Mkoa gani unaongoza kwa gharama kubwa za maisha?

Mnaosema Dar es salaam, kwa maoni yangu kwenye jiji hili gharama inategemea na style yako ya maisha. Unaweza kuishi kwa buku 2 au laki 8 kwa siku ni wewe tu, karibu sana.
 
Arusha gharama za maisha ni kubwa labda kutokana na utalii na madini,dodoma serikali iliuharibu kwa promo zisizo na uhalisia, mtwara na lindi maisha si tu ni ghali,bali ni magumu in general,nadhani location yake inachangia.
 
Mikoa yote wanakochimba madini maisha ni ghali sana...Geita wali na maharage shs 5,000 wakati kule kwa wadigo Tanga wali maharage sh. 1,000
.


.
Geita maisha yako cheap sana, huo mkoa una ardhi yenye rutuba nzuri hivo mazao mengi yanastawi sana, pia unapakana na mikoa ya Kagera na Kigoma ambayo ni inazalisha na kusafirisha vyakula vingi kwa Geita.
Nimeishi Geita miaka kama 8 hivi hakuna sehemu wanauza wali maharage kwa elf 5, ni elf 1- 2 kulingana na eneo. Ukishindwa maisha Geita basi jitafakari
 
Wanaosema Arusha nadhani hawajazunguka hilo jiji vizuri. Sehemu kama sombetini, shauri moyo, ungalimited, enaboishu, ngaramtoni, olasiti, kisongo na mwanama kote huko maisha ni rahisi sana ukiwa na buku 2 unakula siku nzima. Vyumba single vipo mpaka vya 15k.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…