mwongeaji ye anafanya kazi tu ajawekeza kwenye majungu basi anaonekana anavimba

yule bwana ni mfatiliaji sana nimewahi hudhuria kikao na watendaji wa vijiji,kata jamaa anauliza miradi inavyo endeleo huko watendaji walikuwa wanatoa takwimu/taarifa za uwongo lile bwana linawaumbua ila kusema jamaa mpigaji ama mkuu wa wilaya anapiga kazi ni uongo mtupu jamaa ni kanjanja
 
Kazi aliyeifanya Mbunge Msukuma ya kufichua matumizi mabaya ya mkurugenzi wa Geita ni yakishujaa sana namuomba aendelee kuwafichua wengine nchi nzima maana yeye ni rahisi kusikika.

Wakurugenzi wa namna hii ndio chanzo cha kuchonganisha serikali na raia, ni kama wanamuhujumu Mh. Rais. Kama mtu mmoja anaweza kuwanyima mamia ya walimu hela ya kujikimu kwa matakwa yake mwenyewe, wakati hela serikali ishatoa hili jambo sio la kufumbiwa macho.
 
mtoa mada kaleta porojo tu

1. Pesa iliyotokana na uuzaji wa magogo/ faini na uuzaji wa mkaa kwa wasio na kibari nilimsikia Mkuu wa mkoa ndg J.Z Homera siku ya ufunguzi wa stendi iliyopo Tanganyika (jirani na ofisi za h/mashauri ya Tanganyika ) akieleza mgawanyo wake na matumizi yake kusema eti mkurugenzi kaipiga ni uongo wa wazi.Tena nakumbuka mkuu wa wilaya aliomba fedha kiasi zirudi kuimarisha ulinzi na doria kwa wanaovuna magogo/ mkaa bila kibari

kwa iyo hela mkurugenzi kuila lazima awe na roho ngumu ya kujifunika shuka moja na nyoka,maana mkuu wa wilaya anaifahamu (na ndiye alikamata roli 2 za mkaa ), mkuu wa mkoa anaifahamu na alisha elekeza ifanye kazi gani?

3. Madai ya miungu watu ni vile walimu mnakuwa hajiamini tu wala hakuna kukingiwa kifua acheni woga

4. Hakuna alilofanya yawezekana ni kweli ila chini yake nimeona kiwanda cha kuchakata pamba kimejenngwa (juhudi kubwa yeye na mkuu wa wilaya), kagawa mbegu za ufuta na stakabadhi gharani iliwezekana kiasi (japo ilikuwa na mapungufu), ujenzi wa hosp, umekamilia, naona vikundi vya vijana wanapewa mikopo.

sina hakika sana na hizi tuhuma ila wahusika wasipuuzie wazichunguze japo naona zimekaa kimajungu majungu
 
Am sure,
mtoa mada kaleta porojo tu

1. Pesa iliyotokana na uuzaji wa magogo/ faini na uuzaji wa mkaa kwa wasio na kibari nilimsikia Mkuu wa mkoa ndg J.Z Homera siku ya ufunguzi wa stendi iliyopo Tanganyika (jirani na ofisi za h/mashauri ya Tanganyika ) akieleza mgawanyo wake na matumizi yake kusema eti mkurugenzi kaipiga ni uongo wa wazi.Tena nakumbuka mkuu wa wilaya aliomba fedha kiasi zirudi kuimarisha ulinzi na doria kwa wanaovuna magogo/ mkaa bila kibari

kwa iyo hela mkurugenzi kuila lazima awe na roho ngumu ya kujifunika shuka moja na nyoka,maana mkuu wa wilaya anaifahamu (na ndiye alikamata roli 2 za mkaa ), mkuu wa mkoa anaifahamu na alisha elekeza ifanye kazi gani?

3. Madai ya miungu watu ni vile walimu mnakuwa hajiamini tu wala hakuna kukingiwa kifua acheni woga

4. Hakuna alilofanya yawezekana ni kweli ila chini yake nimeona kiwanda cha kuchakata pamba kimejenngwa (juhudi kubwa yeye na mkuu wa wilaya), kagawa mbegu za ufuta na stakabadhi gharani iliwezekana kiasi (japo ilikuwa na mapungufu), ujenzi wa hosp, umekamilia, naona vikundi vya vijana wanapewa mikopo.

sina hakika sana na hizi tuhuma ila wahusika wasipuuzie wazichunguze japo naona zimekaa kimajungu majungu
Ww
mtoa mada kaleta porojo tu

1. Pesa iliyotokana na uuzaji wa magogo/ faini na uuzaji wa mkaa kwa wasio na kibari nilimsikia Mkuu wa mkoa ndg J.Z Homera siku ya ufunguzi wa stendi iliyopo Tanganyika (jirani na ofisi za h/mashauri ya Tanganyika ) akieleza mgawanyo wake na matumizi yake kusema eti mkurugenzi kaipiga ni uongo wa wazi.Tena nakumbuka mkuu wa wilaya aliomba fedha kiasi zirudi kuimarisha ulinzi na doria kwa wanaovuna magogo/ mkaa bila kibari

kwa iyo hela mkurugenzi kuila lazima awe na roho ngumu ya kujifunika shuka moja na nyoka,maana mkuu wa wilaya anaifahamu (na ndiye alikamata roli 2 za mkaa ), mkuu wa mkoa anaifahamu na alisha elekeza ifanye kazi gani?

3. Madai ya miungu watu ni vile walimu mnakuwa hajiamini tu wala hakuna kukingiwa kifua acheni woga

4. Hakuna alilofanya yawezekana ni kweli ila chini yake nimeona kiwanda cha kuchakata pamba kimejenngwa (juhudi kubwa yeye na mkuu wa wilaya), kagawa mbegu za ufuta na stakabadhi gharani iliwezekana kiasi (japo ilikuwa na mapungufu), ujenzi wa hosp, umekamilia, naona vikundi vya vijana wanapewa mikopo.

sina hakika sana na hizi tuhuma ila wahusika wasipuuzie wazichunguze japo naona zimekaa kimajungu majungu
Ww utakuwa n mtumishi tena uanyenufaika na udhalimu wa mkurugenzi. To be honest, jarib kufatilia hvyo vitu, mm nlikuwa huko 1week ago, na nikuambie tu, mm wala sio mwalim na sio mtumishi, hzo issue za kutokujiamn wapelekee walim huko. Lkn mm nazungumzia the reality. Mwakani nitakuwa huko tena, kwa week mbili mwez wa3, hvi vitu nlivovisema, tutaona kama vitakuwa vimetekelezwa
 
Am sure,
Ww
Ww utakuwa n mtumishi tena uanyenufaika na udhalimu wa mkurugenzi. To be honest, jarib kufatilia hvyo vitu, mm nlikuwa huko 1week ago, na nikuambie tu, mm wala sio mwalim na sio mtumishi, hzo issue za kutokujiamn wapelekee walim huko. Lkn mm nazungumzia the reality. Mwakani nitakuwa huko tena, kwa week mbili mwez wa3, hvi vitu nlivovisema, tutaona kama vitakuwa vimetekelezwa
Ndo maana nimekwambia umeleta porojo tu, mambo ya kusikia vijiweni kuhusu kuwa mtumishi si kweli fatilia michango yangu utagundua huwa nafanya kazi zangu tu.

umekiri mwenyewe huwa haukai huku ko mengi yanayo fanyika huyajui zaidi ya kupewa stori za vijiwe

Niseme kitu hpa sasa hivi naenda chukua miche ya korosho pale kitalu cha mchaka mchaka naipeleka kupanda shambani tanganyika ko yanayo tokea kiasi nakuwa nayafahamu


kwa unoko wa mkuu wa wilaya salehe muhando na unaa wa R.C Homera ule mkwanja walio utafuta wao na wakaupangia matumizi
 
Back
Top Bottom