Mkopo wa Pesa kwa gari

Mkopo wa Pesa kwa gari

Yaani ukopeshwe hela halafu umtask aliyekukopesha tena afanye biashara na gari yako? Hauko serious ndugu
 
Wakuu, mimi nina Gari yangu Toyota Spacial Old medel, Hii gari inadaiwa na mtu Tsh Laki sita .

Sasa nilikuwa nataka mtu anikopeshe hizo laki sita then nimwachie gari afanyie biashara yake yoyote ambayo atapata faida ya milion moja then anirudishie gari yangu.

Tuandikishiane kila kitu kwa wakili au mahakamami.

Yoyote ambae anaweza kunisadia kwa ilo anipm.

Napata mashaka kama gari ni lako,maana hata jina la gari lako hulijui?

Upande wa Pili,inaonekana sio mzoefu saana wa kukopa au kunamashaka kwenye dili lote,na usipokuwa makini utapigwa na watu wachukue gari kwenye Mkataba.Au kuna dalili pia ya mtu kupigwa hapa.

Mie binafsi,naamini gari ya kutembelea kwa jiji la Dar ni anasa,Sasa nakushauri Uza gari lako,utatue matatizo yako.Kisha utanunua tena mbele ya Safari.
Maana suala tu la kukopa laki sita,na kumuambia mtu aigeuze taxi ili apate hela yake,ni kwamba wewe mwenye huna matarajio ya kupata laki sita za kurejesha.Inatia shaka sana hapa.

Kimfaacho mtu chake,kuuza chako si ujinga,ila kukutwa na fedheha na unacho cha kukusaidia ni ujinga zaidi.
 
Wakuu, mimi nina Gari yangu Toyota Spacial Old medel, Hii gari inadaiwa na mtu Tsh Laki sita .

Sasa nilikuwa nataka mtu anikopeshe hizo laki sita then nimwachie gari afanyie biashara yake yoyote ambayo atapata faida ya milion moja then anirudishie gari yangu.

Tuandikishiane kila kitu kwa wakili au mahakamami.

Yoyote ambae anaweza kunisadia kwa ilo anipm.

Kwa hesabu zako hiyo laki sita itapatikana baada ya muda gani?
Na kama gari ikiibiwa (labda wewe mwenyewe usuke mipango?) Itakuwaje?:smokin:
 
KUwa smart kwenye mkataba gari yaweza ibiwa ikiwa mkononi mwako
Halafu ukapata kesi:deni mpyaaa
Huu ni mji:smokin:

Nimejifunza kitu kwa hii Comment yako,aisee mji siku hizi umeharibika.
Ndio maana jamaa ametoa mwanya wa kufanya kazi ili ilipe.Maana uandishi tu inaonekana ametoka Kanda ilee.
Maana hata gari kuiandika jina anachapia,na option ya yeye kuweka bond kisha baadae alipe ameikwepa.

Hapa ataumizwa mtu vibaya mno.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom